Kwanini wananchi wana chuki kubwa na Jeshi la Polisi?

Kwanini wananchi wana chuki kubwa na Jeshi la Polisi?

Luka 3:
Luke

14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.

14 Likewise the soldiers asked him, saying, "And what shall we do?" So he said to them, "Do not intimidate anyone or accuse falsely, and be content with your wages."
 
Wanadhulumu raia mali zao?

Wanabambikia raia kesi?

Wanachukua rushwa kwa nguvu?

Wanapiga raia hovyohovyo?

Wananachukua wake za watu kwa nguvu?

What' s wrong with PT?
Kama IGP ndie kiongozi wa kuagiza watu wauwawe, una tegemea raia wawe na mapenzi na polisi?

Kama Igp ndie kinara wa kufungulia watu kesi za kutunga una tegemea nini kwa raia?

Kama Igp hamtii hata Rais wake je kuna haja ya polisi kuheshimiwa? Kama polisi ndio wanaongoza kwa kupokea rushwa je! Una tegemea muitikio gani toka kwa raia?
 
Na wanakwambia kabisa ukiingia selo ni bure ila kutoka ni hela, yaani sehemu ya usalama imekuwa sio salama
 
Ni baadhi tu yao tena ni wachache sana.
Polisi wengi ni weredi sana na wana busara nyingi.

Licha ya kuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu sana ni wavumilivu sana.

Nalipongeza sana Jeshi la Polisi kwa Utumishi Uliotukuka.
 
Umewauliza Wananchi wote wa Tz wamekujibu hivyo? Au ni halmashauri ya Kichwa chako pekee ime conclude hivyo..!! Kuna jamaa hiyo kitu ikikutokea wanaita 'Hallucinations'....! Iwapo itaendelea watakuita Mgonjwa Wa Akili..Be careful.
 
Sure.

Polisi wetu wanafanya kazi masaa 24. hakuna kulala iwe Mvua liwe Jua.
Tena kazi hatari za kupambana na Wahalifu wa aina zote ili kumlinda Mwananchi wa Mjini, Vijijini na Vitongoji vyake vya mbali sana huko.
Usiku wa manane wako kazini iwe Mvua Liwe Jua.
Na maisha yao tunayaona yalivyo duni sana.
Kipato chao ni duni.

Kazi ya Jeshi liwe la Polisi
ni ya kujitolea tu, malipo yao ni kama Posho tu ya Asante kwa kazi ngumu.
Kwa nchi zetu za dunia ya Tatu na ya Pili, tunashindwa kuwalipa watumishi wa Jeshi la Polisi sawasawa na kazi zao.
Kutokana na Uchumi mdogo.
 
Hili jeshi la polisi limeharibiwa na serikali ya ccm. Serikali inafahamu vizuri sana namna jeshi hili linavyonyanyasa raia kwa kuwatesa na kuwabambikia vyesi feki.

Lakini serikali haiwezi kusema chochote kwani wanaona jinsi jeshi hili linavyowahangaikia wakati wa uchaguzi na kuwafanya wapate "Ushindi wa Kishindo", hivyo serikali haina namna inabidi wawafumbie tu macho.

Hili jeshi la polisi wakati wa uchaguzi na hata baada ya uchaguzi, wako tayari kufa lakini ccm ibaki madarakani kwa njia zozote zile yaani punda afe lakini mzigo ufike.
 
Hii yote ni kwasababu wanawawezesha watawala kukandamiza yeyote wanaetaka akandamizwe kwa faida yao.
Hivyo watawala hawana sauti kwa jeshi hili kwa kulipa fadhila.
Jeshi ili libadilike, ni wananchi wanao nyanyasika na kukandamizwa waamuke. Ila kuamuka kwa wanyonge wasio na silaha ni ngumu, kinachohitajika ni kupata msaada toka nje kwa wenye silaha kama za hawa polisi.
 
Sure.

Polisi wetu wanafanya kazi masaa 24. hakuna kulala iwe Mvua liwe Jua.
Tena kazi hatari za kupambana na Wahalifu wa aina zote ili kumlinda Mwananchi wa Mjini, Vijijini na Vitongoji vyake vya mbali sana huko.
Usiku wa manane wako kazini iwe Mvua Liwe Jua.
Na maisha yao tunayaona yalivyo duni sana.
Kipato chao ni duni.

Kazi ya Jeshi liwe la Polisi
ni ya kujitolea tu, malipo yao ni kama Posho tu ya Asante kwa kazi ngumu.
Kwa nchi zetu za dunia ya Tatu na ya Pili, tunashindwa kuwalipa watumishi wa Jeshi la Polisi sawasawa na kazi zao.
Kutokana na Uchumi mdogo.
Acha kuzuga watu wewe.
 
Police hawatumikii tena wananchi bali ni chama tawala, pia upigaji, wamekuwa wapiga dili inafika mahala adi wanadhurumu haki za wanyonge

Ushauri wangu WAUAWE tu, hawana msaada kwa jamii.
 
Back
Top Bottom