Mkuu mimi ni kilaza tu wa haya makitu niliyakimbiaga kitambo olevel
Sijawahi kuisikia hiyo theory yako na wengi wetu humu labda ndio tunaanza kuisikia............Kama ya Newton yenyewe ilituchanganya darasani itakua hii umeigusia tu hapa
Labda aje mjuzi anayielewa
Lakini......
Kama law ya Newton inasema vitu vinavutwa chini na gravity, na hii chupa ikiwa imeshikiliwa huoni kwamba ina maanisha ukitoboa chupa maji yatapata pakuvutwa na na hiyo gravity?
Na unapo iachia chupa itamaanisha sasa maji na chupa vyote vina vutwa na gravity kwenda chini.......kwa muktadha huo inamaana sasa gravity haita vuta tena maji kupita matundu ya chupa kwakuwa chupa na maji vyote sasa vinavutwa chini
Hapa twende ki layman layman kama itawezekana
Wewe unatumia hoja gani kwamba kwakuwa maji yanaacha kutoka kwenye matundu kuhalalisha hayavutwi na gravity?
Hatuwezi kuikwepa kuirejea gravity kwasababu ndio inayojulikana kwa sasa
Kwa mujibu wa Newton mvuto wa kwenda chini unategemea na uzito wa kitu mfano wa lift iwapo lift itafeli na kuanza kuvutwa kwenda chini itategemea ndani ya lift kuna nini
Kama kuna vitu vyepesi kuliko lift inamaana kadiri umbali ulivyo ndivyo hivi vitu vitaonekana vinaelea kwenye lift kwasababu lift itavutwa kwa speed kubwa kuliko vitu vyepesi
Na ikiwa ndani ya lift kuna vitu vizito kuliko lift basi vitaongeza speed ya lift kwenda chini na havitaonekana kuelea
Sioni ni wapi huu mfano wako unapingana na law ya Newton
Nisaidie kuelewa ni nini kilipaswa kutokea kwa mujibu wa mifano yako ili sasa kuthibitisha gravity ipo
Kitu kinachochanganya hapa ni Ku assume existence ya Gravitation ili kuelezea Gravitation
Tutazame mfano wa "mtu anaye fall kwenye elevator"
Hii tunaiita "Free fall motion"
Sasa whether kuna "Force inayomvuta kuja chini" au "Hakuna Force yoyote inayo mvuta" ndio swali kwanza la kujibu
Kulijibu hili swali,turudi kwenye "first law of motion" au "Law of inertia"
Hii law inasema (roughly) kama hakuna any external force inayo act kwenye certain frame of reference (eneo lolote lile utakalo tumia Ku "observe ulimwengu")
Basi sheria zote za Physics zitakua sawa kabisa kwa aina hio ya Frame of reference
Frame of reference ambayo hakuna " Force" yoyote inayo act kwake tunaiita "Inertial Frame of reference"
Na sifa kuu ya inertial frame of references ni kwamba sheria zote za physics zinakua "valid" kwa kila inertial frame of reference
Means kama tukiamua Ku perform "Physical Experiment" yoyote ile tukiwa katika inertial frame of references mbili tofauti tutapata the same result
Shika hii point kuwa "inertial frame of reference" ni frame of reference ambayo hakuna "force" yoyote inayo "act" kwake...
Sasa imagines watu wawili tofauti Let's say "Juma" na "Asha"
Asha yupo mbali kabisa na dunia na mbali kabisa na kitu chochote chenye Mass...
I mean yupo kwenye "Outer space"
Hapa "Asha" hayupo subjected na Force yoyote ile...
So tunasema yupo kwenye inertial Frame of reference (F=0)
Na "Juma" ndiyo yupo hapa kwenye elevator inayo dondoka
Wote hawa wata feel weightlessness
Sasa conclusion ya muhimu hapa nikua,huyu "Juma" akiamua Ku perform "Physical experiment" yoyote ile ndani ya hii elevator inayoonekana kuanguka atapata majibu Yale Yale atakayo pata "Asha" kama naye akiamua Ku perform the same experiment
Implication yake ni nini?
Kama hakuna tofauti ya matokeo atakayo pata Asha na Juma
Basi wote tunasema wapo kwenye inertial Frame of references
Kumbuka Asha hayupo subjected na force yoyote ile...
Kama wote wapo kwenye inertial Frame of references basi hata Juma na elevator yake hayupo subjected na force yoyote ile (F=0)
Kama hayupo subjected na Force basi hii "downward acceleration' tunayomuona nayo inahitaji " maelezo mengine tofauti "
Cause hayupo subjected na Force yoyote ile so hakuna reason ya yeye Ku accelerate downwards
Cause a=0 kwa inertial frame of reference
Kwa logic hii "Elevator" hai accelerate chini kama "common sense inavyotwambia"
Ipo "stationary" hai move....
Na hio ndio "Equivalent principle"
Ukielewa hii umeelewa msingi wa General Relativity
General Relativity ni ngumu kuielewa cause inabidi utoke nje ya common sense ulizozizoea
Na nahisi wengi hawapo familiar nayo ndo maana napata ugumu huu kujibiwa swali langu
So turudi kwenye point kama "Juma" na "Elevator" hawa accelerate downwards tunaelezea vipi hiki kitendo cha "elevator" kuanguka chini wakati logic inatwambia elevator hai accelerate kuja chini
General Relativity imetupa majibu na majibu hayo nimeshindwa kuyaelewa thus why nimeuliza hili swali kwa walisoma General Relativity
Hint kidogo niliyopata ni kwamba "Mda ndio unaelezea kwanini kitu kudondoka"
Yaani "forward movement into future" inayotupa hii illusion of "falling"
Hapa ndipo sijaelewa
Matokeo yake nimeuliza in wrong platform ambao wengi hawapo familiar na hio General Relativity