Habari wadau, namshukuru Mungu na mimi leo nimepata placement kupitia database. Nilifanya written mbili mwezi Februari mwaka huu nikakandwa zote sikutoboa kuingia oral. Mwezi juni nikatinga tena Dodoma nikafanikiwa kupiga oral, zikatoka placement taasisi niliyopiga oral sikuwepo.
Leo nimefanikiwa kutokea kwenye mkeka. Niwatie moyo ndg zangu tuendelee kumuomba Mungu hakuna kukata tamaa naamini kila mtu atalamba asali humu. Huu uzi umebarikiwa sana, nilikua nikiona shuhuda humu zilikua zikinitia moyo na mimi siku moja nitatokea kwenye mkeka, hatimaye siku leo imetimia.
Status ni selected for oral both web na app.