Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Usipotangaza ndio unakuwa forgiven?
Ukitangaza unatoa promo za dhambi kwa wengine na kueneza uovu kuliko yule anayekaa kimya , mfano mimi nikianza kufichua maovu yangu kuna watu labda walikuwa wananihesabia kama kiigizo chao sasa wakijua na ikiwatokea situation kama yangu kupelekea kufanya dhambi watasema kama fulani yule kila siku swala tano na anafanya vitu fulani mimi ni nani nisifanye ?

Vilevile kutangaza ni dalili ya kibri kwamba aliweka makatazo si lolote hilo jambo ni kawaida.

Ndio mtu anakuwa Forgiven kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu kuna madhambi mtu atasamehewa kwa kuwa hakutangaza akayasitiri.
 
Soma iyo
20230514_144044.jpg
 
Hahahahaha watu mmeanza kutiririka sasa... kwa nini shule zao zinajengwa kwa sadaka na michango ya waumini (wakati mwingine hata kwa kuwalazimisha kuchangia), ila ada ni sawa kwa Wakristo na wasio Wakristo? Sasa kuna faida gani ya kuchangia? Watoto wa waumini wanafaidiakaje japo kwa uchache tu? Ni wenye pesa pekee ndiyo husoma shule hizo. Mfano ni Loyola nk!.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
Hivi na loyola ni yamichango.
 
Heri ya Jumapili kwa nyote.

Niende madani sasa.

Kwa nini uliacha kwenda kanisani mpaka leo hii? Ni nani au nini kilikufanya usiende tena kanisani? Mbona ulikuwa muumini mzuri tu na ulikuwa kiongozi wa vijana? Mbona ulikuwa kiongozi wa kwaya nk?

Unaweza ku share hapa sababu hasa iliyokupelekea ukaacha kwenda kanisani? Je, uliona ni usanii tu?

Karibu!

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
Sadaka
 
Hivi na loyola ni yamichango.
Ni ya msaada, ila ni ya Kikristo, lazima vipaumbele viwe kwa watoto wa kikristo, hata kwa kutoa ufadhili wa kusoma kwa ada nafuu nk! Hakuna shule nimewahi ona inafanya hivi zaidi ya janja janja tu. Ada ya Loyola unadhani mtoto wa mtoa sadaka mlalahoi atagusa?

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Shida ya makanisa ya SASA ni gospel for sale ,michango ni minigi mpaka Mungu mwenyewe atakuwa anatushangaa,ibada hazina mvuto SoMo la utoaji limeshika Kasi, ubatizo masharti kibao wachungaji mapadre tunawachangia Kila siku lakini hawatosheki hubuni majina mapya Kila wakati
Na kwenye makongamano ndio balaa zaidi. Mchungaji wa kutoa neno anaanza saa kumi na Moja, ujumbe mkuu ni matoleo mpaka mwisho. Akafu unaambiwa Kwa upole muda wa kutoa, jitahidi utoe zaidi ili ubarikiwe zaidi. Yaani ni hatari kabisaaaaa siku hizi. Na makanisa yanajazana kila Kona.
 
Nimeshuhudia visa vya watu kadhaa wakibabaika mbele za watu baada ya kukosea kutoa ushuhuda.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
ushuhuda unaweza kuwa kipimo cha imani ya kweli ila sio wakati wote.Kuna situation ambazo sio za kweli.Ni sawa na kuangalia miujiza.Kuna miujiza ya Mungu na ambayo ni ya nguvu za giza.Pia sio kipimo cha imani ya kweli.
Imani ya kweli inapimwa kwa ujumbe.
 
Kwa sababu niligundua Mungu hayupo na habari za kuwapo Mungu ni hadithi za kutungwa na watu tu.

Niligundua hivyo baada ya kufikiri sana kuhusu "the problem of evil", yani jinsi gani Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaoweza kuwa na mabaya, dhambi na shida ni contradiction, na mpaka leo hakuna aliyeweza kutatua contradiction hii.
Imani yako hiyo katika kuamini Mungu hayupo ni kwa sababu una a very narrow and limited scope ya nafsi na mwili wako kuyaona mambo.
Na pengine ukiupata uwezo huo utakuwa Lucifer mwenyewe.
 
Ukitangaza unatoa promo za dhambi kwa wengine na kueneza uovu kuliko yule anayekaa kimya , mfano mimi nikianza kufichua maovu yangu kuna watu labda walikuwa wananihesabia kama kiigizo chao sasa wakijua na ikiwatokea situation kama yangu kupelekea kufanya dhambi watasema kama fulani yule kila siku swala tano na anafanya vitu fulani mimi ni nani nisifanye ?

Vilevile kutangaza ni dalili ya kibri kwamba aliweka makatazo si lolote hilo jambo ni kawaida.

Ndio mtu anakuwa Forgiven kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu kuna madhambi mtu atasamehewa kwa kuwa hakutangaza akayasitiri.
Lakini kumbuka ni swali tu limeulizwa, halina maana ya kuwa anaelijibu anajigamba, hapana. Anaweza akasaidika pia kwa kupata mawazo chanya juu ya changamoto kuu iliyoweka pingamizi kwake kutembelea nyumba za ibada mkuu
 
Back
Top Bottom