Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Huwezi kumkuta Muislamu hata akiwa haendi msikitini ,haswali na mfanya maasi akijianika na kujisifia kuwa haendi msikitini ,labda huyo awe ameachana na imani ya mara nyingi huwa ujasiri huo kwani nafsi yake itakuwa inamsuta.

Misingi ya Uislamu ni haitakiwi mtu kutangaza uovu wake ikiwa Mwenyezi Mungu amemsitiri kwani ni uovu mkubwa mtu kufanya kibri katika maasi na kujisifia kuliko hata uovu wa kosa lenyewe.Na kuna uwezekano mkubwa asitubie kwa kuona ni kitu kizuri ila yule mwenye hofu na akaficha aibu zake kuna uwezekano mkubwa wa kupata rehma akatubu au kusamehewa.

Ila nashangaa upande wenu kila mtu anafunguka bila wasiwasi kama amefanya jambo ambalo zuri , huu sio uzi wa kwanza upo uzi mwingine watu wakijisifia masiku ambayo wasiyoenda Kanisani wakijiona watabe . Unakuta na mtu humu anahubiri neno la biblia lakini u amkuta kesho anapost uzi jinsi anavyogegeda watoto wa watu tena wakati mwingine akijisifu bila aibu.
Usipotangaza ndio unakuwa forgiven?
 
Kwa sababu niligundua Mungu hayupo na habari za kuwapo Mungu ni hadithi za kutungwa na watu tu.

Niligundua hivyo baada ya kufikiri sana kuhusu "the problem of evil", yani jinsi gani Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaoweza kuwa na mabaya, dhambi na shida ni contradiction, na mpaka leo hakuna aliyeweza kutatua contradiction hii.
Ulichokiongea ni kikubwa kuliko vichwa vya waaminio wengi mkuu.
 
Heri ya Jumapili kwa nyote.

Niende madani sasa.

Kwa nini uliacha kwenda kanisani mpaka leo hii? Ni nani au nini kilikufanya usiende tena kanisani? Mbona ulikuwa muumini mzuri tu na ulikuwa kiongozi wa vijana? Mbona ulikuwa kiongozi wa kwaya nk?

Unaweza ku share hapa sababu hasa iliyokupelekea ukaacha kwenda kanisani? Je, uliona ni usanii tu?

Karibu!

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
Nina maswali yaliyokosa majibu ndio maana na hakuna aliyeweza kunijibu kwa ufasaha maswali yangu. Nadhani miaka ya hivi karibuni nitahamia kule...
 
mimiamadiwenani niliacha kuamini mungu yupo baada ya kuona video fulani kisha kufanya utafiti wangu.... kiukweli niseme tu, naona maisha yangu yamekua bora zaidi sasa ambavyo siamini kwenye mambo ya mbinguni na kuzimu
Mfano ukafungua biashara kubwa hapo ulipo, je, utatumia nguvi ipi isiyoonekana kuilinda?

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom