Huwezi kumkuta Muislamu hata akiwa haendi msikitini ,haswali na mfanya maasi akijianika na kujisifia kuwa haendi msikitini ,labda huyo awe ameachana na imani ya mara nyingi huwa ujasiri huo hana kwani nafsi yake itakuwa inamsuta.
Misingi ya Uislamu ni haitakiwi mtu kutangaza uovu wake ikiwa Mwenyezi Mungu amemsitiri kwani ni uovu mkubwa mtu kufanya kibri katika maasi na kujisifia kuliko hata uovu wa kosa lenyewe.Na kuna uwezekano mkubwa asitubie kwa kuona ni kitu kizuri ila yule mwenye hofu na akaficha aibu zake kuna uwezekano mkubwa wa kupata rehma akatubu au kusamehewa.
Ila nashangaa upande wenu kila mtu anafunguka bila wasiwasi kama amefanya jambo ambalo zuri , huu sio uzi wa kwanza upo uzi mwingine watu wakijisifia masiku ambayo wasiyoenda Kanisani wakijiona watabe . Unakuta na mtu humu anahubiri neno la biblia lakini u amkuta kesho anapost uzi jinsi anavyogegeda watoto wa watu tena wakati mwingine akijisifu bila aibu.