Kwanini tunakufa?

Kwanini tunakufa?

ukisema tunakufa kwa sababu cell za mwili zinakuwa zishakufa , sasa vipi kuhusu watoto wadogo?? Cell zao zinakuwa zipo kwenye condition nzuri tu na wanakufa vile vile
Seli hufa kutokana na sababu nyingi, hivo kama kitu kinaitwa natural death ndo seli huchoka zenywe na kufa lakini pia zikisumbuliwa na kushindwa kupingana na usumbufu mwingine wowote hufa

*kufa ndio kitu ambacho mpaka kesho hakina majibu yenye uhakika
 
Tunakufa kwa sababu seli hai zetu zinafika mda zinachoka na hufa.

Kwa nini sayansi haiwezi kufufua watu? Mpaka hapa tulipofikia bado sayansi haijaweza kumfufua binadamu na niseme wazi tu kuwa sina hakika kama sayansi itaweza kumfufua mtu au la katika wakati ujao.
katu, abadan haitoweza
 
Hahahahaa, haka kamada kazuri sana kataifunga midomo ya WASIOAMINI UWEPO WA M/MUNGU, nanina uhakika hawatochangia.
Mimi nataka watumie sayansi yao kufufua wafu ,mfano kama tatizo la moyo kusimama na kupelekea mtu kufa nataka nione hiyo sayansi kama watamuwekea moyo wa bandia ili maiti aamke , au si kuna zile mashine za kushtua moyo sasa kwa nini wanashindwa kuzitumia moyo ukisimama moja kwa moja , au si huwa wana wabadilisha watu figo ili waendelee kuishi sasa kwa nini mtu akifa wanashindwa kumbadilishia figo ili aamke
 
Habari wana jamvi, natumai wote mu wazima na mimi kwa upande wangu ni mzima na bukheri wa afya.

Kama heading inavyosema hapo, nataka kujua ki undani zaidi kwanini tunakufa? Na kwanini binadamu akifa anashindwa kufufuliwa, kama tatizo lilikuwa ni figo kufeli kwanini baada ya kufa marehemu akiwekewa figo nyingine hafufuki?

Maana katika maisha ya kawaida kitu kikiharibika kabisa kama vile gari kikiwekewa kitu kipya kinapona na kinarudia hali yake ya mwanzoni.

Kwa Nini Tunakuwa Wagonjwa na Kufa?
Yesu alipowasamehe watu dhambi zao, waliponywa. Kwa mfano, Yesu alimwambia hivi mtu aliyepooza: “‘Ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kusema, Dhambi zako zimesamehewa, au kusema, Simama, utembee? Hata hivyo, ili mjue kwamba Mwana wa binadamu ana mamlaka duniani ya kusamehe dhambi—’ ndipo akamwambia yule mwenye kupooza: ‘Simama, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako.’” (Mathayo 9:2-6) Kwa hiyo, dhambi ndiyo inayosababisha magonjwa na kifo. Tulirithi dhambi kutoka kwa mtu wa kwanza, Adamu.—Luka 3:38; Waroma 5:12.
 
Tunakufa kwa sababu vital organs za mwili zinaharibiwa ghafla na pia au Cell zinachoka?...mfano neuron cells hazijizalishi, kama zitaharibiwa zitasababisha paralysis ambayo matokeo yake ni kifo.
 
Naye Yesu akajibu, Aliye ndani yangu hatokufa, na akifa atakuwa anaishi... Tukiderive kutoka kwenye kauli ya Yesu, binadamu hafi... Kinachokufa ni mwili huu wa binadamu in the process of transformation au kuhamishwa kwenye ulimwengu mwingine ambao mwili huu wa Duniani hauhitajiki... Ila Yesu akasema kuwa unapokufa kimwili utaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine simply tu kwa kuwa umeamini jina lake... Yesu alikanusha pale alipoambiwa kuwa Lazaro amekufa yeye akasema Lazaro amelala lakini nitakwenda nipate kumuamsha...
 
tunakufa kwa sababu ya magonjwa,afya,kutojali,ajali,kukosa tiba,kukosa kinga hii inatokana na sumu nyingi au wanadamu kuongeza vifo kwa teknolojia kama si hivi basi mungu kakuandikia
 
Kifo ni natural selection ,dunia ina uwezo Wa kubeba kiasi Fulani cha population kikizidi basi kunkuwa na natural selection alie weak ndio atakuwa selected
 
Ili Tukachomwe moto,tukiishi milele shimo la moto litakosa wapangaji.
Sasa kama Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake, tena kwa mapenzi ambayo mungu anampenda mwanadamu.
Kwanini sasa Mungu huyu haoni huruma kuandaa moto kwaajili ya kumchoma mwanadamu ambae anasema anampenda?
Kwahiyo pamoja na Mungu kumuumba mwana kwa mfano wake kama ishara ya upendo, kumbe hampendi?
 
Kifo ni natural selection ,dunia ina uwezo Wa kubeba kiasi Fulani cha population kikizidi basi kunkuwa na natural selection alie weak ndio atakuwa selected
Survival for the fittest haisemi hivyo, bali inatumika pale ambapo kuna upatikanaji mdogo wa labda chakula, maji au hata malazi ambapo wale ambao wako fit ndio wana survive na sio wale legevu kama unavyosema wewe
 
Kufa na kutoamini au kuamini mungu kuna uhusiano gani?
Uhusiano upo lakin mpaka uielewe vizuri hiyo post yote kwaujumla..!
Mfano mtoa post alihoji kwenye post yake kwanini "gari likifa linaweza kufufuliwa kwakubadilishiwa kifaa kilichokufa lakin binadamu akifa kwasababu yafigo hawez kuhuishwa kwa kwakuwekewa figo zengine"

Nyuma yakifo kuna nini na nini siri ya uhai??

##hayo nimaswali magumu kwawasioamini uwepo wa m/mungu##
 
Uhusiano upo lakin mpaka uielewe vizuri hiyo post yote kwaujumla..!
Mfano mtoa post alihoji kwenye post yake kwanini "gari likifa linaweza kufufuliwa kwakubadilishiwa kifaa kilichokufa lakin binadamu akifa kwasababu yafigo hawez kuhuishwa kwa kwakuwekewa figo zengine"

Nyuma yakifo kuna nini na nini siri ya uhai??

##hayo nimaswali magumu kwawasioamini uwepo wa m/mungu##
Asante sana kwa kunisaidia kumuelewesha huyo
 
Uhusiano upo lakin mpaka uielewe vizuri hiyo post yote kwaujumla..!
Mfano mtoa post alihoji kwenye post yake kwanini "gari likifa linaweza kufufuliwa kwakubadilishiwa kifaa kilichokufa lakin binadamu akifa kwasababu yafigo hawez kuhuishwa kwa kwakuwekewa figo zengine"

Nyuma yakifo kuna nini na nini siri ya uhai??

##hayo nimaswali magumu kwawasioamini uwepo wa m/mungu##
Mtoa posti yeye kauliza kwa nini watu tunakufa halafu wewe unaanza kuingiza habari za mungu. Hivi hamuwezi kujadili bila kumhusisha mungu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom