Kwanini Tanzania hatuna furaha? Nini kifanyike?

Kwanini Tanzania hatuna furaha? Nini kifanyike?

20240904_122706.jpg
 
Kwa Tanzania mechi Kati ya Simba na Yanga afu timu moja ipate ushindi bila Shaka kuna watanzania lazima watakuwa na furaha
haha dah ila Tanzania nchi yangu haiishi vioja!
 
Furaha ni kuwa na uwezo wa ku-solve kila changamoto inayoweza kuja mbele yako.

Kama huo uwezo haupo, sahau kuhusu furaha.

Kama upo umepanga tu sehemu umeme ukiisha kuweka hadi mtoke nje kukaa kikao. Mara muanze kuzozana, wakati unakuta ni 10k tu. Furaha haiwezi kuwepo.

Wife ameona kagauni kazuri kanauzwa 35k tu, hiyo hela ina-overtake mfuko. Furaha haiwezi kuwepo.

Parachichi la 500 tu likiwa dogo, furaha haiwezi kuwepo.

Hospital unamgonjwa anahitaji upasuaji unaogharimu 1M, furaha haiwezi kuwepo.
 
Uko sahihi Red black tatizo kauli ilitolewa na mwanasiasa baada ya walimu kucharuka. Pia ukienda SIDO kuna masomo mengi tu ya ujasiriamali kwa vitendo. Tatizo wanaleta siasa kwenye mambo ya msingi. Wako wasomi wengi tu wamejiongeza, wako wanaoendesha bajaji na boda boda pia. Tatizo ni siasa inapotumika kutatua tatizo la kiufundi.
👊
 
Furaha ni kuwa na uwezo wa ku-solve kila changamoto inayoweza kuja mbele yako.

Kama huo uwezo haupo, sahau kuhusu furaha.

Kama upo umepanga tu sehemu umeme ukiisha kuweka hadi mtoke nje kukaa kikao. Mara muanze kuzozana, wakati unakuta ni 10k tu. Furaha haiwezi kuwepo.

Wife ameona kagauni kazuri kanauzwa 35k tu, hiyo hela ina-overtake mfuko. Furaha haiwezi kuwepo.

Parachichi la 500 tu likiwa dogo, furaha haiwezi kuwepo.

Hospital unamgonjwa anahitaji upasuaji unaogharimu 1M, furaha haiwezi kuwepo.
Umeongea ukweli kabisa mzizi wa fitina uko hapo tu.
 
Hio ni quick hypothetical analysis mkuu ila kiuhalisia ukitembelea Tanzania nzima huenda ukapata asilimia zitakazokuacha mdomo wazi!
Hiyo ni kweli hususan ukizingatia yanayojitokeza:
1. Hoja ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Wahusika (Viongozi na Serikali) ni kama haliwahusu na badala yake wanatoa maelekezo tatanishi e.g. Wasomi waende VETA.
2. Kwa ukame unaoendelea sijawasikia Wataalam, Viongozi wa Serikali hata Wanasiasa wakionesha kushtushwa na hali hii kana kwmba wanalo suluhisho in hand wanasubiri muda muafaka waanze kuDish out solutions.
3. Utekaji na mauaji ya raia vimekuwa kama ni vitu personal. Vyombo husika vya Dola havijajikita kutafuta suluhisho au kuwabaini wahusika bali siku zote wanasema ni "Wasiojulikana"
4. Masuala ya Upigaji, Matumizi mabaya ya Fedha za walipa kodi, Upatikanaji wa huduma za kiAfya havishughulikiwi ipasavyo, kupatiwa Suluhisho na The way forward bali vimeachwa au kupuuziwa vitajisolve vyenyewe kwa wakati wake.
 
Natumaini ni kwema wakuu.

Kwa mujibu wa ripoti mpya ya orodha ya nchi zenye furaha duniani, Tanzania(136) tumepitwa mpaka na Somalia(122).

Imesikitisha sana hii habari ni kana kwamba naishi nchi ya majonzi,huzuni, na masononeko!
Tuondoe/tubadili chochote kinachotukosesha furaha!
 
Hiyo ni kweli hususan ukizingatia yanayojitokeza:
3. Utekaji na mauaji ya raia vimekuwa kama ni vitu personal. Vyombo husika vya Dola havijajikita kutafuta suluhisho au kuwabaini wahusika bali siku zote wanasema ni "Wasiojulikana"
Inasikitisha sana na kuongeza huzuni kwa watanzania, hasa hio na.3 nimesikia kuna mwananchi aitwae Pendo walitaka kumtumia kama mercenary akammalize Mpina! ili sijui iweje sasa!
 
Mwaka juzi nilikwenda pale hospitali ya Amana, Ilala, nikakuta wanatoa jengo jipya kwa mbele. Kilichonishangaza wale mafundi pale wanafunga nondo wengine wanatwanga zege lakini miguuni wamevaa kandambili, sasa wale furaha wataitoa wapi?
 
Back
Top Bottom