Kwanini sisi watu weusi hatuvumbui vitu?

Kwanini sisi watu weusi hatuvumbui vitu?

Mfano wa topic gani ambayo kwenye mtaala wetu haipo,

Sijasema ugunduzi umekoma ila ninachosema hauna uhusiano wa moja kwa moja na elimu ya darasani kule tunafundishwa ujuzi au ufahamu wa vitu vilivyokwisha kugunduliwa ila sasa ukishaelewa unaweza endeleza (innovation) hata vitu vingi tunavyovisoma ni ugunduzi wa watu waliofanya research wakajua mambo mbalimbali kuhusu dunia na vilivyomo je hao wenyewe walikuwa na elimu gani kabla ya kuandika?
Ulichokiuliza hapo mwishoni kinaonesha wazi kwamba akilini mwako unaamini ugunduzi umekoma na kwamba kuna kizazi kilishagundua kila kitu tayari. Na kwa mtazamo huu huwezi kunielewa!
 
Sir Isaac Newton alisoma University of Cambridge's Trinity College

Albert Einstein alisoma ETH Zurich (then the Swiss Federal Polytechnic School), the Aarau high school in Switzerland, and the Luitpold Gymnasium in Germany.

Pia gunduzi nyingi zimefanywa na wasomi kuliko ambazo hazijafanywa na wasomi
Ni sawa lakini hoja yangu ni kuwa ni wote wanaosoma cambridge university wamegundua vitu? Je hatuna wasomi waliosoma hivyo vyuo na bado hata kiwembe cha kukatia kucha na stick za kuchokonolea meno hawawezi gundua? Hapo utaona kilichomfanya isaac Newton kugundua vitu sio shule pekeake ila kuna u-genius upo kichwani mwake ambao umemfanya kufika hapo

Pia rasilimali pesa na miundo mbinu ni nyenzo kubwa katika uvumbuzi na hili sio suala la serikali pekeake bali hata na sekta binafsi kuliko kuwekeza kwenye vipaji vya michezo na mziki ziwekeze katika uvumbuzi. Mtu kama bakhresa anaweza anzisha academy yake ya teknolojia kuwadhamini vijana kuonyesha ujuzi wao katika kubuni vitu mbalimbali nchini na mwisho wa siku wakapata exposure kimataifa kama walivyo wachezaji na wasanii
 
Ulichokiuliza hapo mwishoni kinaonesha wazi kwamba akilini mwako unaamini ugunduzi umekoma na kwamba kuna kizazi kilishagundua kila kitu tayari. Na kwa mtazamo huu huwezi kunielewa!
Nakuelewa mkuu ila fact ni kwamba shida sio mfumo wa elimu tulionao kwani duniani mitaala inarandana tofauti ni miundo mbinu na uwekezaji kwenye hicho kinachofundishwa

Mfano ili uive vizuri kwenye somo la chemistry na physics ili siku nawewe uje na innovation yako kunahitajika maabara za kisasa na field za maana kuelewa baadhi ya topics ambazo ndio msingi wa vumbuzi mbalimbali shida inakuja maabara zenyewe utakuta test tube na reagent mbili za kujibia pepa tu

Kingine ndio hicho ubunifu kwenye vichwa vyetu ni zero kabisa yaani kunahitaji elimu gani kubuni stick za kuchokonolea meno ambazo tunaagiza china?
 
Huo ugunduzi utafanyika saa ngapi ikiwa watu wapo busy kufuatilia ujinga ujinga?
Mabadiliko yeyote huanza kwa kubadilisha mindset,
Attitude,beliefs and way of thinking that shape how you see yourself and the World,

Sasa hivi wapo busy kujadili issue ya Doto Magari,ikiisha hii issue,wataletewa Kiki nyingine, na maisha yanaenda na siku zinasonga mbele.
Ni nani wa kulaumiwa kwenye hili?
 
Sbabu ni uwezo mdogo wa kiakili. Chanzo cha uwezo mdogo wa kiakili ndio bado hakijajulikana ila huenda imechangiwa na mambo mengi ikiwemo lishe mbovu, kutawaliwa muda mrefu, matumizi ya bidhaa zenye ubora duni zinazoharibu uwezo wa kiakili n.k.

Watu wachache wenye akili nzuri wakizungukwa na watu wengi wenye akili mbaya matokeo jumuishi ni kuwa wote wataenda sawa, akili mbaya. Kama tungeweza, tungeweka utaratibu kama wa "Genius Visa", kwamba tunaweza toa visa ya mtu kuingia na kukaa nchini kwa exemptions fulani fulani as long as huyo mtu ana akili ya kitofauti ambayo tunaweza kuitumia kutatu matatizo yetu hapa nchini.

Kuna matatizo ya kawaida kabisa ambayo shida yake sio bajeti ila ni akili bunifu ambayo huenda tukiwa honest tukubali kuwa hatuna. Matatizo ya upatikanaji wa maji safi kwenye mikoa yenye vyanzo vikubwa kama Mwanza, Geita na Kagera, matatizo ya foleni, matatizo ya upatikanaji wa huduma za umeme. Imagine mkoa muhimu kama Dar kuna maeneo maji yanatoka kwa wiki mara moja, huu mwaka 2026.

Si umeona tu hata ujenzi wa mabarabara inabidi tulete wachina maana watanzania wenzetu wakijenga baada ya miezi sita mashimo yanajaa.

Umeona pia nchi kama South Africa ambayo wazungu walibaki na wameshika maeneo mengi muhimu ya kiuchumi na kiutawala, leo South Africa imejengwa kama Ulaya. Nchi kama Zimbabwe au Uganda ambayo walifukuza wazungu, nadhani wote tunajua zilivyo kwa maana ya hali ya maisha na upatikanaji wa huduma za kijamii.

Naomba kuwasilisha.​
Nini kifanyike ili tutoke hapo?
 
Watu weusi wapi, mbona kuna watu weusi huko kwa wenzetu wamefanya makubwa. Na kuna mnaowaita weupe huku kwetu hawajafanya lolote pia. We sema tu Afrika.

Afrika inasota kutokana na ujinga wa mababu zetu walioingizwa kingi na wakoloni, wahuni waliobeba mataifa ya Afrika baada ya uhuru bandia, na ukoloni mambo leo. Mambo ni yaleyale, ipo wazi mbona.
Kwa sasa, ni nini kinacho tukwamisha?
 
Uvumbuzi ni mchakato wa kuunda, kugundua, au kutengeneza kitu kipya au mbinu mpya ambayo haikuwepo hapo awali. Ni dhana inayolenga kutoa suluhisho la kipekee na lenye manufaa kwa jamii kwa mara ya kwanza.

Ili kuelewa zaidi maana na tofauti za dhana hii, mambo yafuatayo ni muhimu:1. Tofauti kati ya Uvumbuzi (Invention) na Ubunifu (Innovation)Ingawa mara nyingi hutumika kwa pamoja, maneno haya yana maana mbili tofauti:

Uvumbuzi (Invention): Ni kitendo cha kufanikiwa kuunda au kugundua kitu ambacho hakikuwahi kuwepo kabisa duniani, kama vile balbu ya mwanga au chanjo.
Ubunifu (Innovation): Huu ni utekelezaji wa kuboresha kitu au huduma ambayo tayari ipo ili iwe na tija zaidi, rahisi kutumia, au yenye thamani zaidi.


2. Aina za UvumbuziTeknolojia: Ugunduzi wa vifaa vipya, mashine, au mifumo ya kidijitali.Mbinu na Michakato: Uvumbuzi wa njia mpya za kufanya mambo (kama vile njia mpya za kilimo au matibabu).Sayansi: Ugunduzi wa kanuni mpya za kisayansi, dawa, au vitu vya asili.
 
Uvumbuzi ni mchakato wa kuunda, kugundua, au kutengeneza kitu kipya au mbinu mpya ambayo haikuwepo hapo awali. Ni dhana inayolenga kutoa suluhisho la kipekee na lenye manufaa kwa jamii kwa mara ya kwanza.

Ili kuelewa zaidi maana na tofauti za dhana hii, mambo yafuatayo ni muhimu:1. Tofauti kati ya Uvumbuzi (Invention) na Ubunifu (Innovation)Ingawa mara nyingi hutumika kwa pamoja, maneno haya yana maana mbili tofauti:

Uvumbuzi (Invention): Ni kitendo cha kufanikiwa kuunda au kugundua kitu ambacho hakikuwahi kuwepo kabisa duniani, kama vile balbu ya mwanga au chanjo.
Ubunifu (Innovation): Huu ni utekelezaji wa kuboresha kitu au huduma ambayo tayari ipo ili iwe na tija zaidi, rahisi kutumia, au yenye thamani zaidi.


2. Aina za UvumbuziTeknolojia: Ugunduzi wa vifaa vipya, mashine, au mifumo ya kidijitali.Mbinu na Michakato: Uvumbuzi wa njia mpya za kufanya mambo (kama vile njia mpya za kilimo au matibabu).Sayansi: Ugunduzi wa kanuni mpya za kisayansi, dawa, au vitu vya asili.
Hayo ni maelezo tu; kwa nini hatuvumbui?
 
Hayo ni maelezo tu; kwa nini hatuvumbui?
Unao uhakika kwamba hatuvumbui?

Na hizi ni hoja siyo suluhu ya uvumbuzi kama upo /tunavumbua ama hatuvumbui,

Kujua nini cha kutenda ni rahisi,kwenye kutenda kuna ugumu wake, kama ingekuwa Rahisi basi Madanguro yangekuwa Makanisa/mahekalu na Nyumba za maskini makasri ya kifalme,

Hivi siyo hoja au msemo wa utetezi , Gunduzi zipo fanya utafiti wako kwa kina/vizuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom