Mkuu usikariri multitasking sio 2 apps unaweza fanya multitasking hata apps 100 na zaidi, usichanganye side by side multitasking na multitasking yenyewe. Iphone unapotoka kwenye app baada ya muda ina reload na hai resume instant hivyo kama ni app inayotegemea session inakula kwako.
Unaweza weka video inayoonyesha setting moja imetumika? Mfano zote zinarun at 720p na sio moja inarun 2k na nyengine 720p then ulete claim zisizo sahihi. Fortinite inalag vibaya mno kwenye iphone na android pia nakuwekea baadhi ya ushahidi
Na pia epic wenyewe watengenezaji wamekiri na wameahidi fix
Again nakupa source ya fans wa Apple
Epic Games promises fix for Fortnite’s performance & graphics issues on iOS
All in all point yangu haikuwa kupambanisha nguvu ya hizi device bali kukuonesha processing power ya simu haitoshi na bado inahitajika zaidi.
Mkuu jinsi zitakavyoongezeka power ndio jinsi matumizi yatakavyokuja. Sasa hivi samsung na Huawei wanakuja na docks na kuwezesha simu zao kutumika kama desktop, simu ina 512GB internal na ram 8gb, nikiwa nyumbani inakaa kwenye dock yake na kuconect na monitor naenjoy. Kuna matumizi mengi tu utaenjoy power ya simu.
Mkuu huko kwenu tarehe ngapi leo? Maana sikuelewi ujue uzi mzima unataja tu s4 inaingia vipi hapa simu ya 2013 zaidi ya miaka 5 iliopota?
Samsung anacopy ndio ila Apple anacopy zaidi, 1bn aliopigwa fine samsung haifikii 2B alizolipa Apple kwa Nokia mwaka jana, bado pia Apple amekutwa mara kibao anaiba tech za watu mfano.
2011- touch screen and related technologies toka nokia
2017- processor za Apple zilikuwa zinaiba technology ya Wisconsin University
2018-Virnetx patents za communication
Hizo ni lawsuit kubwa ambazo Apple amelipa trilioni 1 ama zaidi za kitanzania bado nyengine ndogo ndogo anazolipa mara kwa mara, kinachomsaidia Apple ana hela tu na uwezo wa kulipa hizo damage ila haipiti mwaka bila Apple kukamatwa na hatia ya ku copy technologies za watu.
Mkuu issue hapa ni kufuata trend. Hebu tuangalie iphone na samsung miaka 3 ama 5 iliopita.
-iphone zina kioo kidogo na samsung kioo kikubwa na fans wa iphone wanawacheka wa samsung misimu yao mikubwa
-iphone zinatumia LCD na kina samsung OLED/Amoled na wanachekwa kina samsunh vioo vyao vina burn in
-iphone zina bezel na samsung akaanza bezel less kuanzia 2015 kama sijakosea enzi za s6 edge
-Simu za samsung zilikuwa na resolution kubwa sana wakati iphone wao walikuwa hawajali resolution hata HD iphone zilikuwa hazifiki.
-wao iphone chaja za kawaida tu ila kina samsung na wireless charging waliambiwa ni useless feature
-iphone zilitumia chaja za kawaida na Samsung fast charging
-iphone haikuwa water resistant na samsung zilikuwa toka enzi za s5
-iphone zilikuwa na mono speaker na samsung stereo
-iphone ilikuwa mpaka ubonyeze power key ndio uone kama ni saa ama notification za lockscreen wakati samsung alikuwa na always on screen
-ku unlock simu ulikuwa huwezi kwa ku double tap kwenye iphone.
Hayo mambo 10 niliyokutajia Apple hana sasa hivi? Kila mwaka innovation zake ni ku copy feature za wenzake.
APP usichague wewe, app achague mtumiaji, mfano una emulate windows kwenye android gb ngapi za ram utahitaji? Nyingi tu. Na hata hio photoshop unayoitaja wewe ni ile app ya bure, ipo full photoshop ya android adobe aliizindua sema watu walichakachua sana alivyoona hapati mapato akaitoa store na kuo discontinue, uzuri wa android unaweza uka sideload apk yake hata leo na kuitumia. Ina feature nyingi za version ya pc.
Ghz si nguvu ya processor wala wingi wa core intel cpu zake zikiwa na core chache na clock ndogo zinapita cpu za Amd zenye core nyingi na clock kubwa.
Its all about ipc (instruction per clock)
Cpu inaweza ikawa 1.1ghz na ikawa na nguvu kushinda yenye 3.5ghz, cpu inaweza ikawa na core 4 ikaishinda yenye core 8. Mfano mzuri ni snapdragon 820 ina core 4 tu ila ilikuwa best mwaka wake.
Na kama hufahamu kuanzia iphone 6s Apple ana best processor on market ina nguvu kushinda simu zote kama nilivyoelezea post yangu ya kwanza. Hivyo kama unaamini processor yenye nguvu ni useless anza na kampuni yako pendwa.
Kama nilivyokwambia hapo juu multitasking si kurun app mbili kwa mpigo tu, mfano nikupe wa multitasking.
Nafungua youtube naplay playlist ya miziki kisha naminimize app ya youtube, mziki wangu unaendelea kupiga, nafungua app yangu ya wechat mchina amenitumia msg, nafungua google translator, naiweka wechat na google translator side by side, napaste msg zake kwenye translator huku namjibu. Akiwa hajibu upesi naweza fungua game la draft kidogo nacheza huku nasubiria ajibu, naswitch baina ya wechat na game mara kwa mara no reload.
Huo ni mfano mdogo tu ila unaweza fanya multitasking ya apps kibao.