Kwanini siku hizi Bar hazina watu?

Kwanini siku hizi Bar hazina watu?

Mmmh! watu wengi ni wagonjwa wa maradhi mbalimbali kuanzia malaria, pressure, figo, uhanithi, kisukari, HIV na ugumba. Hivyo, baadhi ya masharti wanayopewa na madaktari wao kutibu maradhi yao ni kuacha kunywa pombe, hence low attendance. Acha mwenyewe leo kunywa pombe kabla hujaambiwa na dk. wako uache kunywa pombe. Watu wamegeukia kunywa Tanga fresh na mlonge, na kula matunda tu.

Daaaaaaaaahhhh!!!

Wewe unahamasisha watu waache kunywa POMBE!!!!!!

SErikali inapata mapato makubwa sana katika vinywaji vikali na sigara. Siku hizi hakuna Kodi ya Maendeleo (Kodi ya kichwa)

Hivyo moja ya njia serikali inapata mapato ni kwa watu kunywa POMBE (Simaanishi pombe za kienyeji ingawa nazo ni muhimu kwani zimeongea ajira nchini)

Hivyo licha ya mapato yaserikali pia unywaji wa pombe umeongeza ajira kwani watu tumeajiriwa katika makampuni ya vinywaji vikali (Breweries), kuajiriwa katika maduka na bar zinazouzwa pombe.

Hivyo pombe ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu ikizingatiwa Tanzania bajeti yetu kwa asilimia kubwa ni kuongeza kodi katika vinywaji na Sigara kila mwaka.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
uchumi umekuwa mgumu sana na kutokana na hilo watu wanapunguza matumizi yasiyo kuwa ya razima,asilimia kubwa ya wafanyakazi wanalipwa chini ya mil 1,na wafanya biashara wengi wana mikopo ya benki,na bei za bidhaa ziko juu,steam za bia zinatoka wapi
 
daaaaaaaaahhhh!!!

Wewe unahamasisha watu waache kunywa pombe!!!!!!

Serikali inapata mapato makubwa sana katika vinywaji vikali na sigara. Siku hizi hakuna kodi ya maendeleo (kodi ya kichwa)

hivyo moja ya njia serikali inapata mapato ni kwa watu kunywa pombe (simaanishi pombe za kienyeji ingawa nazo ni muhimu kwani zimeongea ajira nchini)

hivyo licha ya mapato yaserikali pia unywaji wa pombe umeongeza ajira kwani watu tumeajiriwa katika makampuni ya vinywaji vikali (breweries), kuajiriwa katika maduka na bar zinazouzwa pombe.

Hivyo pombe ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu ikizingatiwa tanzania bajeti yetu kwa asilimia kubwa ni kuongeza kodi katika vinywaji na sigara kila mwaka.


Mizambwa
inaniuma sana!!!
wa tz tukigoma kunywa pombe serikali itapata akili ya kutafuta vyanzo vingine vya mapato
 
siku hizi kila nyumba yenye kaduka kuna bia,sasa ya nini nijitese bar wakati bia ziko sebureni kwa mangi?na mkopo juu nalipa mwisho wa mwezi kiuaminifu kabisa
 
Tunaionyesha serikali yako njia yakuingiza mapato,kila mwaka bia,sigara wapandisha bei,iambie twanywa nailoni tu(vroba) tena twanunua madukan tu,
 
Ulevi ni ujanja wa ujanani.Ukishakua unagundua kumbe ni upuuzi so unatupilia mbali tabia hizo.
 
Watu wengi wameokoka wameona wakatoe sadaka na mafungu ya kumi kanisani na bado watazifunga bar zote
 
Na ukitaka kujua hivo angalia hata kwenye maharusi na sherehe mbalimbali kwenye bia za bure watu wanakunywa juyce ma Malta na soda sio via wengi wamegundua bia sio kwanza no dhambi afu zinaharibu afya.
 
wahudumu customer service zero, vyoo vyao vichafuu....ni asavali nijinywee tu home
 
Ukienda bar ukaagiza soda wahudumu wanakuangalia kwa madharau sana tena wanakuhudumia kwa kujivuta sana.
ila ukiagiza bia wanakuhudumia kama king mswati.
 
Bar zimekuwa nyingi kila mwenye kibaraza au kiuwanja kidogo basi usiku panageuzwa bar
 
Wana jamii mm ni mnywaji mzuri sana wa bar tofauti tofauti, lkn cha kushangaza siku za hivi karibuni nikienda bar watu wamepungua sana kwa kiasi kikubwa, anzia bar kubwa kama roozi gaden, kona bar brek point, igo bar watu , uhuru peak bar masai clabu jakalanda pub, mk bar, kote huko watu hamna,na bar nyingine nyingi dar, swali je ni uchumi umeyumba au ni bar zimekuwa nyingi? Swali la pili ni watu wameamua kuokoka na kumedia mungu? Wana jamii naombeni tusaidiane maoni
Mkuu tunajiandaa na Xmass....Tukirudi Moshi na Arusha lazima tuoneshe tulichochuma
 
Naomba mungu anijalie uzima nishudie tukio la kihstoria
 
Back
Top Bottom