Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Hahaha hiyo reli ya SG itabeba nini cha ziada ambacho reli ya mjerumani ilishindwa?! Mnaipa promo ikiisha mtaikana, maana haitaingiza chochote cha ziada tofauti na hii ya mjerumani.
Kwa awamu hii ni whitelephat projects maana hakuna mizigo labda Kwa awamu zijazo.Ili iwe Na tija Na ilipe zaidi yatakiwa uchumi uzunguke,vikwazo viondolewe vilivokimbiza wafanyabiashara wa nje kupitisha mizigo kwetu,Bila mizigo Na abiria,ni bure itakuwa sawa Na ndege,Huwezi ukasomesha watu no then ufanye biashara upate faida,sababu umepunguza purchasing power ya watu.
 
Kwa awamu hii ni whitelephat projects maana hakuna mizigo labda Kwa awamu zijazo.Ili iwe Na tija Na ilipe zaidi yatakiwa uchumi uzunguke,vikwazo viondolewe vilivokimbiza wafanyabiashara wa nje kupitisha mizigo kwetu,Bila mizigo Na abiria,ni bure itakuwa sawa Na ndege,Huwezi ukasomesha watu no then ufanye biashara upate faida,sababu umepunguza purchasing power ya watu.
Hawaonyeshi kufanya lolote kati ya uliyo yaorodhesha, Lakini wanavyoishabikia utadhani huko Bara inakokwenda kuna kitu kilikuwa hakiwezi kusafirishwa, na sasa hiyo Reli ya SG imekuja kukikomboa. Nafahamu hata miongoni mwao wameshaanza kuelewa, maana nilimsikia hata Spika Ndugai alisema, Bora nguvu iliyowekezwa kwenye hiyo Reli ya SG ingetumika kwenye bwawa la SG maana litakuwa na impact ya moja kwa moja, umeme utakuwa mwingi, itapunguza kukatika katika kama siyo kuondoa kabisa, na itawaleta wawekezaji ambao wameshindwa kuwekeza kwa sababu ya kutokuwa na umeme wa uhakika.
Ingawa still wapo wale cheer leaders kazi yao kushangilia hawafahamu hata detail za wanachokishangilia.
Sijui watasafirisha nini, na hiyo kasi wanayo ililia wanataka tuishi mwanza tufanye kazi Dar au kinyume chake au wanataka kasi ili isaidie nini? wao husema biashara, labda kama wana taka kuuza ice cream za Dar huko mwanza.
 
Kigezo cha kujenga reli kuelekea mkoa fulani ni lazima mkoa huo uwe unapakana na nchi nyingine nyingi?,uchumi wa kanda ya ziwa ni mkubwa kuliko kigoma hata mabasi yanayotoka ubungo kwenda kanda ya ziwa ni mengi kuliko yaendayo kigoma.Wewe ungekuwa mtoa maamuzi ungejengea watu wa mji wa Kigoma reli ya SG,halafu ukaacha watu wa jijini?.SGR itakapokuwa kama tunavyoelezwa kwa ubora na spidi yake ikifika hadi Mwanza,na nauli ikawa ya mtu mnyonge,wasafiri wa treni wa kwenda Mwanza ni wengi kuliko huko Kigoma.Rwanda yao inapitia Isaka Kahama,uchumi wa Burundi ni dhaifu sana kanda ya ziwa nafuu.Mashariki ya Kongo itaendelea kuhudumiwa kama ilivyokuwa.
Basi kama kigezo ni hicho basi sgr ingeelekea bukoba Kagera
Maana sizani kama kuna mkoa unapakana na nchi nyingi kama Kagera

Kaskazini Uganda,magharibi Rwanda yote imepakana na kagera kiasi huwezi enda Rwanda bila pitia Kagera
Pia kusini magharibi kuna Burundi na pia ukivuka ziwa unaelekea Kenya.
Lakini Kagera wametulia na sidhani kama kuna lolote serikali ilishawahi Fanya katika mkoa huu


Uzuri wa Kagera kuna wasomi wengi Sana ndo maana huwezi linganisha Kagera na kigoma
 
Hawaonyeshi kufanya lolote kati ya uliyo yaorodhesha, Lakini wanavyoishabikia utadhani huko Bara inakokwenda kuna kitu kilikuwa hakiwezi kusafirishwa, na sasa hiyo Reli ya SG imekuja kukikomboa. Nafahamu hata miongoni mwao wameshaanza kuelewa, maana nilimsikia hata Spika Ndugai alisema, Bora nguvu iliyowekezwa kwenye hiyo Reli ya SG ingetumika kwenye bwawa la SG maana litakuwa na impact ya moja kwa moja, umeme utakuwa mwingi, itapunguza kukatika katika kama siyo kuondoa kabisa, na itawaleta wawekezaji ambao wameshindwa kuwekeza kwa sababu ya kutokuwa na umeme wa uhakika.
Ingawa still wapo wale cheer leaders kazi yao kushangilia hawafahamu hata detail za wanachokishangilia.
Sijui watasafirisha nini, na hiyo kasi wanayo ililia wanataka tuishi mwanza tufanye kazi Dar au kinyume chake au wanataka kasi ili isaidie nini? wao husema biashara, labda kama wana taka kuuza ice cream za Dar huko mwanza.

Kama twapanda,bure sawa,Lkn Kwa runcost usitegemee mashetani watamudu kupanda SGR ,SGR Na ndege hii ni Kwa ajili ya high class people ndo watamudu,mashetani wao watabanana kwenye mabus Na malori
 
Kama twapanda,bure sawa,Lkn Kwa runcost usitegemee mashetani watamudu kupanda SGR ,SGR Na ndege hii ni Kwa ajili ya high class people ndo watamudu,mashetani wao watabanana kwenye mabus Na malori
Ndege waliishasema ni kwa ajili ya watalii,Wanasema walifufua shirika ili kufufu secta ya utalii, ila hiyo SGR sijui itakuwa ya nani maana gharama hata hao wakihoma na mwanza sidhani kama wataweza.
 
Hahaha hiyo reli ya SG itabeba nini cha ziada ambacho reli ya mjerumani ilishindwa?! Mnaipa promo ikiisha mtaikana, maana haitaingiza chochote cha ziada tofauti na hii ya mjerumani.
Wewe umekaribia sana jibu nililotaka kumpa mleta mada, lakini kwa maandishi laini sio kama haya yako.

Ngoja nijaribu: Ujenzi wa miundo mbinu kama reli, hufuatana na biashara iliyopo. Kiasi cha mizigo, abiria watakaotumia miundombinu hiyo. Na kabla ya kuangalia biashara inayotoka nje, kwanza ni biashara ya ndani ndio inatoa msukumo mkubwa. Lengo la biashara ya nchi za jirani, hilo hufuata, kama lengo la mda mrefu.

Eneo la Ziwa, hujumuisha Mwanza, Shinyanga, Kagera, Mara, Simiyu n.k.,, sio Mwanza peke yake; lina wakazi wengi na bila shaka biashara yake nayo itakuwa ni kubwa. Sidhani kuwa ni sahihi kuiangalia Mwanza pekee kuwa ndiyo inayopelekewa hiyo miundombinu.
Kigoma nayo ina sehemu yake, sidhani kuwa imetengwa.

Ukiniuliza kuhusu uwanja 'mkubwa' mpya wa ndege Chato, hapo sina jibu. Hivi Kigoma kuna uwanja kama huo?
 
Wabongo bhana, ukiwa mlevi tu hata unywe maji watasema unakunywa pombe....
Kwa sababu Jamaa anatokea Mwanza itakuwa kajipendelea?
Mleta uzi Gombea urais ili naww tuone Kama utajenga Kwa jirani yako ukaacha kwako.. Kila mtu yuko ktk kutafuta ridhiki na unafuu wa maisha yake... We subiri mletewe reli kigoma...
 
Kuna watu wana chuki sana na Mwanza, awamu zote hazijawah kuwekeza Mwanza, hata Barabara ni mbovu zilizopo kule, lakn hata kwenye reli hewa na penyewe mnainanga tuu.....Bandari Mbovu, hakuna chuo cha serikali, uwanja wa ndege Mbovu,...na bado jiji linashow muscles ya kutosha tuu, Siku serikali ikiamua kupendelea Mwanza kiukweli kweli, si mtahama nchi
 
Kigoma endeleeni na mradi wenu wa TELEZA reli itakuja. Tunaunganisha reli pande zote but tunaanza na kuliko na biashara na watu wengi. Sitasahau mlivyo kuwa wachafuzi wa mabehewa nyie kina Zitto!
 
Mkuu Pasco, Mwanza imeondokaje kutoka kuwa mkoa wa pembezoni? Hizo zote ni itiatiatives za serikali, serikali ndio nayohusika na kutengeneza mazingira ya hizo viabilities ili kukuza uchumi, leo wabunge na wananchi wanapiga kelele kuwa biashara nchini zinadorora serikali nayo imekubali na kuitaka TRA ichukue hatua za kukabiliana na mdororo huo.

Serikali isipoandaa mazingira ya kiuwezeshaji: miundombinu na sheria za kusimumua uchumi wa sehemu husika, Kigoma itaendelea kuwa pembezoni na Mwanza itaendelea kuwa strategic town. Usishangae hata Katavi na Geita mikoa ya juzijuzi tu inaenda kuwa mbele ya Kigoma.

Hivi unajua kuwa mfanyakazi wa serikali anayeishi Kigoma ni masikini kuliko anayeishi Mwanza? Wanaweza kulipwa kima kimoja cha mshahara, lakini kwa uwezo wa kukidhi mahitaji, yule wa Mwanza anahimili zaidi kuliko yule wa Kigoma maana wa Mwanza ananunua kilo ya sukari kwa sh. 2700/= wakati yule wa Kigoma, kwa mshahara uleule analipa sh.3000/- !

Sasa bila serikali kutengeneza mazingira wezeshi kwenye mikoa hiyo ya pembezoni na kuendelea kutoa kipaumbele kwa mikoa iliyo kwenye kitovu, hiyo mikoa ya pembezoni itabaki kuwa masikini na ile mingine itaendelea kufanikiwa zaidi.

Hapo ndipo lile andiko kuwa ' mwenye vingi ataendelea kuongezewa, na yule mwenye vichache hata hivyo vichache atang'anywa na kupewa yule mwenye vingi ".

Vv
Mkuu Vv, kwanza nakubaliana na wewe, serikali za awamu zote zilizopita, ziliutelekeza mkoa wa Kigoma, kwa kutousisimua uchumi wa Kigoma. Tanzania tunatumia fedha nyingi sana kuagiza mafuta ya kula, Kigoma zao la chikichi linastawi, zao hilo lingeendelezwa kama chai na kahawa, lingekuwa na manufaa makubwa kwa taifa kuliko zao jingine lolote na Kigoma would have been the richest region, lakini mkoloni alijikita kwenye cash crops za demand yake na sio demand yetu kama kahawa, as a result, mikoa wazalishaji wa kahawa ndio the richest regions wakati hiyo kahawa tunawazalishia wazungu, halafu foreign currency yote ya kahawa tunaitumia kuagiza mafuta ya kula ya mawese kutoka Malaysian wakati Kigoma ilianza kustawisha mawese kabla ya Malaysia.

Tulipopata uhuru hadi leo tumeendelea kutembea mule mule wakoloni walimotutembeza.

Tuna agitation mchele wakati bonde Ruvu pekee lingetosha kulisha Tanzania nzima, achilia bonde la Usangu na bonde la Kilombero.

Tunaagiza sukari, wakati tuna aridhi ya kutosha kulima miwa kujitosheleza kuuza nje, Anglian ka nchi kadogo kama Cuba, kanatuuzia sukari, ni aibu.

Tanzania sio masikini ni sisi wenyewe tuu na mipango yetu, akina sisi kazi yetu kuuliza, baada ya rais Magufuli kuamua kujenga Tanzania ya viwanda, kwa nchi inayotegemea kilimo, then Tanzania ya viwanda vya ukweli, ni Tanzania ya agro processing industries, kulikuwa na haraka gani kukimbilia kununua midege, na kutengeneza SGR ukilinganisha na fedha hizo zingewekezwa kwenye kilimo?.

Tuna chuma cha kutosha pale Liganga na Mchuchuma, mali ghafi kuu ya reli ni chuma, na ndio the most expensive na most costly kwenye ujenzi wowote wa reli, chuma tunacho kwanini hatukitumii, ni poor planing tuu na ndio hii imepelekea Kigoma kutelekezwa.
Poleni sana wana Kigoma.
P.
 
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
Tanzania: Rise in Lake Victoria cargo sends Port Authority’s earnings up by 55pc

Can th e same be said for Kigoma? Figures do not lie!
 
Mwanza wana Reli, Barabara, tena za lami.
Kigoma ni ile ile Reli ya mkoloni pekee. So sad kwa kweli [emoji58]
Ni kweli mkuu...Ila in mapema kulaumu kwa kua kuna zoezi la ukarabati wa reli ya zamani ya metre gauge ambapo reli inakua na chuma cha paundi 80 na spidi ya 70km/h. Huenda Kigoma ikapatiwa kipaumbele.
Lakini Kigoma iko kwenye awamu ya pili ya ujenzi wa reli.
Pia kuna ujenzi wa Barbara kama Nyakanazi-Kibondo-Kasulu-Kidahwe kama huu ukikamilika itasaidia usafiri wa mizigo na abiria.
Yote katika yote wanapotoa kipaumbele wanaangalia ni eneo gani lenye faida kubwa 'high turn over' kibiashara.
Huenda Kigoma ikawa chini kidogo ya mwanza ndio maana ikapatiwa kipaumbele.
Kumbuka reli ya Mwanza inapita Isaka(Kahama), Shinyanga na Mwanza. Kwa hiyo tukiangalia kwa undani tutaona Mwanza itahudumia watu wengi hasa kwa upande wa mizigo na abiria. Pia pesa itakayopatikana Mwanza itajenga Kigoma pia.
Tuwe na subira mkuu.
 
.
Ukiniuliza kuhusu uwanja 'mkubwa' mpya wa ndege Chato, hapo sina jibu.
JF ni sharing information, ukiulizwa kitu huna jibu, mwenye jibu anajitolea kukuaelimisha, kumbe na wewe hujui faida za uwanja wetu?.
Karibu kipande hii.

P.
 
Ndege waliishasema ni kwa ajili ya watalii,Wanasema walifufua shirika ili kufufu secta ya utalii, ila hiyo SGR sijui itakuwa ya nani maana gharama hata hao wakihoma na mwanza sidhani kama wataweza.
Hakuna shetani atakaemudu gharama ya SGR ni too luxurious project,
 
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
Kigoma inachangia kiasi gani kwenye pato la taifa na ina idadi ya watu wangapi, je ina hadhi sawa na Mwanza? tuanzie hapo
 
Ni kweli mkuu...Ila in mapema kulaumu kwa kua kuna zoezi la ukarabati wa reli ya zamani ya metre gauge ambapo reli inakua na chuma cha paundi 80 na spidi ya 70km/h. Huenda Kigoma ikapatiwa kipaumbele.
Lakini Kigoma iko kwenye awamu ya pili ya ujenzi wa reli.
Pia kuna ujenzi wa Barbara kama Nyakanazi-Kibondo-Kasulu-Kidahwe kama huu ukikamilika itasaidia usafiri wa mizigo na abiria.
Yote katika yote wanapotoa kipaumbele wanaangalia ni eneo gani lenye faida kubwa 'high turn over' kibiashara.
Huenda Kigoma ikawa chini kidogo ya mwanza ndio maana ikapatiwa kipaumbele.
Kumbuka reli ya Mwanza inapita Isaka(Kahama), Shinyanga na Mwanza. Kwa hiyo tukiangalia kwa undani tutaona Mwanza itahudumia watu wengi hasa kwa upande wa mizigo na abiria. Pia pesa itakayopatikana Mwanza itajenga Kigoma pia.
Tuwe na subira mkuu.
True faida yake ni ya long-term hasa wa awamu zijazo kama zikijenga urafiki Na wafanyabiashara Kwa kuikuza sekta binafsi ili uzalisha uongezeke ili ipatikane mizigo ya kutosha,Lkn kama uchumi unasinyaa ni ngumu Kwa project yeyeto kurudisha gharama Kwa sasa
 
Mkuu Vv, kwanza nakubaliana na wewe, serikali za awamu zote zilizopita, ziliutelekeza mkoa wa Kigoma, kwa kutousisimua uchumi wa Kigoma. Tanzania tunatumia fedha nyingi sana kuagiza mafuta ya kula, Kigoma zao la chikichi linastawi, zao hilo lingeendelezwa kama chai na kahawa, lingekuwa na manufaa makubwa kwa taifa kuliko zao jingine lolote na Kigoma would have been the richest region, lakini mkoloni alijikita kwenye cash crops za demand yake na sio demand yetu kama kahawa, as a result, mikoa wazalishaji wa kahawa ndio the richest regions wakati hiyo kahawa tunawazalishia wazungu, halafu foreign currency yote ya kahawa tunaitumia kuagiza mafuta ya kula ya mawese kutoka Malaysian wakati Kigoma ilianza kustawisha mawese kabla ya Malaysia.

Tulipopata uhuru hadi leo tumeendelea kutembea mule mule wakoloni walimotutembeza.

Tuna agitation mchele wakati bonde Ruvu pekee lingetosha kulisha Tanzania nzima, achilia bonde la Usangu na bonde la Kilombero.

Tunaagiza sukari, wakati tuna aridhi ya kutosha kulima miwa kujitosheleza kuuza nje, Anglian ka nchi kadogo kama Cuba, kanatuuzia sukari, ni aibu.

Tanzania sio masikini ni sisi wenyewe tuu na mipango yetu, akina sisi kazi yetu kuuliza, baada ya rais Magufuli kuamua kujenga Tanzania ya viwanda, kwa nchi inayotegemea kilimo, then Tanzania ya viwanda vya ukweli, ni Tanzania ya agro processing industries, kulikuwa na haraka gani kukimbilia kununua midege, na kutengeneza SGR ukilinganisha na fedha hizo zingewekezwa kwenye kilimo?.

Tuna chuma cha kutosha pale Liganga na Mchuchuma, mali ghafi kuu ya reli ni chuma, na ndio the most expensive na most costly kwenye ujenzi wowote wa reli, chuma tunacho kwanini hatukitumii, ni poor planing tuu na ndio hii imepelekea Kigoma kutelekezwa.
Poleni sana wana Kigoma.
P.
#urakozechane
 
Kigoma inachangia kiasi gani kwenye pato la taifa na ina idadi ya watu wangapi, je ina hadhi sawa na Mwanza? tuanzie hapo
Unategemea itawezaje kuchangia iwapo mazingira ya uwezeshaji hayajawekwa? Unawezaje kutegemea maziwa kutoka kwa ng'ombe usiyemlisha? Mikoa mingine imewezaje kuchangia hadi mingine ishindwe?

Watanzania tumekuwa watu wa ajabu saba, yaani tunategemea kupata matokeo pasipo kuweka misingi imara ya kuwezesha matokeo kupatikana. Ndio maana nchi yetu inaiongoza kwa imani za kishirikina Afrika Mashariki na Kusini, yaani tunategemea mazuri yatokee kimiujiza, tutajirike na kufanikiwa kimiujiza-ujiza. Ni Tanzania pekee ndipo matangazo ya waganga wa kienyeji yamesambaa mitaani na kwenye media maana tunaamini mafanikio ya kimiujiza-ujiza.

Serikali sio mfanyabiashara, serikali ni mzazi anayepaswa kuhakikisha inawawekea misingi imara watoto wake ili wafanikiwe. Kanuni za maendeleo ziko wazi duniani kote, serikali inawezekana ktk miundombinu imara na kuweka sheria na kanuni zinazochochea maendeleo.

Vv
 
Hata reli ya kutoka kahama mpk Rwanda itaanza na kukamili huko Kigoma kutabaki hivyo hivyo. Tuliipenda wenyewe!
 
Mkuu, umenena vema
Wabongo bhana, ukiwa mlevi tu hata unywe maji watasema unakunywa pombe....
Kwa sababu Jamaa anatokea Mwanza itakuwa kajipendelea?
Mleta uzi Gombea urais ili naww tuone Kama utajenga Kwa jirani yako ukaacha kwako.. Kila mtu yuko ktk kutafuta ridhiki na unafuu wa maisha yake... We subiri mletewe reli kigoma...
Mkuu, umenena vema, umenena Kiafrika lakini hujanena kama mtu matured. Wanasiasa wa Afrika hawako matured, ndio maana Afrika tuko hivi tulivyo, tumejaa ubinafsi, uchu wa madaraka na wivu. Hatukubali kama tunafanya makosa na hatuko tayari kubadilika.

Vv
 
Back
Top Bottom