Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Vyamavingi

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
6,044
Reaction score
5,920
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
 
Na
Uliza kwanza kwann CHATO kunajengwa internaional airport, ukijibiwa hilo na jibu la SGR litakuwa tayari mkichwani mwako!
Airport.
Hospital ya Rufaa.
Tanapa HQ kwa kanda hiyo.
Chato NP
Traffic light

Hatupingi maendeleo ila vyote vimefanyika ndan ya miaka miwili.
Pia kuna hambavyo havina tiga...kwa sasa!! Mataa, uwanja.. ..
 
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
Mkuu ongea na figures badala ya hisia.
 
Ingeanza Kigoma mngeuliza tena kwa nini Kigoma
Sio kosa, tungeweka vigezo na kuuliza kwa nini Kigoma kwanza badala ya kwingine.

Nimejitahidi kuweka vigezo/hoja, hoja hujibiwa kwa hoja, sio kwa blah blah.

Vv
 
Hahaha hiyo reli ya SG itabeba nini cha ziada ambacho reli ya mjerumani ilishindwa?! Mnaipa promo ikiisha mtaikana, maana haitaingiza chochote cha ziada tofauti na hii ya mjerumani.
 
Ingeanza Kigoma mngeuliza tena kwa nini Kigoma
Umeoma eeeh... Yaani binadamu ni kusema tu,, Kwa kweli watanzani.. Tunahitaji Elimu kwa ukombozi... Kwani tuna watu wamesoma lakini hawajaelimika... (hawajakombolewa na Elimu waliyoipata)
 
Back
Top Bottom