Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Kwanini SGR inatangulia Mwanza kabla ya Kigoma?

Watu wa Kigoma msipotumia fursa hii ambapo mumepata waziri wa fedha kumaliza miradi ya barabara ya kuufungua mkoa wenu ndo mjue imetoka mtasugua sana benchi mwenzenu waziri wa ujenzi anatumia fursa
Rejea post # 40. Nimeizungumzia Rwanda na mbuga yao moja ya Sokwe inayopokea maelfu ya watalii kila mwaka. Kigoma wanazo mbuga mbili za viumbe adimu duniani, umewahi kujiuliza kwa nini watalii hawatembelei mbuga hizo kwa wingi?

Vv
 
Hivi hamna reli inayo enda Kigoma kweli.. Nakumbuka kwenye maarifa ya jamii.. Wale wenzangu tukumbushane hapa
Kigoma treni linakwenda kila siku Tena Delux full raha kama ndege vile huyu jamaa hana shukrani tu kigoma kama DUBAI siku hizi kuna mahotel mazuri kweli
 
Mkuu Mwanza uchumi wake uko juu ukilinganisha na kigoma, jiulize Kwa nini ndege zinaenda zaidi ya mara 4 Kwa siku, uliza mizigo inayoenda Mwanza na kigoma wapi iko mingi, Mwanza ndio centre ya migodi yote Tanzania mizigo ni mingi, sasa hivi wanajenga kuangalia wapi iko pesa sio mambo ya ujamaa inajenga tu hata kama kuna hasara
Uchumi wa mwanza ni mkubwa kuliko hata wa zanzibar alafu nashangaaga eti zanzibar nako kuna rais makam wa rais na mawaziri ha ha ha ha
 
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
Acha uchochezi
 
Kwa nini haujahoji kwanini imeanzia dar es salaam na sio kigoma?
 
Na

Airport.
Hospital ya Rufaa.
Tanapa HQ kwa kanda hiyo.
Chato NP
Traffic light

Hatupingi maendeleo ila vyote vimefanyika ndan ya miaka miwili.
Pia kuna hambavyo havina tiga...kwa sasa!! Mataa, uwanja.. ..
CRDBank
 
Rejea post # 40. Nimeizungumzia Rwanda na mbuga yao moja ya Sokwe inayopokea maelfu ya watalii kila mwaka. Kigoma wanazo mbuga mbili za viumbe adimu duniani, umewahi kujiuliza kwa nini watalii hawatembelei mbuga hizo kwa wingi?

Vv
Ni kwa sababu watalii wanashindwa kutofautisha viumbe wa huko na wenyeji
 
Na

Airport.
Hospital ya Rufaa.
Tanapa HQ kwa kanda hiyo.
Chato NP
Traffic light

Hatupingi maendeleo ila vyote vimefanyika ndan ya miaka miwili.
Pia kuna hambavyo havina tiga...kwa sasa!! Mataa, uwanja.. ..
Hata Mobutu wa Zaire alifanya hayo lkn leo hii kumebaki magofu.
 
Acha uchochezi
Uchochezi uko wapi hapo? Naona unataka sote tuwe wadumavu wa akili, kuhoji na kutaka majibu ni ishara ya kupevuka kiakili, kinyume chake vitisho hutolewa na watu waoga, wasiojiamini kuwa wanaweza kutoa majibu yenye mashiko.

Vv
 
Reli ya Kigoma Ipo na inatumika mpaka leo... Ila Jamaa swali lake kwanin Mwanza kwanza na sio Kigoma ambao miundombinu haijakaa sawa Bado??
Maendeleo hayana Ukanda kote SGR itafika ni swala la muda tu.
 
Kigezo cha kujenga reli kuelekea mkoa fulani ni lazima mkoa huo uwe unapakana na nchi nyingine nyingi?,uchumi wa kanda ya ziwa ni mkubwa kuliko kigoma hata mabasi yanayotoka ubungo kwenda kanda ya ziwa ni mengi kuliko yaendayo kigoma.Wewe ungekuwa mtoa maamuzi ungejengea watu wa mji wa Kigoma reli ya SG,halafu ukaacha watu wa jijini?.SGR itakapokuwa kama tunavyoelezwa kwa ubora na spidi yake ikifika hadi Mwanza,na nauli ikawa ya mtu mnyonge,wasafiri wa treni wa kwenda Mwanza ni wengi kuliko huko Kigoma.Rwanda yao inapitia Isaka Kahama,uchumi wa Burundi ni dhaifu sana kanda ya ziwa nafuu.Mashariki ya Kongo itaendelea kuhudumiwa kama ilivyokuwa.
 
Kigoma imetengwa kwa muda mrefu, kwenye miradi yote ya maendeleo imepelekewa ikiwa ýa mwisho. Barabara ya lami imepelekewa baada ya mikoa yote kuwa imeshaunganishwa. Umeme wa gridi, itakuwa ya mwisho kuunganishiwa, na hata reli ya SGR itakuwa ya mwisho maana shurti ifike Mwanza kwanza.

Kigoma imepakana na nchi mbili- Burundi na Kongo, Mwanza imepakana na nchi moja pekee Uganda. Pili, Kigoma ina changamoto nyingi za miundombinu, ilipaswa ipewe kipau mbele kuliko Mwanza ambayo ina miundombinu yote, Uwanja wa Ndege na barabara za lami zinazoiunganisha na mikoa yote.

Napenda kujua, kwa nini Mwanza wanatanguliziwa SGR kabla ya Kigoma wakati Kigoma ni lango kuu kupeleka na kupokea mizigo kutoka Burundi na Congo ukilinganisha na Mwanza ambayo ni Uganda pekee?

Vv
Ukiniuliza sababu ya airport ya chato, hata mimi siioni lakini SGR ya Mwanza huikwepi. Ni lazima kama ilivyo airport ya Mwanza. Huwezi kuingiza SGR Kigoma kabla ya Mwanza labda kama una lengo la kujitangaza kwa gharama kubwa mjini Kigoma. Kiuchumi huna sababu ya kuipeleka Kigoma kabla ya Mwanza. Mwanza ni kanda. Inakuwezesha kufika Shinyanga, Mara, Bukoba na kwa sasa Simiyu na Geita. Coverage ya Mwanza ni kubwa. Ukiamua kuipeleka Kigoma, ujue unaufuata mji wa kigoma tu! Burundi, na eastern Congo wana njia tofauti kabisa na Kigoma. Tusidanganyane! Kupakana sawa lakini kuna bishara gani ya maana?

Kulikuwa na hadithi za kutunga toka kwa Zitto juu ya manufaa ya Kigoma over Mwanza, lakini mambo hayahitaji utafiti. Faida ya reli huwa siyo kipato cha moja kwa moja bali ni indirect benefits na hasa offloading ya mizigo ambayo ingepitishwa barabarani.

Ukitaka miradi ambayo haina au haingekluwa na sababu ni kama hiyo Bandari ya Bagamoyo na hiyo airport ya Chato. Lakini, tusisahau airport ya Songwe ambayo tangu imejengwa na kuanza kutumika, wenyeji bado hawajazoea kupanda ndege.
 
Rejea post # 40. Nimeizungumzia Rwanda na mbuga yao moja ya Sokwe inayopokea maelfu ya watalii kila mwaka. Kigoma wanazo mbuga mbili za viumbe adimu duniani, umewahi kujiuliza kwa nini watalii hawatembelei mbuga hizo kwa wingi?

Vv
Naona baadhi munafuata upepo. huko Rwanda kuna watalii maelfu wangapi unaowasikia? Hizo hadithi za Kagame tu. They are nothing! Absolutely nothing! Wanachofanya ni usumbufu EAC tu na kutaka kila sehemu wawepo wakati ni member wa hivi majuzi. Wakipata mradi wanafanya promo utadhani kweli wako fit!
 
Mimi naona ingepeleķwa kwenda huko kigoma kwanza sababu mizigo mingi inaenda sana congo sijui kama wamefanya tathmini ya thamani ya mizigo inayopitia tz kwend congo kupeleka sgr mwanza tutaua routes za mabasi ya abiria
 
Uchumi wa Mwanza umechangamka na no mkubwa kuliko was Kigoma. Simple logic!
Your logic is baseless and nonsense, in short it is proffesorial rubbish!

Hivi kiuchumi, ni kipi kiko Mwanza ambacho strategically kinaikuza Mwanza na Kigoma hakipo?

Tuna viongozi wasio na vision hata chembe, kwa Sera ya viwanda mkoa ambao ungeibeba Sera hiyo ni Kigoma

Ina ziwa lenye samaki wengi na watamu zaidi ya Victoria! Kigoma inahitaji miundombinu tu kama Kigoma International Airport (na si Chato), barabara za lami, umeme wa uhakika ili viwanda vifumuke huko na usafiri wa treni wa uhakika (siyo Deluxe Train inayotumia siku NNE kufika Dar

Kwenye usafiri wa anga sasa, ni nafuu kwenda South Africa kwa ndege kuliko kwenda Kigoma
 
Ubishi mwingine hauna maana. Kupeleka Mwanza inamaanisha wanufaika ni shinyanga, simiyu, mwanza, geita, kagera, mara.

Tabora- Kigoma mnufaika ni kigoma tu. Leo hii kusafirisha mizigo ya congo imekuwa ni bora kuliko watanzania walipa kodi!!
Kasome East Africa Community Costums Management Act ili ujue ni mabilioni mangapi tunapoteza!
 
Kati ya mwanza na kigoma wapi kuna abiria wengi,
 
Kifupi ni ukitengeneza kwenda kigoma ni unawajengea majiran wako , kwenda mwanza unajenga nchi yko
Ndo mana Rwanda wametoa kitikita kikubwa kwenye reli kuelekea kigoma japo imo nchin kwetu
 
Back
Top Bottom