Lakini ni jambo ambalo haliwezekani kumjengea kila Mwalimu wa nchi nyumba ya kuishi Serikali haiwezi kufanya hilo wataongea tu kila siku lakini Kiuchumi hilo haliwezekani, chukulia tu kwa mfano kwa sasa hivi Tanzania kuna mwalimu mmoja kwa kila watoto 100 kwa hali ya kawaida inapaswa kuwa mwalimu mmoja kwa watoto 40 sasa kama kila mwalimu tutakayeongeza huko mbele ya safari ni lazima ajengewe nyumba hiyo fedha itatoka wapi? hapo hapo tunahitaji watoto wetu wale chakula cha mchana shuleni, wanahitaji madaftari, vitabu, na madawati na vitu vingine muhimu kwao sasa hiyo fedha itatoka wapi?
Na usisahau kuwa siku zote bajeti za Elimu hupangwa kiasi ambacho Serikali husika hutumia kwa kila mtoto wa shule na SIYO Mwalimu, kwa kawaida Mwalimu ni mwajiriwa na anapaswa ajitegemee na ataishi wapi haipaswi kuwa kazi ya Serikali, Serikali inapaswa imlipe fedha za kumtosha kuishi ( Na hii ni kwa Waajiriwa wote na sio walimu tu) ili ajitegemee sasa kujenga nyumba ni kuongeza gharama kwa maan ni lazima pia serikali hiyo hiyo ilipe umeme luku kwenye hizo nyumba, ilipe maji, ikarabati zikiharibika n.k sasa hiyo fedha ni kwa nini tusiwekeze kwa watoto wa shule?
Lakini kusema kwamba kila Mwalimu ajengewe nyumba ya kuishi siyo ukweli na hilo haliwezekani, kama Serikali imeshindwa kuwajengea nyumba Viongozi wakubwa ambao ni wachache itawezaje kuwajengea kila mwalimu hapa nchini?