Kwanini Serikali inawajengea nyumba walimu?

Kwanini Serikali inawajengea nyumba walimu?

Shida kuna watu toka wazaliwe hawajui shida humu. Nafikiri mtoa mada hajui vizuri mazingira halisi ya mwalimu. Toka azaliwe "baba mkurugenzi wa madini kanda ya……….., mama barozi wa tanzania………. "Mtu kama huyu hawezi jua shida inayompata mwalimu wa kitanzania anayefundisha Kantalampa, namanyele, Tanganyika masgati, kibungo juu, na lindi vijijini.
Unapokosa la kuongea jf tulia comment za wenzako f.ala we.
Heee! Kwani Kantalamba (siyo Kantalampa) kuna shida gani mkuu? Mbona shule ipo mjini (Sumbawanga) kabisa. Kama unaongelea shule zilizo katika mazingira magumu, wala hiyo usiitaje maana uta-dilute magnitude ya hizo shida kwa sababu shule ile haina tofauti kimazingira na shule nyingine unazozifahamu zenye mazingira nafuu sana.
 
mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa serikali asijitegmee kwenye makazi?
yaani mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la serikali bali liwe tatizo binafsi la mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!
nishakutukana sana ,tena sana japo mimi siyo mwl.
 
mtoa post huna akili tena ww ---- 2 c 2po huku kasanga,kipwa,nkasi na ziwa tanganyika hakutamaniki alafu unalopoka 2
 
Nimekuwa sielewi ni kwanini Serikali yetu inatumia fedha nyingi sana kuwajengea walimu nyumba za kuishi? Ni kwanini hiyo fedha tunayotumia kujenga nyumba za walimu tusiziwekeze kwenye kuboresha Shule zetu kwa kuwanunulia Wanafunzi vitabu au hata kuwapa watoto chakula cha mchana badala ya kuwajengea Walimu nyumba?

Nasema hivi kwa maana sielewi mantiki ya kuwajengea walimu nyumba wakati wao ni waajiriwa kama waajiriwa wengine wote na wanalipwa mshahara sasa ni kwa nini jukumu la wao wataishi wapi liwe la Serikali na siyo lao walimu wenyewe?
Mbona wafanyakazi wengine wa Serikali wanajitegemea kwenye malazi?

Ni kwanini Serikali isijitoe kwenye hili na kuwaacha walimu wapange nyumba au wajenge wenyewe kwa kuchukua mkopo kama wakipenda?


Kwa Hesabu tu ya kawaida haiwezekani kwa Serikali kuweza kuwajengea Walimu wote nyumba huku ni kujidanganya na kupoteza fedha ambazo zingeweza kutumika kuwahudumia wanafunzi ambao hawana mahitaji muhimu na isitoshe wanafunzi wengi wanatoka nyumba ambazo wazazi wao hata chanzo cha kipato hawana sasa ni kwa nini Serikali iwahudumie walimu ambao wana wanalipwa mshahara?

changamoto za nchi hii huzijui!!! nahisi unaishi kariakoo..na haujaitembelea Tanzania yote!!!! unataka nchi yetu iendelee kweli?
unafahamu kuwa kuna maeneo nchi hii hakuna nyumba za kupanga?..unafaham kuwa asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi vijijini? na unafaham kuwa sehemu zingine za nchi zinaitaji nguvu ya ziada ili ziendelee?
 
wewe ndiyo kichaa. watalipwaje night na hawafanyi kazi usiku? watalipwaje posho na hawana safari wala smina?. kubeba kazi nyumbani ni uvivu wao. masaa 8 kwa siku yanatosha kusahisha, kuandaa somo, lesson plan, scheme of work, kuchapa na kufundisha.

Hivi ww mtanzania kwel.....hebu rudia kusoma ulichoandika
 
huyu hamnazo kuna siku, utasema kwa nini serikali inawajengea manesi na madaktar , mawazir na usalama wa taifa
 
Kwani shule zote ziko mijini ambako kuna nyumba za kupanga? shule iliyoko kijijini kwenu ambako mnakunya porini kama wanyama wasipelekwe walimu? au unataka walimu wakaishi kwenye tembe la babu yako alilolijaza mahirizi na ngozi za alubino?

aisee!!! naona unapiga za uso!!
 
Naona waalimu wanatoa uhalisia mfano kuna shule moja wilaya ya Nanyumbu inaitwa Napacho secondari wakati wanaanzisha wanafunzi walikosa eneo la kupanga hasa wale waliotoka mbali na eneo lile ndipo serikali ikaamua kuwajengea wanafunzi hostel pamoja na nyumba za waalimu.kwa hiyo kinachopelekea serikali kuwajengea nyumba waalimu ni mazingira ya tanzania hasa vijijini
 
Heee! Kwani Kantalamba (siyo Kantalampa) kuna shida gani mkuu? Mbona shule ipo mjini (Sumbawanga) kabisa. Kama unaongelea shule zilizo katika mazingira magumu, wala hiyo usiitaje maana uta-dilute magnitude ya hizo shida kwa sababu shule ile haina tofauti kimazingira na shule nyingine unazozifahamu zenye mazingira nafuu sana.
kantalamba iko mjini kabisa ni kama azania kwa dar es salaam au benjamin mkapa
 
Hakuna nyumba za walimu, kuna nyumba za serikali za walimu.
Ushawahi kujiuliza kwa nini kuna nyumba za:
TAZARA
RELWE
UDSM
VETA
BIMA
JWTZ
POLICE
DC
RC
KILOMBERO SUGAR

Taasisi na Mashirika mengi ya umma, yanamiliki nyumba kwa ajili ya wafanyakazi wake.
 
Hakuna nyumba za walimu, kuna nyumba za serikali za walimu.
Ushawahi kujiuliza kwa nini kuna nyumba za:
TAZARA
RELWE
UDSM
VETA
BIMA
JWTZ
POLICE
DC
RC
KILOMBERO SUGAR

Taasisi na Mashirika mengi ya umma, yanamiliki nyumba kwa ajili ya wafanyakazi wake.

Bora umemwambia maana huyu jamaa mtoa mada naona haelewi Mwalimu anavyoishi mazingira magum japo anapata mshahara mdogo ukilinganisha na kada zingine
 
Ni shida pale mtoa mada anapozungumzia masuala ya elimu angali hakwenda shule na kuelimimika.Majimarefu ana uelewa mpana kuliko wewe
 
Serikali inawajengea nyumba walimu kwa sababu vijijini hakuna nyumba za walimu, yaani hata uwalipe milioni sita hawawezi kupanga kwa sababu hakuna nyumba bora za kuishi mwalimu labda wanakijiji wamjengee tembe la kufunikwa na nyasi, kitu ambacho hata wewe ukiambiwa ukaishi humo na wanao na mkeo nadhani utakataaa.

Walimu post zao sio permanent kwa hiyo hawawezi kujenga nyumba zao binafsi vijinini, na ukipelekwa sehemu kama Nkasi vijijini, ujenzi bora unategemea upate vifaa vya ujenzi kutoka Sumbawanga mjini na kuvisafirisha hadi Namanyere (makao makuu ya wilaya) halafu uvipeleke na baiskeli hadi kijijini kwako vilimani huko....hiyo ni adha, aibu and sometimes simply impossible, wacha tu serikali iwajengee nyumba kama ilivyojengea madaktari wa wilayani, hata vijijini zahanati ikijengwa pembeni yake inajengwa nyumba ya daktari...sasa kwa nini shule zinapojengwa zisijengwe na nyumba za waalimu? hata kama shule ipo chini ya mbuyu, mwalimu lazima awe na nyumba sio anashinda chini ya mti analala kwenye tembe...

Wakimaliza nyumba za walimu waendelee na nyumba nyingine za wafanyakazi wa umma. la sivyo hakuna atakayekwenda kufanya kazi vijijini
 
We Unakichaa, Umejiuliza Kwanini Waalimu Hawalipwi POSHO WALA NIGHT NA WAFANYAKAZI WENGINE WANALIPWA WAKATI KAZI WANAZOZIFANYA HADI KULIPWA POSHO WANALIPWA MSHAHARA? Kwanini Hizo Posho Zisiende Kwenye Ujenzi Wa Barabara Vijijini? Umewahi Kujiuliza Mwalimu Wa Digrii Anapoanza Kazi Analipwa Laki Sita Na Daktari Anaeanza Kazi Mwenye Digrii Hy Hy Analipwa Milioni Moja Na Laki Tano? Kwanini Na Wao Walipwe Pesa Zote Hz?Kwanini Wasilipwe Viwango Sawa Na Waalimu? FICHA UJINGA WAKO.

tofauti kati ya mwalimu na daktari,inatokana na mafunzo na umri wa mafunzo. daktari anatumia miaka 5 na wengine inafika miaka 7 inategemea na kozi aliyochukua, lakini walimu mafunzo yao ni miaka 3 zaidi ya hapo wanarudi shule kuongeza mshahara. kwa mantiki hii lazima viwango vya mshahara vitofautiane.
 
Nani alikudanganya kuwa ukichanganya lugha utaeleweka au utaonekana kama msomi? Hovyo kabisa! hayo ndio madhara ya elimu duni mliyookoteza katika shule za kata.

Nilimaanisha matusi... Ukitaka ujumbe ulioukusudia ufike vile unavyotaka, zingatia yafuatayo
1. Muda... zingatia muda ambao jamaa unayetaka kumweleza chochote naye awe na muda
2. Mazingira.. Jambo husika unamwelezea mkiwa wapi
3. Mood...
4 Lugha unayotumia kama ni kejeli au la au ni matusi
 
Nilimaanisha matusi... Ukitaka ujumbe ulioukusudia ufike vile unavyotaka, zingatia yafuatayo
1. Muda... zingatia muda ambao jamaa unayetaka kumweleza chochote naye awe na muda
2. Mazingira.. Jambo husika unamwelezea mkiwa wapi
3. Mood...
4 Lugha unayotumia kama ni kejeli au la au ni matusi
Peleka upumbavu wako kwa wapumbavu wenzako, nani alikuambia mawasiliano hupangwa kama kanuni za hesabu? wewe ninani hapa jamvini wa kuwapangia wachangiaji nini cha kuandika? nenda kuzimu na elimu yako ya kuokoteza!
 
umeanza vizuri ila umemaliza vibaya,ulikuwasahihi kusema wabunge na mawaziri wanalipwa vizuri lkn kugeneralize kuwa watumishi wengine wa serikali wanalipwa vizuri kuliko walimu na Madaktari hauko sahihi labda tutajie n watumishi wapi hao maana ninachokijua mimi serikalini wote wanalia njaa tu, hakuna cha house allowance wala nini labda kwa wakuu wa idara tu
Kwa sababu mishahara yao ni midogo na ujenzi wa nyumba unaondoa gharama za kila mwaka kwa serikali kulipa mishahara mikubwa kwenye bajeti yake. Chukulia hili kwa nini balozi wetu wananunua nyumba nchi za nje wakati wangeweza kupanga!

Hivyo badala ya kumlipa mwalimu tuseme milioni 3 kila mwezi ili kumwezesha kupanga nyumba ya Milioni 1.5, serikali itatumia milioni 1.5 kumlipa mwalimu kila mwezi kwa miaka yote wakati bado ikihodhi nyumba hiyo. Ni mpango mzuri sana kwa kuzingatia mpango wa muda mrefu ila kiukweli mishahara wanayopewa walimu na Madaktari bado haitazami market value ya pango ili kukidhi matumizi ya kawaida. Walimu na Madaktari bado wanapewa mshahara mdogo sana pamoja na kwamba hukaa nyumba za serikali wakati wabunge mawaziri na watumishi wengine wa umma wanapokea mishahara inayopitiza hata gharama za nyumba na usafiri ukijumlisha.
 
Peleka upumbavu wako kwa wapumbavu wenzako, nani alikuambia mawasiliano hupangwa kama kanuni za hesabu? wewe ninani hapa jamvini wa kuwapangia wachangiaji nini cha kuandika? nenda kuzimu na elimu yako ya kuokoteza!

Hata wa milembe huwa wanadhani sisi wazima ndo vichaaa.............

Zamani ilikuwa mtu anaanza kuwa kichaa then anaokota makopo , lakini siku hizi ni kinyume... Watu wanaanza kuokota makopo halafu baadaye wanageuka kuwa vichaa
 
Kama sikosei huyu mleta mada atakuwa mfagizı ofisı ya mkurugenzi wa halmashauri.Hawa huwa wana roho za kwa nini, unamwonea wivu hata mwalimu??Utaratibu ni kwamba warau kila shule kuwe na walimu wanaokaa hapo.Mazingra mengne magumu sana, kumbuka hz shule kila mahala tofauti na ofisi za watendaji wengne.Kwa nn usiseme juu ya polisi,jeshi,maliasilı,madaktarı wa rufaa,bot n.k.Mana hawa wengi wamepewa nyumba za serikali.Watumishi idara zingne hupewa posho ya nyumba kwenye mishahara yao.
 
Back
Top Bottom