Kwanini Serikali haijengi Techinical College Kanda ya Ziwa badala yake wanarundika vyuo vyote Dodoma?

Hii itasomwa? Ikitokea wamesoma ni tiba ya ghiliba na wivu. Hawatasumbua tena hapa
Mtu wenu jiwe alikuwa Rais alishindwa nini kuwajengea hizo technical college Matokeo yake akaenda jenga uwanja wa ndege huko chato maporini, mara lihospital kubwa na kusahau mwanza ka ndio mji mkubwa kanda ya ziwa, so jilaumuni wenyewe
 
Hoja yake inatafuta rationality ya uzi huu
Usirukie kila mkoa wakat mtoa mada kasemea kwa kanda nzima ya ziwa hakuna kikuu cha serikali, kila mkoa serikali yako inaweza kujenga maana vilivyopo
kanda ya pwani udsm,sua,ardhi,mzumbe.
Katikati ya nchi udom.
Nyanda za juu kusini kuna MUST.
Kaskazini kuna ATC.
Kanda ya ziwa kuna PRiVATE cha SAUT.
 
Mimi sioni shida Sana.

Huko Dodoma , Morogoro na Dar Kuna vyuo kibao lakin vimejazwa na wasukuma,wahaya,wanyakyusa na wachaga . wenyeji unaweza husikute hata mmoja darasani zaidi ya kuwa mama ntilie nje


Kipi Bora wasomi au majengo ya vyuo.
Kagera hakunaga vyuo vya serikali lakin ndo mkoa wenye wasomi wengi hapa nchini
Umeacha Wakurya, Wazanaki, Wajita...Kanda ya ziwa kuwa watu makini sana
 
Mkuu chuo kikuu ni kwa ajili ya local communities? Hadi Kigezo cha idadi ya watu kizingatiwe? Je vyuo vikuu vinajengwa eneo fulani kwa sababu ya uchumi mkubwa uliopo eneo husika? Kwani hivi vyuo vunaenda kuuzwa ama kufanya biashara? Shida hasa ya kanda ya ziwa ni nini? Je wanafunzi wake kwa sasa hawapati nafasi ya kuingia katika vyuo vilivyo maeneo mengine ambayo wewe umeamua kuyata kanda? Wacha nane na haya mambo, ni moja hii na ni ya kila mtu.
Watu wananiona kama napendelea kanda ya ziwa kwenye maada hii! Ila naangalia population,economic power ya kanda ya ziwa alafu chuo kikuu cha serkali hamna hii haiko sawa!
 
Huwa nawashangaa badala ya kurundika technical college wao wanarundika ma vyuo vikuu vingi Ili vijana wazidi kuwa masikini.
Mkopo wa mwanafunzi mmoja ingetosha vijana 20 kusoma veta wakawa na tija na kuondoa shida ya ajira nchini.
 
Kusini Mtwara,Lindi na Ruvuma Kuna chuo gani au nao sio Watanzania?
Magharibi pia Kuna chuo kipi?
Ninyi watanzania wa Kanda ya ziwa, Pwani na kaskazini ndio mnajikuta watanzania zaidi ya wenzenu au sio?
Unataja mikoa ambayo ipo karibu na dar Lakin pia hujui kuwa kanda ya ziwa ndo inaongoza kwa kuwa na wasomi wengi Lakin pia fikiria suala la ukubwa wa mkoa husika mtwara,lindi huwezi kupafananisha na Mwanza ambapo ni jiji kabisa.

Lengo sio tu kuweka kila mkoa chuo hapana pia kwenye chuo kuna fursa nyingi za biashara na ukiangalia na ukubwa wa mji husika itasaidia kuleta wafanyabiashara sehemu husika.

NB:Nimesoma kusini ila huko elimu sijui wanaichukulia kama nini yaan kifupi hawaithamini kabisaaa
 
Inasikitisha mno kuona JPM amewaachia watanzania kufikiria kikanda, kikabila, kikabila na kimkoa. Viongozi aina yake hatari mno. Kwani ukienda IFM UDSM UDoM au Sokoine si unakuta makabila kanda na dini zote? So why worry? Au hao wataalam na wanasiasa aliowabeba JPM unadhani walisomea wapi? JPM angekuwa anawapenda wote kanda ya ziwa asingejenga international airport porini angejenga vyuo mnavyolilia. Bahati mbaya dhambi ya ubaguzi iliendekea mpaka chato home ikawabagua wakandaziwa wengine. Subirini wakati mwingine lakini pia watanzania wengine wameshawaogopa sana nyie kumbe mkipata ndio tabia zenu za ubaguzi, wizi, uuaji, matusi, kejeki na majigambo?
 
Hata wakijenga pemba visiwa ndui huko..vitajazwa na watu wa kanda ya ziwa..mana ni wengi pia wana ari ya kusoma..labda tu admission zi seme hawataki wasukuma..wasukuma ni kama maji nchi hii huwezi kuwakwepa kwenye suala la kielimu kwa sasa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nasema hivo baada ya majuzi hapa kuona Serikali imeeanza ujenzi wa DODOMA TECHNICAL COLLEGE wakati Mwanza kuna tawi la chuo cha DIT ambalo linahitaji kupanuliwa na kuwa chuo kamili MWANZA TECHNICAL COLLEGE

Eneo la Kanda ya Ziwa ndo linalotoa wanafunzi wengi sana kwenye TECHNICAL College kulingana na vijana wa ukanda huo kupendelea masomo ya engineering.

Dodoma tayari ina vyuo vingi sana hivyo Serikali iangalie jinsi ya kusambaza vyuo kama hivi maeneo mengine.

Pia kwa Kanda ya Ziwa hakuna huo cha maana cha Serikali kinacho-deal na mambo ya Sayansi na Teknolojia.

Ombi langu kwa Serikali naomba sana Technical College Mwanza ipanuliwe ili watu wasome Diploma mbalimbali za engineering na niikumbusheTechnical za aina hii zipo Mbeya, Arusha na Dar es salaam.
Kwani lazima ijengwe huko Mwanza?

Dodoma ndio Mji mkuu lazima uwe na facilities zote..

Afu hata vyuo vinginevyo viko vingi mikoani kuliko huko Mwanza kwa sababu mbalimbali.
 
Ni kweli ila serkali lazima iangalie mfano mkoa wa mwanza na ukubwa wake hauna chuo kikuu cha serkali! Na ukisema mwanza maana yake ukanda wote wa ziwa!
Kwani vyuo vinajengwa kikanda au kufurahisha miji? Kanda ya Chato hujaziona? Tena ina kila kitu
 
Mkuu chuo kikuu ni kwa ajili ya local communities? Hadi Kigezo cha idadi ya watu kizingatiwe? Je vyuo vikuu vinajengwa eneo fulani kwa sababu ya uchumi mkubwa uliopo eneo husika? Kwani hivi vyuo vunaenda kuuzwa ama kufanya biashara? Shida hasa ya kanda ya ziwa ni nini? Je wanafunzi wake kwa sasa hawapati nafasi ya kuingia katika vyuo vilivyo maeneo mengine ambayo wewe umeamua kuyata kanda? Wacha nane na haya mambo, ni moja hii na ni ya kila mtu.
Achana na mjinga fulani tuu huyo
 
Wewe unafikiri kwann Kalemani kaondolewa?

Serikali haitaki Wasukuma wawe Wataalamu! Ndiyo maana Magufuli alikuwa ana lazimisha MAENDELEO YAENDE KANDA YA ZIWA. Kwa sasa baada ya JPM kuondoka taraatibu Serikali imeanza kurudishareverse ili Wasukuma wabaki palepale.

Sina hakika kama UDSM , UDOM, SOKOINE, IFM au BUSINESS COLLEGE kama wana Branches zao Kanda ya Ziwa( Kwa maana ya Mwanza)

Ukichungulia kwa jicho la tatu unaweza kugundua kuna Ubaguzi wa chinichini kwa Sukumaland.
Kule kazi yao mama ni kilimo na mifugo😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom