Hizo ni shule za tech kama Bwiru na moshi tech!Musoma technical siku hizi haifanyi kazi?
Mtu wenu jiwe alikuwa Rais alishindwa nini kuwajengea hizo technical college Matokeo yake akaenda jenga uwanja wa ndege huko chato maporini, mara lihospital kubwa na kusahau mwanza ka ndio mji mkubwa kanda ya ziwa, so jilaumuni wenyewe
Usirukie kila mkoa wakat mtoa mada kasemea kwa kanda nzima ya ziwa hakuna kikuu cha serikali, kila mkoa serikali yako inaweza kujenga maana vilivyopo
kanda ya pwani udsm,sua,ardhi,mzumbe.
Katikati ya nchi udom.
Nyanda za juu kusini kuna MUST.
Kaskazini kuna ATC.
Kanda ya ziwa kuna PRiVATE cha SAUT.
Umeacha Wakurya, Wazanaki, Wajita...Kanda ya ziwa kuwa watu makini sanaMimi sioni shida Sana.
Huko Dodoma , Morogoro na Dar Kuna vyuo kibao lakin vimejazwa na wasukuma,wahaya,wanyakyusa na wachaga . wenyeji unaweza husikute hata mmoja darasani zaidi ya kuwa mama ntilie nje
Kipi Bora wasomi au majengo ya vyuo.
Kagera hakunaga vyuo vya serikali lakin ndo mkoa wenye wasomi wengi hapa nchini
Watu wananiona kama napendelea kanda ya ziwa kwenye maada hii! Ila naangalia population,economic power ya kanda ya ziwa alafu chuo kikuu cha serkali hamna hii haiko sawa!
Unataja mikoa ambayo ipo karibu na dar Lakin pia hujui kuwa kanda ya ziwa ndo inaongoza kwa kuwa na wasomi wengi Lakin pia fikiria suala la ukubwa wa mkoa husika mtwara,lindi huwezi kupafananisha na Mwanza ambapo ni jiji kabisa.Kusini Mtwara,Lindi na Ruvuma Kuna chuo gani au nao sio Watanzania?
Magharibi pia Kuna chuo kipi?
Ninyi watanzania wa Kanda ya ziwa, Pwani na kaskazini ndio mnajikuta watanzania zaidi ya wenzenu au sio?
Ghiliba haiwaishi kabisa watuHii itasomwa? Ikitokea wamesoma ni tiba ya ghiliba na wivu. Hawatasumbua tena hapa
Kwani lazima ijengwe huko Mwanza?Nasema hivo baada ya majuzi hapa kuona Serikali imeeanza ujenzi wa DODOMA TECHNICAL COLLEGE wakati Mwanza kuna tawi la chuo cha DIT ambalo linahitaji kupanuliwa na kuwa chuo kamili MWANZA TECHNICAL COLLEGE
Eneo la Kanda ya Ziwa ndo linalotoa wanafunzi wengi sana kwenye TECHNICAL College kulingana na vijana wa ukanda huo kupendelea masomo ya engineering.
Dodoma tayari ina vyuo vingi sana hivyo Serikali iangalie jinsi ya kusambaza vyuo kama hivi maeneo mengine.
Pia kwa Kanda ya Ziwa hakuna huo cha maana cha Serikali kinacho-deal na mambo ya Sayansi na Teknolojia.
Ombi langu kwa Serikali naomba sana Technical College Mwanza ipanuliwe ili watu wasome Diploma mbalimbali za engineering na niikumbusheTechnical za aina hii zipo Mbeya, Arusha na Dar es salaam.
Kwani vyuo vinajengwa kikanda au kufurahisha miji? Kanda ya Chato hujaziona? Tena ina kila kituNi kweli ila serkali lazima iangalie mfano mkoa wa mwanza na ukubwa wake hauna chuo kikuu cha serkali! Na ukisema mwanza maana yake ukanda wote wa ziwa!
Kusini ya Ntwara kucheere labdaVyuo vijengwe kusini kwa Tanzania kumesahaulika kwa makusudi sana
Kama mna economic power kwa nini hamjengi hadi mbereko? Economic power gani huko?Watu wananiona kama napendelea kanda ya ziwa kwenye maada hii! Ila naangalia population,economic power ya kanda ya ziwa alafu chuo kikuu cha serkali hamna hii haiko sawa!
Achana na mjinga fulani tuu huyoMkuu chuo kikuu ni kwa ajili ya local communities? Hadi Kigezo cha idadi ya watu kizingatiwe? Je vyuo vikuu vinajengwa eneo fulani kwa sababu ya uchumi mkubwa uliopo eneo husika? Kwani hivi vyuo vunaenda kuuzwa ama kufanya biashara? Shida hasa ya kanda ya ziwa ni nini? Je wanafunzi wake kwa sasa hawapati nafasi ya kuingia katika vyuo vilivyo maeneo mengine ambayo wewe umeamua kuyata kanda? Wacha nane na haya mambo, ni moja hii na ni ya kila mtu.
Kwani lazima kiwe cha serikali?Daaa yaani kanda nzima hakuna chuo kikuu cha serkali kwa kweli maajabu haya!
Kule kazi yao mama ni kilimo na mifugo😂😂😂😂Wewe unafikiri kwann Kalemani kaondolewa?
Serikali haitaki Wasukuma wawe Wataalamu! Ndiyo maana Magufuli alikuwa ana lazimisha MAENDELEO YAENDE KANDA YA ZIWA. Kwa sasa baada ya JPM kuondoka taraatibu Serikali imeanza kurudishareverse ili Wasukuma wabaki palepale.
Sina hakika kama UDSM , UDOM, SOKOINE, IFM au BUSINESS COLLEGE kama wana Branches zao Kanda ya Ziwa( Kwa maana ya Mwanza)
Ukichungulia kwa jicho la tatu unaweza kugundua kuna Ubaguzi wa chinichini kwa Sukumaland.