Kwanini saba iwe moja kwenye masaa?

Kwanini saba iwe moja kwenye masaa?

Kwanza tukubaliane kuwa siku maja ina masaa 24. Na siku inaanza saa sita kamili usiku. Sasa hapo ukianza kuhesabu unaanzia 00:00 lakini kwa wakati huo ni usiku ikifika saa limoja inakuwa 01:00, likifika saa la pili inakuwa 02:00 na kuendelea mpaka 23:00. Hapo inakuwa masaa 24. Sasa kupanga ni kuchagua. Saa yako bwana mleta mada iset namna hii. Ikifika saa sita kamili usiku weka saa yako idisplay 00:00 ukiwa unajua ndio siku imeanza.
 
mbwembwe za mswahili tu, akiona kumekucha ndo anasema siku imeanza anaita saa moja huku kuna masaa 7 yalishapita tangu siku ianze, ndo maana wenyewe huwa wanasema seven a.m.
kwahyo kama mpango wa 666 mnao usema basi safari hii sisi wa bongo ndo tumeutengeneza 🙂
 
Inasemekana ni mfumo wa ki freemasonic, maana inasemekana namna ya freemason ni 6 hivyo kwa usomaji wa saa 7=1, 8=2 kwa mzungumko wote wa saa basi zinabaki 6, ambayo ndio namba ya freemanic
 
Kama mwenzetu mmoja alivyokueleza hapo mwanzoni, utaratibu wa muda unaotawala dunia ni wa wazungu. Tukichukulia kwa Kiswahili au kwa mazoea yetu, tuna ama saa moja asubuhi au usiku, na kwa saa saba ni hivyo hivyo. Kwa utaratibu wa dunia, siku inaanza usiku, pale sisi tunaposema ni saa 7 usiku, ndio mwanzo wa siku/tarehe mpya, ndio maana wao wanasema 1. Tofauti ni kuwa sisi tunatumia zaidi masaa 12, ila wao wanatumia masaa 12 pia na masaa 24 kwa mambo ya utaalamu zaidi.
Tofauti nyingine, ni pale sisi tunapoita ile saa 7 usiku ni usiku, wao wanaita ni 1 asubuhi (am). Saa 1 asubuhi yetu, wao ni mwendelezo wa walichoanza nacho tangu ile saa 7 ya usiku yetu, hivyo wao ni 7am. Saa 7 mchana ya kwetu, kwao (kwa masaa 12) ni saa 1 pm, (kwa masaa 24) ni saa 13, na jioni yao ndio inaanzia hapo.
Thread closed!
Labda kama ni ubishi tu utaendelea.
 
Habari zenu ndg WA jamii forum,,Mimi Nina swali/maswali ambayo nahitaji kujua kama ifuatavyo
Kwanini katika mzunguko WA dunia tunatumia masaa ambayo so sahihi?kwa maana ya kwamba tunatumia;

7kama SAA moja
8kama SAA mbili
9kama SAA tatu ,n.k..
nadhani hapo umenipata sasa swali langu la msingi kwanini tusitumie saa moja kama 1 badala ya 7,au saa mbili kama 2 badala ya 8 n.k
Msaada tafadhali
saa ilianzia libya au algeria,sikumbuki vizuri,ilikua inaenda na jua kwa kupima kivuli,likitoka alfajiri hadi saa sita,kivuli kunakua sawa na kipimo,kisha saa saba kivuli kinaanza kuangukia upande mwingine,hapo walianza kuhesabu upya,yaani moja,ndo tulipopatia mfumo wetu
 
Hapana iko hivi, kwa kiswahili waweza rekebisha saa yako isome kiswahili which mean ikiwa moja utasoma saa moja ila ukiweka kwa kizungu ndipo kwenye moja utasoma saa saba na kwenye mbili utasoma saa nane hiyo ni kwa kingereza si kiswahili, hope umenielewa samjarusha
 
7am, means, 7 hours has passed since the beginning of the day, 12.01am

Kiswahili sisi hatujagundua chochote kuhusu masaa na mwenendo wake.

Tukubali kuwa tunatumika na wazungu
 
Mtoa mada kama nimekuelewa vizuri swali lako ni kwamba kinachoonekana katika saa ndio kitamkwe au wakati uliopo ndio uandikwe kwenye saa, badala ya hii "viceversa" tunayotumia, kwa maana ya kwamba saa 7 kutamka saa 1.
Kwa Tanzania tunatumia huo mfumo wa viceversa mfano sasa hivi ni saa kumi na moja kamili jioni lakini kwenye saa yako ukiangalia ipo 5:00pm.
Kwa nchi za ulaya kilichopo kwenye saa yako ndio kinachotamkwa kwa maana ya kwamba, tukirudi katika mfano wetu wa saa kumi na moja kamili jioni wao wanasema ni saa tano kamili jioni kama ilivyo kwenye saa.
Kwa nchi za kiarabu, tukirudi kwenye mfano uleule wa saa kumi na moja jioni wao wanasema ni saa kumi na moja hivyo hivyo na saa zao zinaonesha hivyo hivyo Saa 11.

Swali la kujiuliza sisi Watanzania utaratibu huu wa kutamka viceversa tumeupata wapi?

Kwa mtazamo wangu hii imetokana na kuchanganya tamaduni tofauti za mataifa ya nje hasa waarabu (waislamu) na waingereza.
Kwanini?

1. Uarabuni siku inaisha saa kumi na mbili jioni. Kwahiyo saa moja jioni ndio saa la kwanza kwa siku mpya na tarehe mpya.
2. Waingereza siku inaisha saa sita usiku, hivyo ikiingia saa saba usiku kwao ndio saa la kwanza na tarehe mpya.

Sasa sisi baada ya utawala wa mwarabu, alipokuja mwingereza tumechukua utamaduni wa mwarabu tukachanganya na mwingereza tukapata kitu chetu "viceversa". Saa zetu tunaziweka zisome kingereza lakini kutamka, tunatamka kwa kiarabu. Matokeo yake ndio hivyo 5:00pm tunasema saa kumi na moja.
 
7- 1= 6
8- 2 = 6
9- 3= 6
Hapo ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita sitini na sita. (Ufunuo 13 : 8)
 
Ndiyo maana ni muhimu sana kuzingatia kutaja eneo ulipo unapotaja saa. Kwa mfano nikiwa bongo sasa hivi ni saa 10:59 jioni kwa saa za Afrika Mashariki(EAT?) Yeyote aliye upande mwingine wa Dunia atatumia time zone yetu kujua unamaanisha saa ngapi kwa GMT. Suala la inasomekaje kwenye saa yako inategemea uelewa wako kuhusu siku/terehe mpya inaanza wakati gani. Mimi kwa mfano; huwezi kunishawishi eti nianze siku usiku wa manane kama desturi ya Warumi wa kale ilivyo! Kwa hiyo ninaanza siku na tarehe mpya saa 12:00 jioni na inaisha saa 11:59 jioni. Kwa hiyo wakati wewe unasubiri usiku wa saa sita ndiyo uingie Alhamisi, mimi nitakuwa nimeianza tangu saa kumi na mbili jioni hii.
 
BaKita wanatakiwe watufumbulie hili na ikiwezekana moja iitwe moja na saba iitwe saba..
ndio maana unaambiwa Tanzania ni magenious maana mambo yao ni complicated sana....mtoto wakati yuko nyumbani anafundishwa saa kwa kilugha ,,akienda madrasa anafundishwa kiarabu mara sijui alaasir au adhuhur au magharib...akienda english media anajazwa na oclocks na 2300hours ...akiiingia mtaa anaambiwa hii ni mida ya wanga...yaani huu mchanyato ukiweza kuumaster ni lazima uwe genious.
 
Wanageuza mambo wazungu, sio watu wazuri...............................
 
Hii ni elimu ya namba(ni pana zaidi kiroho) kwa mfano kama ni saa 7 halafu saa inaandika 1, bhasi chukua 7-1=6(namba ya uasi), kama ni saa 8 ila saa inaandika 2, chukua 8-2=6 ama kama ni saa 10 halafu saa inaandika 4 bhasi chukua 10-4=6 yaani hii inaitwa 666(ikiwakilisha uasi wa mwanadamu anayelazimisha kuabudiwa kama Mungu) =pope, unajua vitu huanzia kutokea ktk ulimwengu wa roho kisha huja ktk ulimwengu halisi, shtuka chukua hatua kwa kumsoma Pope Gregorian X111 kisha utajua jinsi alivyobadili majira, mtafute Bwana ungali hai, barikiwa.
 
Habari zenu ndg WA jamii forum,,Mimi Nina swali/maswali ambayo nahitaji kujua kama ifuatavyo
Kwanini katika mzunguko WA dunia tunatumia masaa ambayo so sahihi?kwa maana ya kwamba tunatumia;

7kama SAA moja
8kama SAA mbili
9kama SAA tatu ,n.k..
nadhani hapo umenipata sasa swali langu la msingi kwanini tusitumie saa moja kama 1 badala ya 7,au saa mbili kama 2 badala ya 8 n.k
Msaada tafadhali
Nadhani unajua kua dunia imitawaliwa na 666 so kila saa ni 6


Mfano SAA 9 ni 3 je 9-3
SAA 4 ni 10 je 10-4
Usiumize kichwa

Hata ukija masaa24 utakua hujakwepa kitu cc huwa tunasema Massa 24 ndio kiswahili

Mfano kwakiswahili SAA 7 ni 13 je 13-7

Mfano SAA 11 ni 17 je 17-11
 
Huo n mpango wa Freemasonry kutumia hayo masaa ili tuwetunazungukia ktk namba za shetani(666)ambayo n pnga Kristi. Chukua 7-1=6,8-2=6...huo n mpango wa kshetan
 
Habari zenu ndg WA jamii forum,,Mimi Nina swali/maswali ambayo nahitaji kujua kama ifuatavyo
Kwanini katika mzunguko WA dunia tunatumia masaa ambayo so sahihi?kwa maana ya kwamba tunatumia;

7kama SAA moja
8kama SAA mbili
9kama SAA tatu ,n.k..
nadhani hapo umenipata sasa swali langu la msingi kwanini tusitumie saa moja kama 1 badala ya 7,au saa mbili kama 2 badala ya 8 n.k
Msaada tafadhali
Swali zuri sana, ntakujibu kama ifuatavyo..
_Chukua hyo 7 toa 1, jibu utalipata kichwa.
Chukua hyo 8 toa 2, jibu unalijua.
_vhukua 9 toa 3, utapata jibu.
NB: jibu utakalopata katka masaa yote yatafanana.. Sasabas tutafute maana ya hyo namba.
666
 
Habari zenu ndg WA jamii forum,,Mimi Nina swali/maswali ambayo nahitaji kujua kama ifuatavyo
Kwanini katika mzunguko WA dunia tunatumia masaa ambayo so sahihi?kwa maana ya kwamba tunatumia;

7kama SAA moja
8kama SAA mbili
9kama SAA tatu ,n.k..
nadhani hapo umenipata sasa swali langu la msingi kwanini tusitumie saa moja kama 1 badala ya 7,au saa mbili kama 2 badala ya 8 n.k
Msaada tafadhali
Ni opposite yake kwa saa ya mshale zinaangaliana.....ilipokaa saba ukacross kwa juu unaona zinatazamana
 
Habari zenu ndg WA jamii forum,,Mimi Nina swali/maswali ambayo nahitaji kujua kama ifuatavyo
Kwanini katika mzunguko WA dunia tunatumia masaa ambayo so sahihi?kwa maana ya kwamba tunatumia;

7kama SAA moja
8kama SAA mbili
9kama SAA tatu ,n.k..
nadhani hapo umenipata sasa swali langu la msingi kwanini tusitumie saa moja kama 1 badala ya 7,au saa mbili kama 2 badala ya 8 n.k
Msaada tafadhali
Watanzania Tunaanza siku asubui. Wazungu saa 6 tukianza asubui tutakuwa nyuma masaa 6
 
Mazoea yetu ya kufanya mambo bila ya tafakari.
sisi tunafuata utaratibu wa wakoloni waliotutawala...mbona wachina wanasheherekea mwaka mpya kivyao ...sisi bado tunatawaliwa na ndio maana vitu vingi tunaiga toka kwao ila wachina majority wanabuni wenyewe
 
Back
Top Bottom