Kwanini PCM wengi wanaenda commerce na BAF?

Unajua kusoma uhandisi ni mchaka mchaka pale UDSM watu wanaumia kwelikweli lakini wakisha maliza hawathaminiwi wanajitafutia kazi na mishahara midogo kweli mtu amehitimu uhandisi analipwa laki mbili au tatu kwa muhindi au muarabu? Hizo opportunity unazozisema ni zipi? Ukiangalia mwenzako aliyesoma uhasibu au Marketing kakuacha mbali kimaisha! Nakumbuka kuna jamaa mmoja alisoma uhandisi na ilikuwa katika Engineers' day 2008 akasema anaapa watoto wake hata wahamasisha wasomee uhandisi maana yeye amesota sana! Hii ERB imeanzishwa vizuri lakini wanafaidika wachache hawatetei wahandisi kabisa zaidi ya kuwakandamiza! Katika wahandisi 10 utakuta 1 au 2 ndio wanapata chance ya kuwa ktk mashirika mazuri na wanapata maisha bora! Hili suala ni la kuliangalia sana ! Na hata wengi waliohitimu Uhandisi still wanaendasoma MBA ambayo ni masters ya Biashara

Kwangu mimi siamini kwamba kuna fani mbaya isiyolipa. Hii inategemea mtu mwenye fani hiyo anauwezo kiasi gani wa kuitumia kumletea kipato.
Nina mfano hai ya jinsi mhandisi wa mitambo mmoja(Mechanical Engineer) ambaye alimaliza chuo miaka hii ya 2002-4 aliyekataa katakata kuajiriwa,lakini leo anaishi mjini kwa kuservice generators tu kiasi kwamba ana hela za kumtosheleza.
Wapo wengine wengi pia wenye kampuni za ujenzi na consultancy firms ambazo zimeanza kukua taratibu taratibu.
Kwangu mimi binafsi hakuna fani nzuri kama uhandisi.Inategemea mtu unaitumiaje.
Tatizo lipo kwenye namna elimu yetu inavyotolewa. Huwa tunajiandaa kusolve madesa mengi ili tufaulu mitihani na kuwa na GPA kubwa badala ya kujituma kuwa creative ili tunapoingia kwenye system tuweze kuwa na uwezo wa kusimama as individuals with ability to sell our skills to get money.
Well, wanaoamua kusoma biashara wanasababu zao za msingi na siwezi kuwalaumu.
Ntalaumu sana kama watu tuna fikra kwamba engineering ya jana ndio itakuwa ya leo na kesho.Mishahara ya wahandisi itabadilika tu kama nao watakuwa na demand ambayo waajiri watakuwa na kila sababu ya kuhakikisha wanawalipa vizuri ili wasiwakimbie.
Kwa ujumla idadi wa wahandisi inapungua sana wakati kazi zao zinakuwa nyingi sana. Mfano, project za maji zilizopo leo ndani ya nchi hazina wahandisi wa kutosha wa kuzisimamia na kuziendeleza ili ziwe sustainable.
Na tatizo hilo la wahandisi lipo pia kwenye construction, power generation etc etc.

Tusisahau, Times Change
 
Siyo PCM tu hata PGM ambao huwa wanandoto za kurusha ndege lakini wanakuwa wahasibu! Tanzania Bana
 
Kwa kuwa sekta zote Tanzania zinatawaliwa na wanasiasa na ili ufanikiwe huhitaji kwenda kusomea uhandisi ambayo ni njia ndefu kwanini wasitafute njia fupi na inayokupeleka kimoja jikoni?

Sekta ya kuuza na kununua imepanuka haraka na ndiyo inayotajisha haraka na imekuwa sehemu ya siasa Tz

Hakuna utashi wa kisiasa kufanya watu wajenge utaalamu wao katika fani wanayoitaka.

Nakumbuka wakati nasoma o-level kazi nyingi zilikuwa zikionyesha viwango vya mishahara kulingana na fani mtu aliyosoma. Ni aghalabu ungemkuta katibu wa siasa wa chama anapata mshahara mkubwa kuliko daktari, lkn leo katibu wa ccm wilaya anamlipa mshahara Daktari anayeanza kazi na bado anabakiwa na mlo wa mwezi.
 
Kwa kuwa sekta zote Tanzania zinatawaliwa na wanasiasa na ili ufanikiwe huhitaji kwenda kusomea uhandisi ambayo ni njia ndefu kwanini wasitafute njia fupi na inayokupeleka kimoja jikoni?

Sekta ya kuuza na kununua imepanuka haraka na ndiyo inayotajisha haraka na imekuwa sehemu ya siasa Tz

Hakuna utashi wa kisiasa kufanya watu wajenge utaalamu wao katika fani wanayoitaka.

Nakumbuka wakati nasoma o-level kazi nyingi zilikuwa zikionyesha viwango vya mishahara kulingana na fani mtu aliyosoma. Ni aghalabu ungemkuta katibu wa siasa wa chama anapata mshahara mkubwa kuliko daktari, lkn leo katibu wa ccm wilaya anamlipa mshahara Daktari anayeanza kazi na bado anabakiwa na mlo wa mwezi.

Umenena ukweli ! Hili ni jambo sugu sana
 
Ni kweli ndugu yangu kuhusu hili,ila kwanza unapoanza ku judge kuhusu hili lazima uangalie mambo mengi sana na si vitu vidogovidogo kama ulivyoanza kwa kusema kwamba si eti BAF ni rahisi au vipi. jibu rahisi ni kwamba WANADHANI UKISOMEA MABO YA FEDHA BASI WE NI FEDHA FEDHA KILA WAKATI NA WANAOSOMEA FEDHA WAO WANA FEDHA KIBAOOOOOO.. ULIMBUKENI PIA.
 
Hamjui Tanzania( Africa in general) mambo yote ni opposite ya dunia inakokwenda! siasa ipo juu ya technical issues, so is wastage of time hadi hapo siasa itakapothamini vipaji! Hata wahasibu hawalipwi sana basi tu sababu wanashika hela wanajipangia, ila uhandisi unalipa tz kama utajiajiri! But wote wajiajiri itakuwaje?
 
Kwanza jamani ukisoma hiyo Engineering ni lazima ufanye kazi bongo tu??Kwanza engineering unaweza kwenda popote duniani na ukapata kazi je hayo masomo yenu B.Comm na BAF (Bachelor of Accounting and Finance) pia yanakuwaje??Maana mfano Dubai sasa engineering inalipa sana tena sana,ila kila mtu na mtazamo wake,Nadhani ukiwa shule ukichukua masomo nadhani ni vizuri kufikiria je hii kazi nitaipata hapa hapa Tanzania au popote pale??Nadhani hiyo ndio point,zaidi ya hapo mambo ya kusoma masomo kila mtu anasoma hayo hayo inakuwa kuwaste time na kupoteza mda sana yaani!!
 
Bongo hakuna uwiano mzuri wa kipato baina ya fani moja na nyingine
Mfano angalia mshahara wa mwalimu mwenye shahada ya kwanza linganisha
na mshahara wa mhasibu mwenye shahada ya kwanza ni tofauti kabisa, ni hivyo
hivyo kwa madaktari na wahandisi. Kifupi ni kuwa watu wamechoka kuhesabiwa hela mkuu wanataka waende kuhesabu wenyewe, Kusema masomo ya uhandisi magumu sio sababu
kwani mbona watu wanamaliza kula siku na digrii zao.
 
Tatizo kubwa ni umaskini vijana wanadhani wakisoma masomo ya biashara watapata pesa nyingi na kuwa matajiri.Vyuo vingeweka msisitizo kama umesoma Sayansi basi lazima chuoni ukasome kozi za Sayansi na sio Biashara, kila kozi inalipa
 
Fuculty of engineeringfoe iliharibiwa na prof ninatubu mathias lema, na kundi lake

NDUGU KAMA ULIKUWA AKILINI MWANGU;HUYU MZEE AMIARIBU KABISA ILE FACULTY MI NI MMOJA WA PCM BOYS NILIMALIZA 2003 NDUGU 2006 NILENDA OPEN KUSOMEA BBA GENERAL 2009 NKALA SHAVU SASA NAKULA KIPUPWE MOJA YA KAMPUNI KADHAA NCHINI YALIYO KUWA REG NA BRELA..WAMEWAFANYA MA ENGINEER WENGI SANA KUISHI MAISHA MBOFU MBOFU.....WAKATI NAAJIRIWA WALINIULIZA MBONA UMESOMA ENGINNERING NA HUKU SIKUWADANGANYA ENGINEERING NI MATESO..NAITAJI KUISHI MAISHA YENYE FURAHA NA AMANI..UWEZIKUWA NA MATATIZO KWENYE NDOA HADI KAZIN NO...SO KAMA UMEONA THREAD MOJA NIMEONA WAKINA MAYO NA WENZKE WALITUKIMBIZA SANA SANA YAANI MI SOMO LA YULE MPUUZI NILILWEKA PENDING KWA SUP HAMAD AKAJA KUNIULIZA MBONA KILA MWAKA UKO SUPP YANGU NKAMWAMBIA NAITAJI KUMALIZA CHUO NIKIBEBA VYOTE NAACHA VYOTE...ELIM YA ENGINEERING NZURI SANA LAKINI SI KWA TANZANIA...NA NAHISI WALIMU WENGI WA ENGINEERING WAMESOMA KWA SHIDA SANA SO WANAKUWA KAMA WANALIPIZA MATATIZO WALIYOYAPATA NIKIMNKUU DK MMOJA ishengoma wa COMPUTER..JAMANI BADO YUPO 1999 TUKIINGIA ALIKUWA GUMZO TUKAOMBA KWELI MUNGU 2002 KICHWA KIKARUDI TOKA NORWAY...AISEE SIKUMOJA NIKAMUULIZA DK MBONA WATU WANAKUOGOPA NA WANADAI UNA SIFA MOJA ULISHAWAHI KUMWONDOA MTOTO WA DADAKO//NA WA KAKAKO WA DAMU HAPA ENGINEERING ALIJIBU KAMA MI NILISOMA KWA SHIDA LZIMA NAO WAANGAIKE..LOH SIKUAMINI ILE SENTENSI MPAKA LEO...SO KILE KITIVO NI SHIDA TUPU NAKUMBUKA NIKIWA MWAKA WA PILI NILIENDA KUOMBA NAWEZA KUANZA MWAKA WA KWANZA BCOM...U CAN IMAGINE ......HAMAD NAMALIZA HATA JOO NKAONA KAMA MATESO TU...TUNAIAJI WATU WENYE KUFUNDISHA KWA MALENGO MEMA...HIVI HUYU LEMA BADO MKUU WA CIVIL ENGINEERING???
 
jamani, ngoja kwanza mi nihakikishe namaliza civil halafu ndo nije kuandika hapa!:mod:. maana nahisi ya kusimulia ni mengi! ila all in all engineering is good! sema kuna uzembe wa wanafunzi na wafundishaji! plus everybody anaweke hela mbele! ngoja kwanza nikamue, nina assignment ya Prof. mayo na prof. lema ninatakiwa kusubmit!

see you in two months when I shall be a graduate I pray!
amen!:smow::grouphug::pound:
 
Nadhani nashawishika kukubaliana na wewe. Kwa kweli watu wengi wameacha kufuata interest na kuamua kufuata hela. Yaani pesa ndo imekuwa interest yao. Hii inatokana na mambo mengi lakini, changamoto za kiuchumi, lakini pia, nahisi uzalendo uliopungua, labda kutokana na watu kukata tamaa na kupoteza imani na nchi yao!
 
Kwanza jamani ukisoma hiyo Engineering ni lazima ufanye kazi bongo tu??Kwanza engineering unaweza kwenda popote duniani na ukapata kazi je hayo masomo yenu B.Comm na BAF (Bachelor of Accounting and Finance) pia yanakuwaje??Maana mfano Dubai sasa engineering inalipa sana tena sana,ila kila mtu na mtazamo wake,Nadhani ukiwa shule ukichukua masomo nadhani ni vizuri kufikiria je hii kazi nitaipata hapa hapa Tanzania au popote pale??Nadhani hiyo ndio point,zaidi ya hapo mambo ya kusoma masomo kila mtu anasoma hayo hayo inakuwa kuwaste time na kupoteza mda sana yaani!!

naona kama elimu ya bongo unaisikia tu ilivyojaa madudu,watu wa coet wanatumia vya mwaka 82 kwenye practical, au unaambiwa kifaa flani hakipo nenda ukadese.nani atakuajiri huko Dubai wakati elimu yako ya Madesa?
 
Sera mbovu za Serikali ya kutoangalia jinsi ya kuwatumia watu wa Science!ie Engineers.Hakuna mvuto wa makusudi wa kushawishi vijana kupenda masomo hayo kwa maana kuwa ni wachache sana wanaweza kupata ajira nzuri afterwards.
Tukumbuke nchi itaweza endelea kwa mambo makuu mawili yaani viwanda na Kilimo.Sasa viwanda na kilimo ni lazima viwe Scientific na kuyafanya hayo ni watu wa science ndio wanahitajika.
Ukikosa mvuto wa aina hiyo basi haya tunayoyaona ndio hutokea.
 
Nchi yetu haina vipaumbele vya maendeleo yetu.Tunaenda kama kishada kilichakatika uzi! Kuna kiongozi aliulizwa vipaumbele vya TZ ni vipi, yeye alijibu vipo vingi sana!!!
 
Mkuu nadhani ingekuwa vizuri kama ungekuja na stats na facts hapa useme mwaka fulani wanafunzi(idadi) fulani waliomaliza PCM au PCB na kufaulu vizuri walikwenda kusoma Biashara chuo(vyuo) fulani na fulani.Ninavyofahamu wanafunzi wa high school wanaofanya hii michepuo siyo wengi kama wa arts au biashara labda iwe imebadilika hivi karibuni.Sasa kama unasema wengi wa hawa PCM na PCB wanasoma biashara,na wale wanafunzi wanaosoma biashara wanakwenda vyuo gani?Au tuna vyuo vingi vya biashara siku hizi kiasi kwamba enrollment imeongezeka sana?Ina maana huko engineering intake imepungua sana kwa vile hakuna waombaji manake wengi wanaenda B.com and the likes?Halafu kwa mfano kama mhitimu wa PCM(division one point 5) akaomba B.com pamoja na mhitimu wa ECA(division two point 10) nani atapewa kipaumbele?
Kifupi lete data kwanza tuone kabla ya kukadiria madhara yake.

Haya maswali yote unamuuliza nani?....kwanini wewe usinge tafuta data za kuja kupingana nae kuwa mwaka fulani mpaka fulani wanafunzi walienda eng. walikuwa hivi compare na wa biashara...so muazisha thread akachakachue kichwa chake aje na fact....unamuuliza na kumuelekeza..na wewe umesoma masomo magumu.Hayo..Hayo...Kila kitu data?
 
Hata hakuna hata ya kufikiri kuhusu hoja hii, ni wazi kuwa tz nw utaalam hauthaminiki kbs, sasa ya nini watoto wa watu wakaumize vichwa vyao hali akihtimu bdo atatakiwa kwenda kuwanyenyekea wanasiasa waliotoka vyuoni na gpa za >2. Kama kuna shortcut hata mimi ningepita
 
Back
Top Bottom