Wolle Melkas Fernando
JF-Expert Member
- May 4, 2016
- 218
- 297
Niliuliza hili swali kupata maoni, sio hapa tu ni kwenye majukwaa mbalimbali, Asante kwa wote waliotoa maoni yao.
Lakini kwa ufupi misaada na Mikopo kihistoria vilianza miaka ya 1945 na ilikuwa baada ya vita kuu ya pili ya dunia kwa malengo mawili;
i) Kujenga miundombinu iliyoharibiwa wakati wa vita na jukumu hili ilipewa Benki ya Dunia.
(ii) Na lengo la pili lilikuwa ni kuharakisha maendeleo ikiwemo biashara na kudhibiti masuala yote yahusuyo Fedha Duniani, jukumu hili likawa ni la Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Shirika la Biashara Duniani.
Lakini kwa pamoja mashirika haya waliyaweka pia kwaajili ya kudhibiti ama kuzuia kutokea tena kwa mdororo wa uchumi (Great Economic Depression) uliowahi kutokea miaka ya 1930's (Hawa watu wana akili , kumbuka Kati ya wadau 700 waliokuwa wanajadili haya, hakuna mdau hata mmoja aliyetoka Afrika kwa ujumla).
Mwaka 1946 na 1947 nchi za Ulaya zilichukua mikopo na misaada kutoka kwenye mashirika haya. Nchi kama Ufaransa, Denmark, Netherlands na Luxembourg waliweza kufanikisha kuunda upya nchi zao na kufuta uharibifu wote uliosababishwa na vita, pamoja na kujenga uchumi wao. Kwa kiasi kikubwa taasisi hizi za Kimataifa zilimudu kudhibiti na kuchochea Uchumi wa Dunia.
Sasa ni nini kilizikuta nchi za Afrika ikiwemo Tanzania ambapo nchi hizi zinaonekana kuwa na ugonjwa sugu wa Umaskini usiosikia dawa licha ya kupewa mikopo na misaada ya matrilioni ya Fedha? Tutaona Part (ii)
Lakini kwa ufupi misaada na Mikopo kihistoria vilianza miaka ya 1945 na ilikuwa baada ya vita kuu ya pili ya dunia kwa malengo mawili;
i) Kujenga miundombinu iliyoharibiwa wakati wa vita na jukumu hili ilipewa Benki ya Dunia.
(ii) Na lengo la pili lilikuwa ni kuharakisha maendeleo ikiwemo biashara na kudhibiti masuala yote yahusuyo Fedha Duniani, jukumu hili likawa ni la Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Shirika la Biashara Duniani.
Lakini kwa pamoja mashirika haya waliyaweka pia kwaajili ya kudhibiti ama kuzuia kutokea tena kwa mdororo wa uchumi (Great Economic Depression) uliowahi kutokea miaka ya 1930's (Hawa watu wana akili , kumbuka Kati ya wadau 700 waliokuwa wanajadili haya, hakuna mdau hata mmoja aliyetoka Afrika kwa ujumla).
Mwaka 1946 na 1947 nchi za Ulaya zilichukua mikopo na misaada kutoka kwenye mashirika haya. Nchi kama Ufaransa, Denmark, Netherlands na Luxembourg waliweza kufanikisha kuunda upya nchi zao na kufuta uharibifu wote uliosababishwa na vita, pamoja na kujenga uchumi wao. Kwa kiasi kikubwa taasisi hizi za Kimataifa zilimudu kudhibiti na kuchochea Uchumi wa Dunia.
Sasa ni nini kilizikuta nchi za Afrika ikiwemo Tanzania ambapo nchi hizi zinaonekana kuwa na ugonjwa sugu wa Umaskini usiosikia dawa licha ya kupewa mikopo na misaada ya matrilioni ya Fedha? Tutaona Part (ii)