Kwanini Mungu yupo?

basi tuhitimishe Mungu ni nadharia ya mwanadam kukabiliana na hofu na kujipa tumaini
 
Umejitahidi at least
 
Mungu aliyetuumba binadamu wote na kuumba ulimwengu wote
Kwa muktadha huo, wewe unatambua uwepo wake Mungu, ila unatamani kujua kwanini Mungu yupo?

Jibu:
Mungu muumbaji wa ulimwengu wote wa kiroho na halisi (Spiritual and physical), yupo ili ulimwengu wote wa kiroho na halisi (Spiritual and physical) uwepo. Bila uwepo wa Mungu hakuna ulimwengu wote wa kiroho na halisi (Spiritual and physical).
 
kuna hoja nzito hapa.
najarib kufikiri kwamba bila uwepo wa hofu na tumaini, je mwanadam ataishi kwa mizania gani? ni sawa na kujadir uoteshaji wa mmea bila pa wapi utashikiria hata kama si lazma udongo! ndo Mungu, kwa mtazamo wangu, akaibuliwa.

ninachokubaliana na wewe ni kwamba huenda tungekuwa salama zaid kama tungeishi kwa kanuni za asili ikiwemo survival of the fittest, kuliko mtafaruku uliozalishwa na nadharia ya Mungu, mungu, imani na dini!

Adui yetu mkubwa ni KESHO!
 
 
Nilikuambia mwanzo kua uki set vi principle vya kijanja janja kwa malengo ya kuthibitisha jambo lisilo na uhalisia itakuwa ngumu sana kufika hitimisho wa jibu lako bila kuivuruga principle

Kwahiyo unakana hoja yako ya awali uliyosema kuwa Energy haiumbwi?
 
Yeye yupo kwa ajili ya kumuabudu Mungu tu?

Ni kumuabudu tu au kuna kingine cha ziada?

Yani ni sawa uajiri watu uwe unawalipa mshahara mnono kwa kazi ya kukusifia tu

Inshort umemfanya Mungu wako aonekane hana malengo au sababu za msingi za yeye kuumba watu

Mungu katuumba kwa kazi ya uchawa
 

Kwanza lazima ujue Mungu anapotaka kuumba kitu anakiamuru kiwe na kinakuwa wala katika hilo hahitaji ushauri kutoka popote, Yeye ndiye Causa causan.

Kwa yeye kukuumba wewe ili umuabudu ni kwa ajili ya faida yako wewe kwani unapomuabudu anakulipa, kifupi ni kwamba katika ibada ni wewe ndiye unafaidika wala sio Yeye kwani Yeye amejitosheleza na kila kitu ukiwemo wewe ni mali yake na kama angependa angekuumba nyumbu ili ukawe chakula cha fisi na mamba.

Umshukuru Yeye kukuumba binadamu unayejitambua basi toa shukrani zako kwake aliyekuumba na fanya ibada kwake.
 
Hakukuwa na error isipokuwa amevipa viumbe free will na ujuzi wa kutambua baya na jema lakini wanatakiwa na anawataka wafanye mema na yule mwenye kushinda huo mtihani atazawadiwa na aliyeshindwa ataadhibiwa.
Binadamu hatuna free will kama mungu anajua yote yatakayo tokea mbeleni na kingine ww unajuaje una free will
 
Mungu ni baba, kwa maana rahisi ni mzazi, furaha yake ni watoto alioumba, ametuumba kwasababu anafurahia kuwa mzazi, hali kadhalika wewe kuna jambo au hali fulani unayofurahia pale unapoitwa baba ndio maana unatamani kuwa na watoto
Je wewe kama mzazi mwanao akikosea unamuua au unampa adhabu ya milele
 
Kulingana na imani za dini, Mungu alikuwepo, yupo na ataendelea kuwepo (haitaji sababu ya nje ili awepo)

Kama hilo jibu halijitoshelezi kwako, basi inabidi uipinge hiyo imani na kukataa kabisa uwepo wa Mungu.
Mungu yupo ila dini zetu ndio za uongo, uongo mwingi sana kwenye dini zetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…