Kwanini MO Dewji anataka kufunga kiwanda chake cha chai Nchini Tanzania? Bashe amgomea!

Nchi nyingine Viwanda vikisuasua Serikali huingilia kati kuviokoa ili kuokoa Ajira za Wananchi wake.

Shout out to Bashe huyu Jamaa namkubali sana.
 
Viwanda vilivyomshinda kuendesha Ni vile vinavyo saga chai Kama Ambangulu, Dindira huko TANGA na vingine mby na Iringa. Hivi vya chai alivinunua kutoka kwa wazungu.
Viwanda vyake alivyojenda Ni Kama Nicola, Mo energy, Cha ngano na kile Cha mafuta ya alizeti, nimesahau na kile Cha maji ya kunywa.

MeTL Group ina mashamba matatu ya chai katika mikoa miwili tofauti yenye hekta 2,350 za chai iliyopandwa na hekta 1,200 chini ya kilimo cha mkataba kwa wakulima wadogo.

Asilimia 95 ya chai inayozalishwa inauzwa nje ya nchi moja kwa moja au kupitia Mnada wa Mombasa katika nchi jirani ya Kenya, na iliyobaki huuzwa kwa wachanganyaji wa ndani.

Viwanda vipya 3 vya chai vyenye laini 5 za mashine za CTC na laini 1 ya mashine ya chai ya asili yenye uwezo wa kusindika wa kilo 250,000 za majani mabichi kwa siku. Viwanda hivyo ni: Mlima wa Arc na Dindira wilayani Korogwe na Chivanjee wilayani Rungwe. Uzalishaji wa chai ya ubora wa hali ya juu kutoka kwa majani mabichi yaliyovunwa kama inavyopendelewa na wachanganyaji na wapakiaji wengi wakuu kote ulimwenguni wanywaji chai katika viwanda vyetu vitatu, hapo juu.

Chai inayozalishwa katika viwanda hivi hupandwa kwenye udongo wenye madini mengi kwenye mwinuko. Mvua za misimu miwili kwa mwaka hunyesha kwa kipindi cha karibia miezi yote na kuwezesha uzalishaji wa majani mabichi mwaka mzima katika mashamba yetu ya chai.

Zahanati za Kikundi za matibabu zina wafanyikazi wa matibabu waliofunzwa, ambao hutoa huduma ya afya kwa familia za wafanyikazi na jamii za jirani, ambazo zinaishi katika maeneo ya mbali. Mpango wa Mama na Mtoto ni msingi wa utunzaji wa afya ya familia.

Mashamba ya chai huwapa wanawake katika jamii jirani vyanzo salama, visivyobagua, vya mara kwa mara na endelevu vya mapato, pamoja na vituo vya kulelea watoto mchana na shule za msingi kwa watoto wao.

More info :
Tanzania’s largest home-grown company, with a presence in 11 countries in Africa, such as Uganda, Ethiopia Kenya, Rwanda, Burundi, Zambia, Mozambique, Malawi, DR Congo and Tanzania. LG Room Air Conditioners (RAC) External Training – MeTL Group


More info on Tanzanian tea :


View: https://m.youtube.com/watch?v=7Cq1NlwdwjA
 
Zipo taarifa kwamba Serikali ya Tanzania imekataa ombi la Mohamed Dewji la kutaka kufunga kiwanda chake cha chai.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemuomba Bwana Dewji kufanya majadiliano na Serikali kwanza kabla hajachukua uamuzi huo, ambao unatarajiwa kuathiri watu wengi wanaofanya kazi kwenye kiwanda hicho.

Lakini swali letu ni hili, kwanini MO amefikia hatua ya kufunga kiwanda chake alichojenga kwa gharama kubwa na kufunga mitambo ya kisasa? Kuna nini?

Swali jingine ni hili, kwanini jambo hili lishughulikiwe na Wizara ya kilimo badala ya Wizara ya Viwanda?


======

Serikali imegoma kuridhia ombi la kufungwa kwa Kiwanda cha chai cha Mo Enterprises na Viwanda vingine kadhaa Nchini ili kuepusha athari ikiwemo Watu kupoteza ajira.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiwa Dodoma leo, amesema kama Wawekezaji wana changamoto yupo tayari kujadiliana nao ili kuzitatua huku viwanda vikiwa vinaendelea na uzalishaji.

“Nimepokea barua ya kampuni ya Mohamed Enterprise kutaka kufunga Viwanda nimewaambia hawawezi kufunga viwanda, tujadiliane njia nyingine lakini sio kufunga kwasababu kwetu bado sekta ya chai bado ni muhimu kwa ajira za Watu, binafsi naamini nikienda Rungwe kama Wakulima wangekuwa hawana mazao mengine umasikini ungekuwa mkubwa mno kwa hali ya chai ilivyo, Lupembe, Mafinga, Mufindi kote hali ingekuwa mbaya”

“Nimepokea maombi ya MO kuja kwetu Serikali kwamba Serikali tuyachukue mashamba (ili kuyaendeleza) tutaunda Timu itaenda kuyakagua tutaangalia thamani halisi ya wakati huu kwasababu hayakutunzwa vizuri mashamba wala vile Viwanda kwa muda mrefu sana kwahiyo tutaangalia njia zote lakini sekta ya chai itaendelea kuwa hai, nimeagiza hakuna kufunga kiwanda lazima waendeele na uzalishaji hilo ni la lazima kisha tutakaa chini kujadiliana mambo mengine”

“Nawahakikishia ninaendelea na majidiliano na Wizara ya Fedha ili tuwe na njia bora kupima viwango vya tozo, nimeongea na Waziri wa Uwekezaji ili hivi viwanda vipate nafuu ya kodi ya kuagiza nje kwasababu kama tunampa Mtu wa Export sehemu nafuu ya kodi, ukitazama sekta ya chai kwa ujumla bidhaa zake zinahusisha kusafirisha nje”

“Nimekaa na Timu ya Wataalamu imenifanyia uchambuzi wa bei ya majani mabichi ya chai, kwa namba inatakiwa bei ishuke lakini nimewaambia bei ya Mkulima haitoshuka tuta-mantain bei ya mwaka jana” —— amesema Waziri wa Kilimo
Unambembeleza mtu wakati ameshahamia U.A.E. Ninashangaa serikali inahangaika na waarabu na kukopa nje wakati kuna watanzania kibao wanauwezo wa kuwekeza. Kipi bora kumpa mtanzania ambaye anaishi hapa nchni au kumpa mtu wa nje. Tanzania tuna matajiri kibao ambao hata sio maarufu kuanzia Iringa,Niombe, Kahama, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha. Dola haipatikani kwa sababu nchi imeshikiliwa na watu wasio watanzania. Na cha kushangaza wenye mamlaka hawataki kuwapa fursa watanzania.
 
Hapo ni dili inachezwa mkuu
Inawezekana ikawa dili inachezwa, inawezekana isiwe dili.

Ni muhimu kuhakiki na kuandika vitu vyenye ushahidi ili kuepuka speculations zisizo na ushahidi wala uthibitisho. Hizi zipo nyingi sana.

Just because Mo ni mtu wa deal na kashafanya deal huko nyuma, hilo halimaanishi kila anachofanya ni deal.
 
Yes. Morogoro kuna kiwanda Mweshimiwa Rais Aliongea na Wamiliki wake wakarudi na kukifunguwa hicho kiwanda na mpaka sasa kipo kinafanya uzalishaji.
Kuna tofauti kati ya mtu kulazimishwa asifunge kiwanda na serikali kumuomba mtu asifunge kiwanda, wakafanya mazungumzo kiwanda kisifungwe.

Tanzania tofauti hii inaeleweka?
 
MeTL Group ina mashamba matatu ya chai katika mikoa miwili tofauti yenye hekta 2,350 za chai iliyopandwa na hekta 1,200 chini ya kilimo cha mkataba kwa wakulima wadogo.

Asilimia 95 ya chai inayozalishwa inauzwa nje ya nchi moja kwa moja au kupitia Mnada wa Mombasa katika nchi jirani ya Kenya, na iliyobaki huuzwa kwa wachanganyaji wa ndani.

Viwanda vipya 3 vya chai vyenye laini 5 za mashine za CTC na laini 1 ya mashine ya chai ya asili yenye uwezo wa kusindika wa kilo 250,000 za majani mabichi kwa siku. Viwanda hivyo ni: Mlima wa Arc na Dindira wilayani Korogwe na Chivanjee wilayani Rungwe. Uzalishaji wa chai ya ubora wa hali ya juu kutoka kwa majani mabichi yaliyovunwa kama inavyopendelewa na wachanganyaji na wapakiaji wengi wakuu kote ulimwenguni wanywaji chai katika viwanda vyetu vitatu, hapo juu.

Chai inayozalishwa katika viwanda hivi hupandwa kwenye udongo wenye madini mengi kwenye mwinuko. Mvua za misimu miwili kwa mwaka hunyesha kwa kipindi cha karibia miezi yote na kuwezesha uzalishaji wa majani mabichi mwaka mzima katika mashamba yetu ya chai.

Zahanati za Kikundi za matibabu zina wafanyikazi wa matibabu waliofunzwa, ambao hutoa huduma ya afya kwa familia za wafanyikazi na jamii za jirani, ambazo zinaishi katika maeneo ya mbali. Mpango wa Mama na Mtoto ni msingi wa utunzaji wa afya ya familia.

Mashamba ya chai huwapa wanawake katika jamii jirani vyanzo salama, visivyobagua, vya mara kwa mara na endelevu vya mapato, pamoja na vituo vya kulelea watoto mchana na shule za msingi kwa watoto wao.

More info :
Tanzania’s largest home-grown company, with a presence in 11 countries in Africa, such as Uganda, Ethiopia Kenya, Rwanda, Burundi, Zambia, Mozambique, Malawi, DR Congo and Tanzania. LG Room Air Conditioners (RAC) External Training – MeTL Group


More info on Tanzanian tea :


View: https://m.youtube.com/watch?v=7Cq1NlwdwjA

Wewe unajua unachokiongelea mpaka unajua mashine za CTC yaani CURL TEAR & CUT.
Hiki Cha mlima wa Arc ndio Ambangulu ambacho nacho Kiko Korogwe au ni Balangai wilayani Lushoto?
Thanks.
 
Kuna tofauti kati ya mtu kulazimishwa asifunge kiwanda na serikali kumuomba mtu asifunge kiwanda, wakafanya mazungumzo kiwanda kisifungwe.

Tanzania tofauti hii inaeleweka?
Serikali aiwezi lazimisha Mtu ! Ni lazima kuwe na mazungumzo ya pande zotr husika based on win win Sitaution.Kwa hiyo MO atatoa Sababu na Serikali ikazisikiliza na kuja na majibu.Then The Govwrnment can Give MO an Offer Which He cant refuse😁
 
Wafanyabiashara mara zote wanataka kuoperate kwa faida tu.

Hawataki kushare profit kwa namna yeyote ile.
 
Bashe kibaraka katumwa na Mo atishie nyau Ila sio vizuri hilo take waziri Bashe anaharibu kwa hiyo statement kuwa mwekezaji ukiwekeza Tanzania huruhusiwi kufunga biashara serikali itakukomalia.Hiyo statement inatisha wawekezaji

Raisi amuondoe uwaziri

Hakuna mwekezaji anaeogopa kuja Tanzania kwa kauli za waziri. Mwekezaji wa maana anajijuza sheria na sera za biashara wakati anafikiria kuwekeza, na anafunga mikataba. Tumekuwa wahanga wa kudumu wa mikataba, na mpaka juzi kuna kampuni ya gesi imeibembeleza Tanzania ianze mradi haraka maana inanusa harufu ya ulaji kwenye machimbo au mahakamani.

Hatubembelezi wakekezaji, na hatupaswi, not least the Dewji cabal.

Kampuni hii haiwezi kufanya maamuzi kivyakevyake, ina wiwa, ina deni na taifa. Everything from conditioned grants of sisal plantations in Tanga, MUTEX apparel factory in Lake Zone, tea industry in Mbeya and Iringa, and massive swathes of real estate in Lindi, which all belonged to the state, and were used as collateral to secure critical loans to erect the Dewji Conglomerate, this company owes the state. And yes, they breached all the conditions attached to the state assets privation sweetheart deals.

They simply can not make unilateral decisions about the future of the company. Dewji and his son did not singlehandedly build this business behemoth. The state is going to have a say as well.
 
Nchi nyingine Viwanda vikisuasua Serikali huingilia kati kuviokoa ili kuokoa Ajira za Wananchi wake.

Shout out to Bashe huyu Jamaa namkubali sana.
Kwamba Viwanda vya Private visipopata faida Serikali inaingilia kuviokoa kwa kutumia pesa ya mlipa Kodi vikipata faida mlipa Kodi kivyake....!!

Na hilo unaona ni sustainable ? Kwanini from day one hivi viwanda taasisi ambazo ni nguzo ya Taifa na UMMA serikali isiwe na kiwanda chao na Private pia vya kwao wote wapambane kwenye Soko..... ?

Na kama hailipi kwanini tusifanye vitu ambavyo vinalipa kulingana na advantages tulizonazo.... (Na kwanini isilipe iwapo tunalima Chai na wanywaji wa Chai) ?

It is the maxim of a every prudent master of a family, never to attempt to make at home what it will cost him more to make than to buy. The taylor does not attempt to make his own shoes, but buys them of the shoemaker. The shoemaker does not attempt to make his own cloths, but employs a tailor.
 
Serikali aiwezi lazimisha Mtu ! Ni lazima kuwe na mazungumzo ya pande zotr husika based on win win Sitaution.Kwa hiyo MO atatoa Sababu na Serikali ikazisikiliza na kuja na majibu.Then The Govwrnment can Give MO an Offer Which He cant refuse😁
Serikali kuanza ku negotiate na Mo tayari inaonesha uchumi mbovu.

Katika uchumi mzuri ilitakiwa Mo hata kama hataki kufanya biashara, kabla hajaamua kufunga kuwe na wafanyabiashara kibao wanaomsumbua wakitaka kununua biashara yake.

Mo angeweza kuuza biashara watu wengine waendelee na uzalishaji, hata kama yeye hataki kufanya biashara.

Sasa hivi serikali kuanza kumbembeleza Mo asifunge biashara ni kama vile hakuna mtu mwingine yeyote anayeitaka biashara hiyo.
 
MO angeuza tu kiwanda kama labda hapati faida. Hana haja ya kukifunga coz economically wananchi watauza wapi chai yao?
Haya mambo ya kuuza Chai kuna Ukiritimba wa hali ya Juu..., Jaribu ku-export chai utasikia utitiri wa vibali yaani kuna Bodi ya Chai na yenyewe lazima uwasiliane nao ni balaa bin balaa katika hii songombingo yote mkulima sio mfaidika....., kwahio hata hio Chai akiuza Bongo ni kwa bei ya kutupa..., akitaka apeleke nje atapewa utitiri wa vibali itabidi ashindwe kabla hajaanza

Cheki hapo chini steps 38
Obtain tea processing licence (8)expand_less
1Register and apply for licence
language
2Obtain payment control number

3Pay for tea processing licence

4Obtain TBT receipt

5Obtain provisional green leaf processing licence
language
6Inspection of premise

7Inspection for quality end product

8Obtain green tea processing licence
language
Obtain green leaf tea buying licence (2)expand_less
9Register and apply for licence
language
10Obtain green leaf tea buying licence
language
Obtain tea export permit (2)expand_less
11Register and apply for tea export permit
language
12Obtain tea export permit
language
Obtain certificate of radioactivity analysis (4)expand_less
13Apply for certificate of radioactivity analysis
language
14Pay and obtain sample label
language
15Submit samples

16Obtain certificate of radioactivity analysis
language
Pre-clearance documentation (3)expand_less
17Contract a clearing agent

Obtain TRA assessment documentOPTIONAL
language
18Book shipping space with shipping line

Obtain phytosanitary certificate (4)expand_less
19Register and apply for certificate
language
20Pay fees
language
21Consignment inspection

22Obtain phytosanitary certificate

Obtain EAC certificate of origin (5)expand_less
23Obtain online user credentials
language
24Verification of goods

25Apply for certificate of origin
language
26Pay certificate fees
language
27Obtain certificate of origin

Custom declaration (2)expand_less
28Lodge custom documents (TRA)
language
29Obtain Tanzania Single Administrative Document (TANSAD)
language
Consignment inspection (2)expand_less
30Request for consignment inspection

31Consignment inspection and stuffing

Obtain TRA release order (2)expand_less
32Submit stamped documents
language
33Obtain release order

Port clearance (5)expand_less
34Lodge cargo clearance documents (TPA)
language
35Pay port charges

36Create truck or driver announcement
language
37Obtain gate in ticket

38Obtain gate out permission
 
Kwamba Viwanda vya Private visipopata faida Serikali inaingilia kuviokoa kwa kutumia pesa ya mlipa Kodi vikipata faida m
Sio Financial tu Serikali inaweza kuvipunguzia Ushindani kwa kuvilinda na Bidhaa zilizoruzukiwa kutokea Nje kwa mfano Chai kutoka Kenya na Uganda inayoingia kiholela kwa njia za Panya kuongeza Kodi kwenye Chai inayotoka nje nk.
 
Kwa hiyo mtu anaweza kulazimishwa kuendesha viwanda hata kama yeye anataka kufunga viwanda vyake?
Sababu ni ajira alizozitengeneza lakini pia mapato Kwa maana ya Kodi.
Hata hivyo inaweza kuwa ni sindicate ya kuongeza bei ya bidhaa kwa visingizio vya mwenye kiwanda.
 
Back
Top Bottom