Kwanini MO Dewji anataka kufunga kiwanda chake cha chai Nchini Tanzania? Bashe amgomea!

Ukienda kuwauliza raia wa kawaida pale Marekani hii kitu "Bailout" hawaipendi na hawataki kuisikia , na ni kwasababu wanajua mwisho wa siku anayefaidika si raia wa kawaida ,ni sawa na kumkamua masikini ili kumfaidisha tajiri ,kitu ambacho si sustainable kwenye uchumi na kinazalisha mentality ya uzembe na kuua ubunifu ,maana huyo anayepewa Bailout kila siku atakuwa anatapanya resources ovyo ovyo na kuongoza biashara ovyo akijua kuna kodi za wananchi zitatumika kuja kuokoa biashara yake akikwama .
Mo aachwe afanye maamuzi anayoona yanafaa
 
Kwani MO hicho kiwanda cha chai alijenga yeye ? Na mashamba je ?? vyote alinunua bei chee toka serikanli wakati wa ubinafsishaji wa serikali ya awamu ya tatu.Arudishe serikalini wala asimtishe mtu !!
 
Kwangu Bailout ni mentality ya kijamaa na kijima na haifai kwa ulimwengu huu wa competition na utandawazi na mifumo ya kipebari
 
Mohammed Dewji anataka kuwanyonya wakulima.

Kuna jamaa yangu kutoka nchi fulani iliyoendelea (kiufupi nahisi ni jasusi) alikuja kufanyakazi METL kwa miaka kadhaa. Ameondoka nchini na full picture ya Mo Dewji dhidi ya mifumo ya uchumi wa Tanzania. Pia hata ukaguzi wa mali inayoenda kwa walaji hufanyika in favor kwa sababu ya uduni wa viwango vya uzalishaji....

Hawa matajiri, wanaonekana kwenye Forbes kama leading moguls lakini ukija kwenye eneo la kulipa kodi hayupo kwenye top margins.

Mengine siandiki kwa sababu mfumo wanajua mengi sana na sijui ukimya wao kama ni tafsiri ya wanufaika wenza
Duuuuuu
 
Zipo taarifa kwamba Serikali ya Tanzania imekataa ombi la Mohamed Dewji la kutaka kufunga kiwanda chake cha chai.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemuomba Bwana Dewji kufanya majadiliano na Serikali kwanza kabla hajachukua uamuzi huo, ambao unatarajiwa kuathiri watu wengi wanaofanya kazi kwenye kiwanda hicho.

Lakini swali letu ni hili, kwanini MO amefikia hatua ya kufunga kiwanda chake alichojenga kwa gharama kubwa na kufunga mitambo ya kisasa? Kuna nini?

Swali jingine ni hili, kwanini jambo hili lishughulikiwe na Wizara ya kilimo badala ya Wizara ya Viwanda?


======

Serikali imegoma kuridhia ombi la kufungwa kwa Kiwanda cha chai cha Mo Enterprises na Viwanda vingine kadhaa Nchini ili kuepusha athari ikiwemo Watu kupoteza ajira.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiwa Dodoma leo, amesema kama Wawekezaji wana changamoto yupo tayari kujadiliana nao ili kuzitatua huku viwanda vikiwa vinaendelea na uzalishaji.

“Nimepokea barua ya kampuni ya Mohamed Enterprise kutaka kufunga Viwanda nimewaambia hawawezi kufunga viwanda, tujadiliane njia nyingine lakini sio kufunga kwasababu kwetu bado sekta ya chai bado ni muhimu kwa ajira za Watu, binafsi naamini nikienda Rungwe kama Wakulima wangekuwa hawana mazao mengine umasikini ungekuwa mkubwa mno kwa hali ya chai ilivyo, Lupembe, Mafinga, Mufindi kote hali ingekuwa mbaya”

“Nimepokea maombi ya MO kuja kwetu Serikali kwamba Serikali tuyachukue mashamba (ili kuyaendeleza) tutaunda Timu itaenda kuyakagua tutaangalia thamani halisi ya wakati huu kwasababu hayakutunzwa vizuri mashamba wala vile Viwanda kwa muda mrefu sana kwahiyo tutaangalia njia zote lakini sekta ya chai itaendelea kuwa hai, nimeagiza hakuna kufunga kiwanda lazima waendeele na uzalishaji hilo ni la lazima kisha tutakaa chini kujadiliana mambo mengine”

“Nawahakikishia ninaendelea na majidiliano na Wizara ya Fedha ili tuwe na njia bora kupima viwango vya tozo, nimeongea na Waziri wa Uwekezaji ili hivi viwanda vipate nafuu ya kodi ya kuagiza nje kwasababu kama tunampa Mtu wa Export sehemu nafuu ya kodi, ukitazama sekta ya chai kwa ujumla bidhaa zake zinahusisha kusafirisha nje”

“Nimekaa na Timu ya Wataalamu imenifanyia uchambuzi wa bei ya majani mabichi ya chai, kwa namba inatakiwa bei ishuke lakini nimewaambia bei ya Mkulima haitoshuka tuta-mantain bei ya mwaka jana” —— amesema Waziri wa Kilimo
Upunguani,Bashe ndio Huwa anampa pesa za Kuendesha kiwanda?

Kama anapata hasara Kwa nini asifunge?
 
Mimi chuo hata sijasoma uchumi , Ila basic commerce studies za olevel tu zilinipa ideas kamili za jinsi economic wheel inavyofanya kazi , cha kushangaza kuna wapumbavu wameajiriwa humo kwenye wizara za viwanda , biashara na uchumi ili kufanya analysis na kutoa maamuzi ya vitu kama hivi ila ni vululu vululu .
Hii nchi ni failure kabisa ,na mpaka siku tutakapotatua tatizo Tulilo nalo ndio tutaanza kuona mwanga , ni aibu kila kitu mpaka Rais ahusishwe .
Yaani ni kama kwamba hao maamuma waliajiriwa kama mawaziri na watendaji wengine humo kwenye wizara na taasisi hawana akili timamu ya kutengeneza mifumo imara ya utendaji na kufanya implementations na kuhakikisha uchumi wa hii nchi unathrive , ni aibu kabisa
 
Haya mambo ya kuuza Chai kuna Ukiritimba wa hali ya Juu..., Jaribu ku-export chai utasikia utitiri wa vibali yaani kuna Bodi ya Chai na yenyewe lazima uwasiliane nao ni balaa bin balaa katika hii songombingo yote mkulima sio mfaidika....., kwahio hata hio Chai akiuza Bongo ni kwa bei ya kutupa..., akitaka apeleke nje atapewa utitiri wa vibali itabidi ashindwe kabla hajaanza

Cheki hapo chini steps 38
Duh , mlolongo wa ukiritimba balaa
 
Kulinda ajira hata 3 ni Jambo jema.
At what cost ? Kulinda ajira za Makuli sita kwa kusababisha walaji milioni kadhaa kulipia bidhaa hafifu kwa gharama ya juu ?

Tunasema serikali isiingilie (kutokuwa na viwanda vya UMMA - vyote tubinafishe) alafu tunaowapa hatuishii hapo tunakikishe hawapati competition kwa kuzuia bidhaa nyingine..., Unaona hii ina-make sense ?

Kwanini hao private wasilete vya kwao na jamii / UMMA na yenyewe iwe na vya kwao hususan kwenye hizi Cash Crops...
 
Kwani MO hicho kiwanda cha chai alijenga yeye ? Na mashamba je ?? vyote alinunua bei chee toka serikanli wakati wa ubinafsishaji wa serikali ya awamu ya tatu.Arudishe serikalini wala asimtishe mtu !!
"Arudishe serikalini" maana yake nini?

Auze viwanda serikalini? Kwa bei gani? Serikali itakubali kununua kwa bei atakayoitaka baada ya yeye kukaa navyo kwa muda wote huu?

Serikali imeuza viwanda kwa kujitoa kwenye biashara, Mo arudishe viwanda serikalini ili iweje? Serikali irudi kwenye biashara?

Ikiwa serikali ilijitoa kwenye biashara mpaka kuuza viwanda, Kwa nini unataka Mo arudishe viwanda serikalini, asiviuze kwa wafanyabiashara wengine?
 
Kwamba Viwanda vya Private visipopata faida Serikali inaingilia kuviokoa kwa kutumia pesa ya mlipa Kodi vikipata faida mlipa Kodi kivyake....!!

Na hilo unaona ni sustainable ? Kwanini from day one hivi viwanda taasisi ambazo ni nguzo ya Taifa na UMMA serikali isiwe na kiwanda chao na Private pia vya kwao wote wapambane kwenye Soko..... ?

Na kama hailipi kwanini tusifanye vitu ambavyo vinalipa kulingana na advantages tulizonazo.... (Na kwanini isilipe iwapo tunalima Chai na wanywaji wa Chai) ?

It is the maxim of a every prudent master of a family, never to attempt to make at home what it will cost him more to make than to buy. The taylor does not attempt to make his own shoes, but buys them of the shoemaker. The shoemaker does not attempt to make his own cloths, but employs a tailor.
Huenda pamoja na kuwa na wataalamu wa uchumi na biashara kwenye hizo wizara ,Bongo zao hazijajua campetative advantage tuliyonao kama taifa ( yaani sisi ni mabingwa wa kuzalisha nini kwa ufanisi na bei cheap ambacho kinaweza kuliwa na mataifa mengine na mwisho wa siku kuleta faida na tija kwa mwananchi na taifa kwa ujumla ) , hapo ndipo tulipo kwama .
Tunakimbilia viwanda ,wakati wizara zetu na taasisi ni so poor kwenye kudeliver utendaji na kuhudumia miundombinu , na miundombinu yenyewe au kodi na mazingira ya biashara ni so poor .
Tunatakiwa tujiulize maswali magumu kama taifa na tufanye maamuzi
 
Mengi hakuwahi kuwaweka Watanzania-wakulima-Rehani. Nipo tayari kusahihishwa

Ni hivyo tu.
Mfanyabiashara yupo answerable kwa shareholder wake (profit) ndio alpha na omega... hio sio charity wala sio kazi yake kuangalia Welfare ya wakulima Hio sio kazi yake ni kazi ya watumishi wetu na watunga sera tunaowalipa (serikali)

Tukirudi kwa Mengi zunguka kwenye Media zake na pengine ni wangapi wanadai mishahara (sio kwamba nalaumu Kampuni sio Mengi hivyo kama Kampuni haizalishi sitegemei Mengi atoe pocket money yake kufidia biashara) i.e. Throwing Good Money after Bad...
 
Ndo maana tunasema kuwa CCM ikae pembeni waje wanasiasa wenye moyo wa kuikwamua nchi. Kuna mengi sana yanayosababisha CCM ing'ang'anie madarakani ikiwemo namna inavyowekeza indirectly kwa hawa mnaowaona ni matajiri wa kutisha leo.

Unakumbuka issue ya Deep Green na ile kampuni ya Uwakili?

Tanzania ni zaidi ya CCM na mamlaka zote za nchi. Tanzania ni watu na Katiba bora
 
Inawezekana ikawa dili inachezwa, inawezekana isiwe dili.

Ni muhimu kuhakiki na kuandika vitu vyenye ushahidi ili kuepuka speculations zisizo na ushahidi wala uthibitisho. Hizi zipo nyingi sana.

Just because Mo ni mtu wa deal na kashafanya deal huko nyuma, hilo halimaanishi kila anachofanya ni deal.
Subiri utaona jibu
 
Zipo taarifa kwamba Serikali ya Tanzania imekataa ombi la Mohamed Dewji la kutaka kufunga kiwanda chake cha chai.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemuomba Bwana Dewji kufanya majadiliano na Serikali kwanza kabla hajachukua uamuzi huo, ambao unatarajiwa kuathiri watu wengi wanaofanya kazi kwenye kiwanda hicho.

Lakini swali letu ni hili, kwanini MO amefikia hatua ya kufunga kiwanda chake alichojenga kwa gharama kubwa na kufunga mitambo ya kisasa? Kuna nini?

Swali jingine ni hili, kwanini jambo hili lishughulikiwe na Wizara ya kilimo badala ya Wizara ya Viwanda?


======

Serikali imegoma kuridhia ombi la kufungwa kwa Kiwanda cha chai cha Mo Enterprises na Viwanda vingine kadhaa Nchini ili kuepusha athari ikiwemo Watu kupoteza ajira.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akiwa Dodoma leo, amesema kama Wawekezaji wana changamoto yupo tayari kujadiliana nao ili kuzitatua huku viwanda vikiwa vinaendelea na uzalishaji.

“Nimepokea barua ya kampuni ya Mohamed Enterprise kutaka kufunga Viwanda nimewaambia hawawezi kufunga viwanda, tujadiliane njia nyingine lakini sio kufunga kwasababu kwetu bado sekta ya chai bado ni muhimu kwa ajira za Watu, binafsi naamini nikienda Rungwe kama Wakulima wangekuwa hawana mazao mengine umasikini ungekuwa mkubwa mno kwa hali ya chai ilivyo, Lupembe, Mafinga, Mufindi kote hali ingekuwa mbaya”

“Nimepokea maombi ya MO kuja kwetu Serikali kwamba Serikali tuyachukue mashamba (ili kuyaendeleza) tutaunda Timu itaenda kuyakagua tutaangalia thamani halisi ya wakati huu kwasababu hayakutunzwa vizuri mashamba wala vile Viwanda kwa muda mrefu sana kwahiyo tutaangalia njia zote lakini sekta ya chai itaendelea kuwa hai, nimeagiza hakuna kufunga kiwanda lazima waendeele na uzalishaji hilo ni la lazima kisha tutakaa chini kujadiliana mambo mengine”

“Nawahakikishia ninaendelea na majidiliano na Wizara ya Fedha ili tuwe na njia bora kupima viwango vya tozo, nimeongea na Waziri wa Uwekezaji ili hivi viwanda vipate nafuu ya kodi ya kuagiza nje kwasababu kama tunampa Mtu wa Export sehemu nafuu ya kodi, ukitazama sekta ya chai kwa ujumla bidhaa zake zinahusisha kusafirisha nje”

“Nimekaa na Timu ya Wataalamu imenifanyia uchambuzi wa bei ya majani mabichi ya chai, kwa namba inatakiwa bei ishuke lakini nimewaambia bei ya Mkulima haitoshuka tuta-mantain bei ya mwaka jana” —— amesema Waziri wa Kilimo
Na hapo mtamsingizia Magufuli? Na Bado mengi yanakuja
 
Back
Top Bottom