Kwanini miji ya Africa mingi ipo disorganised?

Kwanini miji ya Africa mingi ipo disorganised?

Kila mtu anajua tatizo, watendaji wetu wakuu wa serikali zetu huku Afrika wapo kwa maslahi yao binafsi. Wote ni watu wenye tamaa ya kujitajirisha au kuwa na unafuu wa maisha kupitia pesa za umma. We fikiria kuna wabunge wangapi nchi hii? Kila mmoja anapewa gari ya maelfu ya dola kila baada ya miaka 5, wanalipana pesa za posho kodi yenyewe yote inayokusanywa ya kujengea mambo muhimu itapatikana wapi? Hizo nchi za wazungu walioendelea hata waziri akitaka gari anunue kwa pesa yake hakuna ujinga. Huu ni umasikini wa kujitakia, msiulizage majibu kama watoto wadogo
City planing kwa kiasi kikubwa inatuhusu sisi wananchi sema ni vile vipato vyeti vidogo Tanga, Dodoma na Moshi ni miji iliyojengwa kwa mipango miji ila shida inakuja unakiwanja unaambiwa unapaswa kujenga hivi kulingana na eneo kiwanja chako kipo je unaweza? Sometimes it's displine tu
 
City planing kwa kiasi kikubwa inatuhusu sisi wananchi sema ni vile vipato vyeti vidogo Tanga, Dodoma na Moshi ni miji iliyojengwa kwa mipango miji ila shida inakuja unakiwanja unaambiwa unapaswa kujenga hivi kulingana na eneo kiwanja chako kipo je unaweza? Sometimes it's displine tu

Tuwape mikopo, viwango.
 
Bora umeliona hili, ukitaka kujua hatuna utaratibu nenda makaburini. Kila mtu anazika anavyojiskia kichwa kinaangalia popote.
Hakuna cha kwamba huu mstari ukijaa unafata huu, hata kama makaburi ni ya dini zote.
Siku ambayo nilijua kwamba hatuko serious ni siku ambayo makamu wa raisi Mpango alimuagiza mkurugenzi wa Jiji Dodoma atoe uchafu, sijui ilikuwa mtaa gani, ambayo una muda mrefu hadi wananchi wanalalamika.
Duh, halafu na Dodoma, michanga imeingia sana barabarani. Inapoteza mvuto wa barabara, zinawahi kupauka
 
Wakuu leo nimeona nilete mada mezani. Kwa nini miji yetu mingi ipo disorganised ukifananisha na wenzetu?
Ukiangalia miji ya nchi za mambele utaona imepangiliwa, misafi, wamepanda miti mingi, haipo chaotic ni miji inayovutia

Mfano angalia mji wa Seattle, Marekani
View attachment 3514771
View attachment 3514773View attachment 3514774

Lakini ukiangalia Africa miji yetu utaona hatujapanda miti, hakuna pavements, michanga imeingia barabarani, ni michafu yani kila kitu kipo disorganised.
Angalia mji wa Lagos, Nigeria
View attachment 3514772
View attachment 3514775

Hapa naleta na picha, mfano wa miji ya mambele halafu tuone.

Paris
View attachment 3514779
View attachment 3514780
.

Tokyo
View attachment 3514777
View attachment 3514778
.

Amsterdam
View attachment 3514776

Halafu hapa naonesha jinsi miji mingi ya Africa ilivyo

Hii picha ni Eastleigh, Nairobi
View attachment 3514781

Hapa ni Pipeline, Nairobi
View attachment 3514782

Hapa ni Paje, Zanzibar
View attachment 3514783

Hapa ni Kampala, Uganda
View attachment 3514784

Kuna watu wanasema sababu ni umasikini. Mimi nakataa. Mbona Rwanda ni nchi masikini lakini miji yao ipo organised sana.
Nakuonesha picha za Kigali, Rwanda. Zipo tofauti kabisa na miji mingine ya Africa
Iangalie Kigali
View attachment 3514786View attachment 3514787View attachment 3514788View attachment 3514789View attachment 3514790View attachment 3514791View attachment 3514792

Sababu ni nini? Kwa nini miji mingine ya Africa isiwe kama Kigali? Au kwa nini isiwe kama miji ya mambele?

NB: Najua kuwa hata miji ya Africa kama Nairobi, Kampala na Lagos ina maeneo ambayo yapo well organised na masafi, lakini ni machache mno ukifananisha na maeneo machafu ambayo hayajapangiliwa vizuri
Utakuaje na mji organized wakati hata tabia na fikra zinategemea social media na wazungu?

Hatuna agenda zaidi ya ulalamishi na kukosoa tu

Hata hii mada… thr best would be, how can we make our cities better and more organized?
 
Utakuaje na mji organized wakati hata tabia na fikra zinategemea social media na wazungu?

Hatuna agenda zaidi ya ulalamishi na kukosoa tu

Hata hii mada… thr best would be, how can we make our cities better and more organized?
Hapana, sio lazima mada iwe hivyo unavyotaka wewe. Hata mada kuwa hivi ni sawa, lazima niulize sababu kwanza kwa wadau wa JF kabla ya kuanza kufikiria suluhisho
Na pia sio kweli kwamba kutumia social media za kizungu ndio kunafanya miji yetu iwe disorganised. Japan na South Korea wanatumia media za kizungu lakini bado nchi zao ni safi na zipo organised
 
Utakuaje na mji organized wakati hata tabia na fikra zinategemea social media na wazungu?

Hatuna agenda zaidi ya ulalamishi na kukosoa tu

Hata hii mada… thr best would be, how can we make our cities better and more organized?
Viongozi wanaweza kuchukua idea nzuri na kuzifanyia kazi kupitia media zozote. Unawafikiaje kuongea nao?
 
Utakuaje na mji organized wakati hata tabia na fikra zinategemea social media na wazungu?

Hatuna agenda zaidi ya ulalamishi na kukosoa tu

Hata hii mada… thr best would be, how can we make our cities better and more organized?
Na pia hii mada nimeamua tu iwe ya kuuliza, nipate maoni ya watu juu ya hili suala
Lakini sio kwamba thread zote naandika kuuliza na kukosoa. Kuna hii thread hapa niliandika kila ninachohisi ni solution kwa kilimo nchini Tanzania. So sio kwamba always nakosoa tu. Huwa natoa idea zangu pia
 
SHIDA ni viongozi wa Africa.
Mfano hapa kwetu Tz, ccm ni changamoto yetu kubwa kuliko changamoto nyingine zote.
Sio kwamba plan nzuri zinakuwaga hazipo, ila hawawez tekeleza jambo bila kupata chao Cha kuweka mfukoni, kama chao hamna au ni kidgo sana wanaua mradi. Mfano mdgo ni Ile karakana ya mwendo Kasi pale jangwani, wakati panajengwa, ata chizi alikuwa anashangaa mbona hapa Kuna shda sana ya maji, tukajua basi labda watazingatia Hilo, matokeo yake wakajenga majengo Yao kama kawaida, baadae wakapatelekeza.

Ukiangalia hospitali nyingi hz wanaziita za wilaya, Yani kwa mbali utasema ni majengo ya vyoo. Yaan hawajali ufanisi, viongozi wetu wengi wanawaza ngono.
 
Nchi ambazo kwa sehemu kubwa ya miji yao wamaefanikiwa kiasi kikubwa kupanga miji.ni Algeria. Morroco. Tunisia. Egypt japo citu centres zingine zinatisha.sana hasa low income earners. South Arica. NAMIBIA. BOTSWANA ZIMBABWE.

Shida kubwa ya waafrika ni ufisadi na kutofuata utaalamu. Mfano oysterbay. Masaki. Msasani penidular haikutakiwa kuwe na kibanda hata kimoja kilichozidi kwenye road reserve lakini alipokufa magufuli mambo yalilipuka kama bomu kila sehemu baa na wauza chakula. Massage na.saloon.

Eneo kama Kawe ilitakiwa libomolewe lote lipangwe upya pangependeza sana.

Kuna nchi hapa afrika hakuna bodaboda wala bajaji nao wanachafua sana miji. Mfano zimbabwe hakuna huo ujinga wa pikipiki za mchina.

Eneo kama Goba sijui tulifeli wapi kulipanga lingevutia zaidi uwekezaji
 
Hakuna changes if we depend on viongozi tu

It starts in thr households
All ideas starts from somewhere, Kwenye watu wa chini. Ndio asilimia 95% ta wananchi. Tambua hivyo.

Viongozi wenye akili wanachukua hizo idea, wanazifanyia kazi.
 
All ideas starts from somewhere, Kwenye watu wa chini. Ndio asilimia 95% ta wananchi. Tambua hivyo.

Viongozi wenye akili wanachukua hizo idea, wanazifanyia kazi.
It starts chini na siyo juu

Anzeni hata mtaani tu
 
It starts chini na siyo juu

Anzeni hata mtaani tu
Ni ngumu mkuu, kwa nchi kama Tanzania lazima ianze juu. Fikiria tuliweza vipi kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki? Ilianza juu hadi ikafika chini

1. USAFI
Serikali inapaswa kuweka dustbins nyingi kwenye kila mji, waweke na CCTV cameras, police nk ili kukamata watakaokuwa wanatupa uchafu hovyo. Pia warudishe Jumamosi ya mwisho wa mwezi iwe siku ya usafi. Mtu atakayetupa chupa, au karatasi au vocha nk mtaani alipishwe faini Tsh 50,000/=. Mitaro yetu ifunikwe, isiachwe wazi. Mitaro ikiwa wazi inavutia watu kutupia uchafu na inaleta mwonekano mbaya kwenye miji. Badala yake watu watupe takataka kwenye dustbin za miji. Maeneo yota yaliyochafuliwa beyond repair, yasafishwe yote kwanza kabla hizi sheria hazijawa implemented
Usafi unapaswa ulazimishwe mpaka uje kuwa habit na uzoeleke kwenye jamii

2. MPANGOMJI
Hatuwezi kubomoa nyumba za watu kisa hazina mpangilio ila tunaweza kuzuia ujenzi holela usiendelee
Viwanja vipimwe kuwe na sheria za ujenzi. Mtu apate kibali kwa wataalamu kabla ya kujenga ili wamwelekeze ajenge vipo nyumba yake, iangalie wapi nk
Mitaa inayojengwa kwa kasi yani mitaa chipukizi, serikali inapaswa kuchonga barabara haraka sana. Sio lazima waweke lami, wachonge tu ili wanancho wanaojenga wajue mipaka yao ipo wapi na kuhakikisha kila nyumba inayojengwa ifikiwe kirahisi na gari

3. MCHANGA BARABARANI
Barabara zetu ziwekwe pavements pembeni na miti ipandwe pembezoni ili kupunguza vumbi na mchanga kuja kuingia kwenye lami. Michanga inaharibu sana mwonekano wa barabara zetu, inatupa shida, kila mara tunakuja kurepair barabara, maana zinafukiwa na mchanga maeneo mengi

4. UZURI WA MIJI
Tupande miti mingi, tuwe na gardens kwenye miji na neighbourhoods za watu, tupande nyasi kwenye neighbourhoods na mitaani, tuanzishe Green parks, na maeneo ya kutembelea kama Forodhani, Zanzibar ili kupendezesha miji yetu
 
RUSHWA , RUSHWA, RUSHWA, na pia ELIMU YA KUKARIRI TULIYOLETEWA NA WAKOLONI ......
Watu wa mipango miji huku Africa wanaweza kukosolewa hata na mwanakijiji wa darasa la saba
Pita mijini uone wanavyo ruhuru vituo vya mafuta kujengwa maeneo unaona kabsa hayafai... Wanaruhusu magorofa yanajengwa barabarani mijini hivyo barabara hazitaweza kupanuliwa tena......ambapo ni dalili ya Rushwa na kujiwazia wao wenyewe (baba mama na watoto)

Lakini pia, kukosa Creativity kwa sababu ya Elimu tuliyosoma ya kukariri badala ya elimu ya kutumia akili.
Huku Africa hata aliyesoma akafika ngazi ya juu kabisa...analilia kuajiriwa kwa sababu alichosoma ni kukariri tuuu....na sio kutumia akili kujikwamua....
 
City planing kwa kiasi kikubwa inatuhusu sisi wananchi sema ni vile vipato vyeti vidogo Tanga, Dodoma na Moshi ni miji iliyojengwa kwa mipango miji ila shida inakuja unakiwanja unaambiwa unapaswa kujenga hivi kulingana na eneo kiwanja chako kipo je unaweza? Sometimes it's displine tu

Bro mwananchi wajibu wake ni kufanyakazi na kulipa kodi, sio kujenga miji. Ukisema city planning hii inahusu na mifumo ya majitaka vilevile. Miji yetu ni mibovu kwasababu viongozi hawawajibiki wao ni kula tu
 
Ulaya kila kilomita mbili tatu kuna parks, gardens.

Nyumba nyingi zina gardens usipo maintain bustani yako majani yakakuwa sana bila mpangilio wanapewa onyo, ikijirudia Mara nyingi unapewa faini, council, serikali ya jiji inakuja na kufanya usafi.
Wenzetu wapo vizuri sana kwenye hilo, mi najiuliza hivi ni kweli hakuna kiongozi anayetamani Tanzania nayo iwe hivyo?
Wenzetu wana green parks nyingi, public spaces za kutosha, wamepanda miti mingi eneo la mjini, wamepanda nyasi nyingi, garden za kutosha, pavements, wana maintain usafi, yani ukiwa mjini kuna ile mixture ya maghorofa na ukijani, inavutia sana. Sisi miji yetu hatujali kabisa kuipendezesha na kuitunza iwe misafi. Ndio maana haina mvuto
Angalia jiji la Kigali, Rwanda kwa mfano, hata sio nchi tajiri, lakini wamezingatia upandaji miti, mpangomji, usafi, upandaji wa nyasi, kuweka pavements mitaani nk. Tanzania tunapaswa kujifunza kwa Rwanda
Yani Kigali ina over 1 million people lakini lipo well maintained, sisi hata mji wenye watu laki 2 tu unakuta ni mchafu hatari
 
Back
Top Bottom