Kwanini miji ya Africa mingi ipo disorganised?

Kwanini miji ya Africa mingi ipo disorganised?

Bora umeliona hili, ukitaka kujua hatuna utaratibu nenda makaburini. Kila mtu anazika anavyojiskia kichwa kinaangalia popote.
Hakuna cha kwamba huu mstari ukijaa unafata huu, hata kama makaburi ni ya dini zote.
Siku ambayo nilijua kwamba hatuko serious ni siku ambayo makamu wa raisi Mpango alimuagiza mkurugenzi wa Jiji Dodoma atoe uchafu, sijui ilikuwa mtaa gani, ambayo una muda mrefu hadi wananchi wanalalamika.
 
Malezi ni sifuri, hatufundishwi kuwajibika Angali wadogo. Kuwajibika kwetu ni msamiati Tu usio na maana...Malezi ndiyo Kila kitu, ukiangalia huo mfano wa Rwanda, wanyarwanda ambao nawafahamu mm ni wasafi halafu vitu viko kwenye mpangilio wenye unafuu kuliko Sisi, yaani kwenye standard za usafi wametuacha hata Kwa level ya mtu mmoja mmoja.

Hata upite na bunduki mtaani kutishia watupa taka bado Tu kuna watu watatupa.

nakumbuka miaka Fulani kule Tanga walikuwa na kampeni ya usafi inaitwa Kalembo day, yaani Hadi hiyo siku ifike ndo watu wanakimbizana kwenye usafi wakati ni Jambo linalotakiwa kufanywa Kwa Kila siku, njoo kwenye nyumba zetu ndo utajua Sisi ni mapimbi wenye miguu miwili nyumba ziko hovyo hovyo, mtu akiamka shuka hatandiki vizuri, shuka chafu, chumba hakifagiliwi, bukta na chupi zipo dirishani, vitana na mafuta yako uvunguni yaani Kila kitu hakipo mahali pale, nenda vyooni sasa hizo harufu na uchafu kwenye masink, sasa watu wa Aina hii watakuelewa kweli unapowaambia masuala ya usafi na mpangilio, tena mijini watu hutoa pesa za usafi lakini wapi watendaji wanakula buyu Tu wanapita kushoto.

Kuna jamii Hapa TZ ukiingia nyumba zao zinapendeza hata kama uchumi si mkubwa mfano Mabohora, hawa Jamaa Kila kitu huwa kinakaa sehemu Yake sasa ukiwa na jamii kama hii ni rahisi Sana kukuta mazingira safi, ww Angalia maeneo mengi tuliyojazana sisi waafrika weusi pako hovyo hovyo Tu, Malezi ni muhimu Sana.

Mtu kanunua bidhaa anakula anatupa Ganda au plastiki barabarani au unakuta anatupa dirishani wala hajali, mtu anakamua kamasi anajifutia na nguo Yake. Umaskini si Tatizo pekee Bali Malezi yetu mabovu, tunazaliwa ili kujaza dunia Tu.
 
Sio tu uchafu, na mpangomji pia naongelea
Mfano hapa ni Ibadan, Nigeria. Angalia jinsi mji ulivyo hauna mpangilio
View attachment 3514815
Nimekulewa. Ishu Bado tuna vipaumbele vingi vinatugharimu. Hatuwezi kufocus huko ikiwa Kuna mamb mengi ya msingi hatujatayakamalisha. Mf tu maji, umeme, wenzetu huku walishatoka ndomana hata ishu ya mipangilio ya miji si tatizo
 
Pia nimesema miji yetu haipo well planned
Yani mpango mji hatuzingatii, mfano nipo huku Mbeya, lakini kuna ujenzi holela sana. Watu wanajenga bila mpangilio matokeo yake mwonekano unakuwa mbaya.
Miji yetu ipo disorganised, kwa namna hiyo yani

Kuna uzi uliikandia sana Mbeya mkuu, nadhani uzi ulikuwa ni comparison kati ya uswahilini ya mikoani na Dar. Hapo tatizo ni mipango miji na ongezeko la watu especially maeneo ya low income earners. Kwa mfano makazi ya watu wa Uzunguni, Uhindini, New Forest au Block T, huwezi linganisha na Ilolo, Sinde au Makunguru/ Jua kali.

Nikiwa Capri Point naona mandhari ni nzuri sana, ila nikienda Mabatini au Igogo na Kitangiri naona utofauti. Low income earners mazingira yao lazima yawe duni ukilinganisha na high income earners areas, the same to developing and developed countries.
 
Kuna uzi uliikandia sana Mbeya mkuu, nadhani uzi ulikuwa ni comparison kati ya uswahilini ya mikoani na Dar. Hapo tatizo ni mipango miji na ongezeko la watu especially maeneo ya low income earners. Kwa mfano makazi ya watu wa Uzunguni, Uhindini, New Forest au Block T, huwezi linganisha na Ilolo, Sinde au Makunguru/ Jua kali.

Nikiwa Capri Point naona mandhari ni nzuri sana, ila nikienda Mabatini au Igogo na Kitangiri naona utofauti. Low income earners mazingira yao lazima yawe duni ukilinganisha na high income earners areas, the same to developing and developed countries.
Ni sahihi. Maeneo ya high income earners yanakuwa well organised
Lakini uchafu pia, inaweza kuonekana nakandia sana Mbeya ila kiukweli mitaa ya low income earners ni michafu, lakini si lazima sehemu wakiishi masikini basi ndio pawe pachafu
Mbona kuna nchi Africa hapahapa ni masikini lakini sio chafu kama Tanzania au majority of other African countries
 
Malezi ni sifuri, hatufundishwi kuwajibika Angali wadogo. Kuwajibika kwetu ni msamiati Tu usio na maana...Malezi ndiyo Kila kitu, ukiangalia huo mfano wa Rwanda, wanyarwanda ambao nawafahamu mm ni wasafi halafu vitu viko kwenye mpangilio wenye unafuu kuliko Sisi, yaani kwenye standard za usafi wametuacha hata Kwa level ya mtu mmoja mmoja.

Hata upite na bunduki mtaani kutishia watupa taka bado Tu kuna watu watatupa.

nakumbuka miaka Fulani kule Tanga walikuwa na kampeni ya usafi inaitwa Kalembo day, yaani Hadi hiyo siku ifike ndo watu wanakimbizana kwenye usafi wakati ni Jambo linalotakiwa kufanywa Kwa Kila siku, njoo kwenye nyumba zetu ndo utajua Sisi ni mapimbi wenye miguu miwili nyumba ziko hovyo hovyo, mtu akiamka shuka hatandiki vizuri, shuka chafu, chumba hakifagiliwi, bukta na chupi zipo dirishani, vitana na mafuta yako uvunguni yaani Kila kitu hakipo mahali pale, nenda vyooni sasa hizo harufu na uchafu kwenye masink, sasa watu wa Aina hii watakuelewa kweli unapowaambia masuala ya usafi na mpangilio, tena mijini watu hutoa pesa za usafi lakini wapi watendaji wanakula buyu Tu wanapita kushoto.

Kuna jamii Hapa TZ ukiingia nyumba zao zinapendeza hata kama uchumi si mkubwa mfano Mabohora, hawa Jamaa Kila kitu huwa kinakaa sehemu Yake sasa ukiwa na jamii kama hii ni rahisi Sana kukuta mazingira safi, ww Angalia maeneo mengi tuliyojazana sisi waafrika weusi pako hovyo hovyo Tu, Malezi ni muhimu Sana.

Mtu kanunua bidhaa anakula anatupa Ganda au plastiki barabarani au unakuta anatupa dirishani wala hajali, mtu anakamua kamasi anajifutia na nguo Yake. Umaskini si Tatizo pekee Bali Malezi yetu mabovu, tunazaliwa ili kujaza dunia Tu.
Hii ni sahihi sana. Inapaswa tuwe wastaarabu kuanzia kwenye personal level. Ni kweli tuna kazi kubwa ya kufanya
 
Wasimamizi wanaopewa msmlaka bogus
Wananchi bogus nao

Ova
 
Kwa sababu civilization ni kitu tuliletewa na mkoloni, ni kama uende porini uwakute nyani uwalazimishe kuvaa suti kwa viboko halafu baadaye uondoke uwaache, mwisho wa siku utakuta wapo hovyo kimpango wao kwa sababu mavazi sio kitu walichojifunza wenyewe kutokana na changamoto za maisha yao
Lakini Namibia, Rwanda na Botswana zipo organised vizuri tu. Watu wake ni wastaarabu na miji yao ni misafi
60+ yrs of independence, kweli tumeshindwa ku-master civilisation?
 
Wasomi mafisadi walio ktk ngazi ya maamuzi ambao ni wakuja.
 
Ul0q0
Ni sahihi. Maeneo ya high income earners yanakuwa well organised
Lakini uchafu pia, inaweza kuonekana nakandia sana Mbeya ila kiukweli mitaa ya low income earners ni michafu, lakini si lazima sehemu wakiishi masikini basi ndio pawe pachafu
Mbona kuna nchi Africa hapahapa ni masikini lakini sio chafu kama Tanzania au majority of other African countries
Mkuu sehemu ambazo masikini ni wengi authorities zinakuwa out of control ukilinganisha na sehemu za watu wanaojiweza.
 
Ul0q0
Mkuu sehemu ambazo masikini ni wengi authorities zinakuwa out of control ukilinganisha na sehemu za watu wanaojiweza.
Dah.. Ila sawa
Sema na hili suala la Africa kuwa masikini kiasi hiki nalo linanisikitisha sana. Kuna namna tu naona sisi ni wazembe
Sema sawa, point yako nimekuelewa mkuu
 
Yani wanawapa akina nani, foreigners au investors?
Wauza magari nk,bora basi uwekezaji pale biafra ungefanyika kimpangilio
Syo huo wa kiovyoovyo
Eneo kubwa kama lile wangeweza kujenga kitu cha maana lkn matumizi ni ya ovyo kabisa

Ova
 
Hili swala hata mimi nashangaa sana, maeneo mengi yaliyojengwa na wakoloni yamepangika mno, na maeneo yaliyojengwa na sisi mengi yapo shaghalabaghala. Inasikitisha sana
Miji ya ccm ni kama Mafinga, Tunduma, Kahama, Kasulu, Kibondo, Kakonko, Chalinze, Mkuranga, nk yote hovyo
 
Mimi naona shida ni wizara ya ardhi na halmashauri za miji zinashindwa kusimamia ugawaji wa maeneo vizuri, pia wanashindwa kutengeneza sheria ndogo ndogo za mazingira. Matokeo watu wanajiuzia maeneo kiholela bila kufuata utaratibu sehemu ya nyumba mbili zinakaa nyumba 7 hakuna hata eneo la kupanda mti , kwa mfano jiji la Mbeya siku za nyuma lilikuwa la kijani, kwa sasa hvi sehem kubwa za Mbeya zimekuwa kama uswazi hakuna miti tena ni vumbi kali kika sehemu kila kaeneo kadogo kanajengwa, Ulaya sehemu kubwa nyumba huwa zina maeneo makubwa.
 
Miji ya ccm ni kama Mafinga, Tunduma, Kahama, Kasulu, Kibondo, Kakonko, Chalinze, Mkuranga, nk yote hovyo
😂😂😂 Hiyo Kahama inakua kwa kasi sana kutokana na mzunguko mkubwa wa hela kutoka kwenye madini, lakini hadi leo barabara zake ni mbovu na mpangomji hakuna
 
Back
Top Bottom