Kwanini Mama wa Kambo huwa na Visa?

Kwanini Mama wa Kambo huwa na Visa?

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,917
Nakumbuka enzi Mzee kanitoa bush kuja kuishi na mama wa kambo town.. Darasani nikawa moto zaidi ya watoto wake. Haikumfurahisha, siku tukifunga shule na kuleta matokeo, nipo juu with flying colours. Sasa dingi hawezi nisifia mbele za Mke wake (my stepmother) tukiitwa sebuleni kutoa report za matokeo mi yangu ni "excellent" na "Very Good"... Kwenye tabia pameandikwa "Best Conduct"..

Mama wa kambo si masimango hayo, kuwa nafanya vizuri sababu nakula bure, nalala bure kwenye umeme na kutumia choo cha kuflash...Asijue hizo ni haki zangu za "kikatiba" mana huyo ni baba yangu, nastahili hayo yote.. Sasa mzee kwa kumuogopa mkewe akawa hawezi kunipongeza kwa zawadi, zaidi ataniita pembeni na kuninunulia zawadi ambayo ni "Perishable" - yaani msosii au chochote ambacho sitafika nacho nyumbani ili wale wadogo zangu wasione wivu.

Ugomvi mwingine ulikuwa ni wa kuongea "kilugha" na baba mzazi, kwa kukulia kwangu kijijini nilikuwa mahiri sana wa lugha ya kikwetu, na nililelewa kuamini kuwa mtu wa heshima kama mzee lugha sahihi ya mawasilino si Kiswahili. Mama hakupenda akihisi namteta (maana hakuwa wa kabila moja na baba). Mzee alipenda sbb ilimkumbusha asili yake, na pia alijifunza kupitia mimi misamiati mingine ya ndani ambayo mi niliichota kwa babu yangu..

Kuna wakati tulizama katika maongezi na baba alicheka sana katikati ya maongezi sababu ya utamu wa lugha...maana story za kilugha zina utamu wake, ilimuudhi mama wa kambo akahisi ninajenga ukaribu na baba kuliko wanae.

Nilipokuwa wa pili darasani, aliniuliza unataka nini? Nikamwambia nipeleke jando, maana nilikuja mjini nikiwa bado nina "mkono wa sweta", hali hii ilinipotezea sana kujiamini mbele ya watoto wenzangu mana walinicheka sana kwa kuwa wengi kama si wote wa umri wangu washakuwa wamekata.

Mbaya zaidi na watoto wa kike mtaani walijua kuwa nina "mzula" kutokana na nilivyokuwa nataniwa. Muhula huo zawadi ya kupelekwa jando ikafa, maana baba alinambia natakiwa kwenda kijijini kwa babu na bibi. Babu alinipenda sana sasa alikuwa kaomba niende, nikapewa ahadi ya likizo ijayo kama nitafanya vizuri basi ntaenda Jando maana pia utakuwa ni msimu wa baridi kwa kidonda kupona haraka.....Muhula ujao nilikaza msuli sana lakin nikaishia nafasi ya pili darasani.

Wakati ukafika nikaenda Jando baada ya kurudi kwa babu mana nilimpa story babu za mjini navopata tabu na kuchekwa halafu dingi ananipiga kalenda. Babu yangu hakupenda sana, alipenda niende jando la porini, aliamini kutibu kidonda cha Jando kwa mitishamba ambayo huongeza nguvu za kiume, mara kidonda kikipona, aliamini kuna namna ya ufanisi kwa mwanaume aliyeenda Jando la porini na yule wa Hospitali kwa kuitibu mishipa ya fahamu kwenye kichwa cha "mjomba".

Pia, Jando la porini vijana hukaa na wazee na kufundishwa miiko na namna ya kuwa baba wa familia. Kwa kufanyiwa Tohara mjini, basi mi ningekosa hizo "fursa".

Mbaya zaidi babu alipata story za jinsi wadogo zangu wale wa mjini jinsi vidonda vyao vilikuwa vinasafishwa na nesi wa kike, jambo lililomuuzi babu, maana mila haziruhusu.. Kwetu vijana walioenda jando huitwa "Wanyamlusi". Hupewa vifimbo vidogo "sungururu" ili kujikoa kwenye "enka" ili kumtuliza "mjomba" anaposimama.

Hali ya kutailiwa iliniongezea kujiamini, nilitamani nirudi mjini haraka, hata wengi wajue kuwa hali iliyonipa unyonge wa ndani haipo tena.

Maisha kwa mama wa kambo yaliendelea, alijaribu kutengeneza ukuta kati yangu na wadogo zangu aliozaa yeye. Huku upande wa shule hali ilikuwa nzuri, nilifaulu Kidato cha Kwanza kwenda Tabora Wavulana, enzi za Tabora ya Jeshi, Afande Chacha mzee wa mwendo legeza. Nilipokuwa narudi likizo niliwafundisha wadogo zangu..

Wakakua nami nikakua, nilichaguliwa tena Tabora wavulana kwa kidato cha tano na sita, nikawa mwalimu mzuri wa tuition kwa wadogo zangu walioanza nao elimu ya upili, hawakutamani tuition za walimu wa mtaani...walinielewa...kupitia nondo zangu na mbinu za kusoma wakafanya vizuri sana..

Mwingine nilimkazania ku-reseat mpaka akaenda SHY-BUSH, Wakagundua mi ni ndugu yao mwenye upendo... Sasa wakaanza kujaribu kunipenda japo mama yao alikuwa hajawatoa kwenye minyororo ya chuki dhidi yangu.

Baba hakuwa tayari kunisifia hadharani na kunitia moyo mbele za mke wake kwa kuogopa kumuudhi. Mahali nilipofanya vizuri aliniita faragha na kunipa moyo, aliona kitu cha pekee ndani yangu, lakini kimvuli cha mama wa kambo kilimtisha!

Maisha yakaenda, wadogo zangu wakakua nami nakakua...upendo na harakati zangu zikawasogeza, walichopewa kwa siri na mama yao ili mimi nisifaidi nao wakanipa kwa siri.. Walianza kung'amua kuwa mie ni ndugu yao ninayewapenda.

Nikawa mkaka, nikaenda chuo...Nikawa sasa kama kiongozi wao, wao wakajua tofauti yetu ni mama tu lakini baba yetu ni wa wote. Ukiingia sebuleni tulipokaa pamoja na mzee huwezi jiuliza.. Maana nilifanana nae kama jezi za timu ya mpira tofauti namba tu, wakaanza kuniita kaka, tofauti ya mwanzo walipokuwa wananiita jina langu la kijijini Madeha.

Sasa tumekuwa wakubwa. Ukitukuta huwezi jua kama tumechangia baba tu, tunapendana na kuheshimiana sana. Mama(my step mother, maana sasa huwezi jua kama si mama yangu jinsi anavyonipenda) amekuwa rafiki, mambo mengine hunambia mimi badala ya watoto aliozaa, hunitumia pia kuwashauri wanae wanapoteleza...Mimi ndio muitisha vikao vya familia na kuwa katibu wa kikao cha Mwenyekiti Baba..

Haya ni maisha niliyojifunza kwa Mama wa kambo. Wakati mwingine wamama wa kambo hawana ulazima wa kuwashurutisha watoto wao kuwachukia watoto wa kambo..Kuna namna ya kuwalea na kuwaelewesha kuwa watoto wote ni ndugu. Hata Wababa pia, wawe na ujasiri wa kuwakanya wamama wanaowasumbua watoto wao wa kambo.

Hivi ni jadi Wamama wa Kambo kuwatendea sivyo watoto wasio wao? KWANINI Wababa hukosa sauti mbele ya mama wa Kambo? Na Mbona wababa wa kambo huwa hawana visa kama mama wa Kambo?
 
Mkuu hiyo ni kawaida ya wamama wa kambo ingawa sio wote. Tabia hii si nzuri na inaumiza sana. Ni vizuri wamama wa aina hii wakaelewa na kujifunza kuwalea malezi sawa na wanayowapa watoto wao . Umenikumbusha mbali sana mkuu nimeona mama flani wa kambo alikua anawachukia sana watoto wa mumewe. Ushukuru wewe ulikua mtoto wa kiume ungekua mtoto wa kike ungenyanyaswa kupita hapo. Kama ujuavyo watoto wa kike wana mahitaji mengi ambayo mama ndiye anaepaswa kuyasimamia nikikumbuka hili huwa naumia sana. Lkn kupitia tabia zao mbaya badala ya kumdidimiza mtoto wa kambo hubadilika na kuwa mafundisho kwake na pia humjengea ujasiri na uwezo mkubwa wa kuishi na watu tofauti tofauti.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Pole kwa bahati mbaya uliyoipata kupata mama wa kambo mwenye roho ya kuntu,wa kwangu mimi anajitahidi sana
Ukarimu na Mungu amzidishie kila jema,lnshaaaalah!
 
Sie mama wa kambo tu...hata ex wives huwatia roho mbovu watoto wao kuwa mama wa kambo ni mbaya huo ni mtihani mkubwa nlionao mimi inaniuma sana any way yakinifika kooni ntayaleta hapa nipate ushauri zaid
 
Hii ndio inaleta ugumu hata kwa wanawake kuolewa na wanaume wenye watoto tayari utajitahidi uwalee vizuri lakini utapata mitihani kwa ndugu wa mume au watu wanaokuzunguka hali inayopelekea kuwa na chuki na kuanza kulipiza kisasi ni ngumu pia kwa mama wa kambo.
 
Hii ndio inaleta ugumu hata kwa wanawake kuolewa na wanaume wenye watoto tayari utajitahidi uwalee vizuri lakini utapata mitihani kwa ndugu wa mume au watu wanaokuzunguka hali inayopelekea kuwa na chuki na kuanza kulipiza kisasi ni ngumu pia kwa mama wa kambo.

Upo sahihi kabisa
 
Namna wanawake wawazavyo huwa wanajijua wenyewe....
 
Mkuu barafu nimeisoma story yako kwa umakini. I can imagine maana pia mimi nimelelewa na mama wa kambo.

Tofauti kubwa baba alikuwa sana upande wangu. Kiukweli baba anapenda sana watoto wake hata mama wa kambo afanye nini.

Baba alikuwa anasifia mbele yake. Ananunua zawadi na kuleta kwa mtoto yeyote atakayefaulu. Kiukweli baba alitufanya watoto tuwe kitu kimoja.

Sasa hivi mama wa kambo ni mshkaji sana tu. Ingawa akisema kitu inabidi uchanganye na zako.

Maisha ya mama wa kambo ni challenge kubwa sana.
 
Last edited by a moderator:
kuna jambo moja ambalo watu wengi husahau kwamba huwez hata siku moja kushindana na mipango ya Mungu dhidi ya mtu. Mungu kama kapanga fulan utoke utatoka tuuu hata mtu akuwekee ukuta namna gani, bado utapewa jia ya kutokea.

nimefururah kwamba wewe hukujenga chuki kwa ndugu wala mama yako.
barikiwa
 
kuna jambo moja ambalo watu wengi husahau kwamba huwez hata siku moja kushindana na mipango ya Mungu dhidi ya mtu. Mungu kama kapanga fulan utoke utatoka tuuu hata mtu akuwekee ukuta namna gani, bado utapewa jia ya kutokea.

nimefururah kwamba wewe hukujenga chuki kwa ndugu wala mama yako.
barikiwa
Unajua mpendwa walio wengi huwa hawajengi chuki na huwa msaada sana kwa watoto wa mama husika. Lkn baba wa huyu kijana alikua anakosea sana kujifanya anaogopa na wababa wengi hufanya kosa hilo. Naikumbuka hii inaumiza mno msamaha ni jambo la msingi na tunapokataa kusamehe mara nyingi huwa hakuna faida kwani wengi hufanya upuuzi wa aina hii kwa sababu ya kutomjua Mungu na daima huwa nasema yeyote anaembagua mtu mwingine kwa sababu zozote Mungu amsamehe kwani hajui atendalo.
 
Barafu, naomba nitoe mtazamo wangu juu ya hii historia yako uliyo share..

Namna ulivyo toa hii story inaonyesha ulikuwa na akili yako timamu wakati hayo yanatokea. Hivyo kuna uwezekano kuwa hii habari ipo biased kwa kiasi Fulani. Ukiwa kama mtoto kujua mama anakuchukulia hivyo kuna uwezekana mkubwa hata wewe ulikuwa humwonyeshi heshima, pengine hata ulikuwa jeuri na mwenye kiburi… Sijui...

Pamoja na kuwa naunga mkono akina mama wengi wa kambo kuwa na visa kwa watoto ambao si wao ni wa Mwenza wao; bado wapo wengi tu ambao huwa ni wamama wema na hulea hao watoto kwa upendo. Wa mama wa kambo kuna makundi tofauti;


  1. Kuna wale ambao huwa na visa hata iweje hamtaki kabisa huyo mtoto.
  2. Kuna wale ambao yeye yupo ‘indifferent' hajali kabisa kuhusiana na huyo mtoto – yaani hata muda wa kumtesa hana sababu hana time nae.
  3. Kuna wale ambao huwa na upendo na akamjali kama mtoto wake kabisa ama kama vile anavyoweza lea mtoto yeyote Yule.

Tukimtazama Baba Yako:-

Sijaona mahala popote ukimlaumu na hali anastahili lawama pia. Mwanaume akiwa na msimamo juu ya watoto wake, mwanamke hata kama ana roho mbaya ni rahisi kuwa mwoga na kumshuka. Baba yako ana makosa sawa sawa kabisa na mama yako ingawa yeye ndio umetaka kuonyesha ndiye mwema na ndiye alikuwa na mapenzi ya dhati zaidi. Baba wa namna hiyo (kama baba yako) ndiye mbaya zaidi! Yeye kama kichwa cha familia na ndie kiungo kilichowaunganisha ilikuwa ni wajibu wake kuwa treat watoto wote sawa, mtoto akistahili pongezi asifiwe, akistahili adhabu aadhiwe wote kwa usawa.

Unakiri baba yako alikuwa akimwogopa mkewe… Unafanya kitu kinachostahili pongezi kama mtoto anaogopa kukupongeza na anaenda nawewe pembeni kukununulia kitu ambacho kipo Perishable. Nikisoma habari hii, mie naona baba alikuwa ni tatizo kubwa zaidi mana alikuwa ni mnafiki na alishindwa kujenga mahusiano mazuri kati yako wewe mtoto na mama yake. Kitendo cha kukuchukua na kukupeleka pembeni alikuwa akiongeza chuki ndani ya nafsi na akili yako juu ya mama wa kambo huku ukimuona baba ndio anakupenda zaidi. Mwanaume lazima kuonyesha misimamo katika vitu vya kifamilia hasa kama inahusu watoto wake! Ilitakiwa awe wazi kwa mkewe na si kuwa mnafiki hivyo.

Hata hivyo nafurahi your story has a happy ending na kuwa all is well and good.

Hongera sana.
 
Waswahili hawakukosea waliposema Mwenyezi Mungu hamtupi mja wake. Kama umeandikiwa mazuri basi yatakuwa mazuri tu na hakuna binadamu yeyote atakayeyazuia. Hongera zako nyingi.
 
Amfyeka motto nyeti kisa kakojoa kitandani

1421031990591.jpg
 
Daaaah pole mtoto,sasa kile kilichokatwa kimeludishwa?,hatma ya huyu kijana urijali wake?...so sad.
 
Back
Top Bottom