Hapo ndo waislamu mnafeli kujitetea, kama maana yake ni Amani iwe nanyi, kwa nini asiongee kiswahili hadi aongee kiarabu. Je, wote watanzania wanajua kiarabu?
Sijasema kwa maana ya hoja iliyopo. Ilo ni Tatizo kubwa kwa Waislamu, waislamu wengi unakutana nao utasikia Asalaam Alaykum, bila kujali huyu mtu anajua kiarabu au hajui.
Tumieni lugha kulingana na mazingira, linaweza likawa neno la kawaida ila kwa vile halipo kwenye lugha inayoeleweka kwa wengi katika jamii ya kitanzania inaleta mkanganyiko.
Mfano ukitumia lugha ya kiswahili ukawakuta watu, ukasema Amani iwe nanyi, hapo awe wa dini yoyote hadi mpangani ataitikia vizuri bila kua na maswali maswali.
Tutumie lugha kulingana na mazingira