Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Hata mie nimejiuliza, huyu Victor na Saloti wana amani kweli kujua walisababisha kifo kisichokuwa a hatia?
Victor aliishatangulia kitambo mbele ya haki, lakini hata hivo mimi nilihusika ktk tukio hilo, Victor was my friend, Habari ina upotoshaji. Ni kweli mimi na Victor wakati huo tukiwa 4th year eng. alikuwa na mahusiano na huyo marehemu Levina, wakati huohuo ana mahusiano na Saloti wa 1st year.

Levina alienda na Victor Silver sand, kuna picha zilipigwa zikionyesha Victor na Levina wakiwa na vinywaji na wenyefuraha hukohuko silver sand. Yupo pia mhadhiri wa B. Com alionekana akiwa nao akishuhudia hali ya upendo huo, jina nalihifadhi, na mimi nilikuwepo. Ugonvi ulizuka kidogo pale Saroti na kundi lake walipojaribu kuingilia furaha ya wawili hao. Huyu Saroti wa msoma alikuwa Kijana wa vurugu sana, nadhani alikuwa anavuta bangi. Alim-harasi sana huyo binti baada ya siku hiyo.

Kwa uelewa wangu Harassment za Saroti kwa Levina nadhani ndizo zilipelekea Mzee Punch kuingilia kati na kumuingiza Levina ktk orodha ya watakao punchiwa kama mwandishi anavyosema. Binafsi namtetea marehemu Victor, Yeye na Marehemu Levina walishawishiana kwa njia za kawaida. Lakini suala la kunyanyasa akina mama pale chuo, ni kweli walinyanyaswa kwa msaada wa mzee Punch! Hivi bado punch yuko?
 
Nilikuwa najiona muhenga humu kumbe kuna wahenga zaidi yangu,nimejifunza kitu kwenye hii stori,shukrani ziwafikie wahenga wote,endeleeni kufunuka juu ya hii issue.
 
LEVINA,

Jina zuri, apumzike kwa amani.

Nyinyi watu wazamani tufahamisheni kuhusu huyu Mzee PUNCH!
 
Kwa akili hizi na ukizingatia hawa wengi wao watakuwa ktk nyadhifa mbalimbali kwa sasa, ndio maana mambo yamesuasua sana nchini. Magu wanyooshe tu
 
Prof . shivji huyu huyu ninayemheshimu aliongea kauli dhaifu kama hiyo? Au alikuwa anamaanisha nini kuhusu saga hiyo labda sikuelewa??!!
Punch ilikuwa inaongozwa na lecturers na viongozi wa juu wa vyuo ikiwamo professors ....Sintashangaa kama nae alikuwa mmoja wapo wa punch hivyo kuitetea
 
Hivi hao PANCHI si ndio nasikia walimchora Rais Mwinyi na kumtukana matusi ya nguoni hadi chuo kikafungwa kwa muda!!!
 
Punch naamini kilikuwa kikundi cha wanafunzi wasio na nidhamu.Hawakujali maslahi ya Taifa,hawakujali pesa Za serikali zinazotokana na Jamii maskini,pia hawakujali walikuwa wametoka kwenye jamii maskini na walio wekeza kwenye Elimu Kwa faida ya vizazi vingi kwenye uhai wa Nchi yetu.
Kwa zama hizi kisiruhusiwe kumea kirusi hicho Cha PUNCH nina hakika ni hatari zaidi ya Ukimwi
 
Punch naamini kilikuwa kikundi cha wanafunzi wasio na nidhamu.Hawakujali maslahi ya Taifa,hawakujali pesa Za serikali zinazotokana na Jamii maskini,pia hawakujali walikuwa wametoka kwenye jamii maskini na walio wekeza kwenye Elimu Kwa faida ya vizazi vingi kwenye uhai wa Nchi yetu.
Kwa zama hizi kisiruhusiwe kumea kirusi hicho Cha PUNCH nina hakika ni hatari zaidi ya Ukimwi
Vijana wa sasa hivi ndo maana mnasoma kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu hamjawahi kugoma wala kudai haki zenu, Punch ilikuwa inachangamsha chuo mtu unapata hamasa ya kusoma machapisho yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kuna shule zilikuwa zinasikika kuwa mwanafunzi wa kike akifika anakuwa ameshachaguliwa na mwanamme, hakuna kusema hapana maana mateso yake hayavumiliki, mojawapo ilikuwa Mkwawa High School
Mkwawa TTC kulikuwa na Kundi linaitwa wasenegali
 
Back
Top Bottom