Kwanini Dar siyo ngome kuu ya upinzani?

Kwanini Dar siyo ngome kuu ya upinzani?

Ni kweli kabisa nchi zenye mwamko wa kimageuzi yanaanzia katika miji mikuu yake tafauti na Tz. Mi nafikiri kwa upande wa tanzania vilaza wengi wapo jijini Dar. Ukitaka kufahamu hayo ninayosema, jaribu kutembelea kwenye mikusanyiko mingi na hasa vijue mahali ambapo inafanyika mijadala mbali mbali. Utakuta pale kuna watu nadhafu sana hata wanaweza kukuogopesha kama unakawaida ya kutizama sura. Lakini ukisikiliza michango yao ndipo utakapogundua kua ni mizigo. Uvivu mwingi na uswahili umesababisha watu wengi jijini kutegemea ndugu zao kwa kila hali na hivyo wengi wa hawa vijana hawana kauli yao ila siku zote wanaiimba chorus ya kile anachoambiwa na mfazili wake. Anaweza kua ni mjomba, baba, dada, shangazi, mpwa nk. Ccm ni wataalamu wa kuchakachua na hivyo wamefanikiwa kupata bidhaa ya kuchakachua na siku zote mtu mvivu wa hata kazi za kujipatia kipato mwenyewe hana kauli. Atanunuliwa hata kwa sh. elfu mbili tu. Kwa mtizamo wangu pia Dar inawezakuwa na watu wengi wasiojua kusoma na kuandika kuliko mikoa mingine. Hivyo japokuwa ni kituvu cha vyanzo vya habari lakini uwingi wa habari zinazotolewa hawana habari nazo kama wale walio nje ya jiji. Kwa siasa za tanzania na uswahili wa mswahili tusitarajie mageuzi kuanzia katika miji ya mwambao. Yataanzia vijijini na kuja kuwaamsha hawa vilaza wa jijini. Hiyo ndio habari yenyewe.
 
Karibu nchi zote duniani ambazo zimekuwa na mwamko wa kisiasa na upinzani uliokomaa zimefanya hivyo baada ya kuteka mji wake wake mkuu au mji mashuhuri. Ni katika miji mikubwa ya nchi ndipo upinzani umeonekana kukomaa

Zambia - Lusaka
Kenya - Nairobi
Irani - Tehran
Thailand - Bangkok
Ukraine - Kiev
Uingereza - London


n.k

Lakini kwa Tanzania, Dar-es-Salaam jiji kubwa zaidi, lenye watu wengi zaidi na lenye kufikiwa na vyombo vya habari vingi zaidi siyo ngome ya upinzani Tanzania. Zaidi ya watu kujitokeza kushangilia na kuonesha kukerwa na serikali ya chama tawala mara kwa mara ni hao hao watu wa Dar ndio wanaipa nguvu CCM na sitoshangaa (natumaini isiwe) upinzani unaweza usinyakue mbunge tena Dar.

Ni kitu gani kinafanya Da isiwe ngome ya upinzani? Kwa mfano kushindwa kuchukua halmashauri hata moja, kushindwa kutoa mameya, madiwani wengi wakiwa bado ni CCM na wabunge bado ni CCM licha ya madudu yote. Na hasa ukizingatia kuwa Dar ndiyo yaweza kudaiwa kuwa ina wasomi wengi zaidi!!!!

Yawezekana lawama ziiangukie CCM au pongezi kwa kuweza kuchakachua nguvu za upinzani Dar? Kwa sababu hata kwenye kura za maoni utaona wana CCM Dar wanaonekana kuchangamka zaidi kuliko wale wa upinzani. Au mimi siangalii vitu kwa usahihi maana hata CUF haina nguvu Dar mahali ambapo tungetarajia kuwa na nguvu ya aina fulani.

Mkuu kuna pia Harare, the capital of MDC. Harare yoote ina mbunge mmoja tuwa wa ZANU PF naye aliingizwa kilazimalazima, madiwani wote ni upinzani na hata vitongoji vya nje ya jiji it's MDC all the way!!

Dar tatizo kubwa ni watu kutopiga kura especially the so called middle class, wao siku ya uchaguzi ndiyo siku ya kutembelea mashamba, kulewa, kutembelea jamaa nk,
 
DAR IN WATU MAKINI.......DAR NI NCCR-MAGEUZI PEKE YAKE NDO ILIFANIKIWA.......! DAR INATAKA FUUL TIME CHAMA KIWE "ON" KAMA ILIVYOKUWA NCCR........SIO VYAMA VINAVYOSUBIRI UCHAGUZI TULIVYONAVYO SASA......! vyama hivi vikiga ya NCCR vitafika mbali!
 
Lakini 1995 hakukuwa na TV na radio kama hivi sasa; hakukuwa na intaneti kama hivi, na hakukuwa na magazeti kwa wingi kama leo. Maana nimekuwa nikiwaambia watu kuwa kwanini 1995 watu walikuwa wameamka sana lakini 2010 watu inaonekana hawajaamka zaidi?
 
Hujuma kubwa inafanywa na serikali DSM kuhakikisha upinzani haufui dafu.

Baada ya uchaguzi wa mwaka 1995 wapinzani wengi walikata tamaa hata ya kupiga kura kwa kuamini kuwa hawatatendewa haki.

Imagine mwaka 1995 nilikaa kituo cha kupigia kura pale River Side kuanzia saa 12.00 asubihi mpaka saa 11.00 jioni bila hata masanduku ya kupigia kura kuwasili. Tangu wakati huo idadi ya wapiga kura Dar ni ndogo sana.

Wapinzani wanahitaji kufanya kazi ya ziada kuwashawishi wafuasi wao kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura kama wanataka kuona mabadiliko.

Na sisi kila mmoja wetu ajitahidi walao apate watu 20 wa kuwashawishi ili wajitokeze kupiga kura. Si tu kushabikia siasa bali kuongoza mabadiliko ambayo yataweza kuleta mapambazuko mapya katika jamii yetu.

Wakati uliokubalika ndio huu. Timiza wajibu wako kuleta mabadiliko na urithi mpya kwa vizazi vijavyo
 
mi nadhani sababu mojawapo pia ni wepesi wa walioshika hatamu kujirekebisha...japo si pote ila kwa dar sehemu kubwa pale wanapokosolewa huitana kuonyana na kureebishana...wapi walikosea na wafanye nini kuweka mambo bayana ....! kiasi kwamba ukitumia mbinu ileile ya 1995 sasa utashindwa vibaya na utakuja na kila aina ya kisingizio kama timu yetu ya taifa....!
 
This has been a mind boggling question for sometimes now. Lakini kama mojawapo alivyosema, tulipoanza siasa za mageuzi mwaka 1995, Dar ilikuwa ngome kubwa ya upinzani. Inasemekana kwenye uchaguzi ule majimbo yote ya Dar isipokuwa la Ilala yalienda upinzani. Lakini kwa sababu Tume ya Uchaguzi ni ya CCM wakaufuta ule uchaguzi. Uliporudiwa, wafuasi wengi wa upinzani walishajikatia tamaa na kujawa na hasira. Matokeo yake wengi walioenda kupiga kura ni makada wa CCM na matokeo yake ndio hapa.

Baada ya 1995, tatizo moja lililojitokeza ni kwamba wapinzani waliweka wagombea dhaifu sana ambao walishindwa kushawishi umma. Mwaka 2005, kulikuwa na mgombea makini moja Dar nzima-JJ Mnyika. Nguvu zote za CCM zilihamia Ubungo. Ukijumuisha na mhemuka uliosababishwa na JK kipindi hicho, pamoja na mauzauza ya Tume yetu ya uchaguzi bwana mdogo akapigwa chini. Safari hii tuna wagombea makini angalau watatu katika Dar wa upinzani: Mnyika (Ubungo), Halima (Kawe) na Mpendazoe (Segerea), na huko Kigamboni si haba. Nina imani kubwa kwamba majimbo haya matatu au angalau mawili safari hii yataenda upinzani.
 
Umenena! Dar kuna wapinzani kweli kweli na wanapiga kura. Sikumbuki ni kipindi kipi matokeo ya hesabu za kura yametolewa Dar bila mikwara, ama kucheleweshwa au kulalamikiwa. CCM wanajua hilo na wanachunga sana Dar na ndio maana waliweza kumbeba Dr Lamwai (hivi ni kosa nikisema walimhonga) akakacha upinzania akahamia CCM

Ikweli kabisa. Kama alivyosema Zak nguvu ya upinzani Dar inafinywafinywa tu na CCM tangu mwaka 1995 -- na siyo imepotea yenyewe kutokana na kupendwa kwa CCM. I'm ready to die defending this statement. Mwaka 2005 watu zaidi ya laki moja hawakupiga kura Temeke kutokana na majina yao kutokuwamo katika daftari la wapiga kura -- na kule ni ngome ya CUF. Ni dhahiri CUF iliathirika kule kimatokeo. Ni kama vile ukaweza kuzuia nusu ya wanawake wote nchini kwenda vituoni kupiga kura Oct 31. CCM itaathirika sana kwani ngome yao kubwa ya wapiga kura hapa nchini ni (I'm sorry to say) wanawake.
 
Unahitajika UTAFITI wa kina,
Ila kwa haraka naona kuna mpango ulishaandaliwa na CCM kutoruhusu upinzani ufurukute Dar. Zipo harakati nyingi ninazoziona ambazo ni well organize zikihusisha takrima kwa walalahoi waliowengi mjini kuhakikisha wanapiga kura kwa wagombea wa CCM. Lakini nilipoenda kujiandikisha kupiga kura niliangalia wananchi waliojitokeza kujiandisha kwa assessment ya haraka ni wale wasio na uwezo mkubwa wa uchumi ndio waliokuwa wengi sana. Hawa ni rahisi sana kushawikika kwa kupewa kitu kidogo na ndio wanaojitokeza kupiga kura. Mbinu nyingine ni hila za kutofungua UDSM kabla ya Uchaguzi, kwani kwa mtizamo wangu ninadhani jimbo la kwanza kuweza kuongozwa na upinzani ni UBUNGO.

Lakini pia kama wengi walivyosema, jamii ya asili ktk jiji hili, haiko tayari kufanya maamuzi magumu. Laiti Moshi ingalikuwa ndo mji mkubwa wa kibiashara, CCM ingalikuwa historia leo.

NINI KIFANYIKE
1) Wale wenye upeo na mwamko wa kisiasa wajitahidi kuwaelimisha wananchi wenzao wanaowazunguka.
2) Vyama vya upinzani viwe na mkakati endelevu wa kujijenga zaidi kwenye miji na kwa kuanzia Dar, kwani ni rahisi sana kutumia mass media zilizopo zaidi mijini. Pia watu wengi wanaoishi mijini wana upeo mkubwa zaidi kuliko wale wa mijini.
3) Pamoja na kulenga kuanzia mijini, upinzani unapaswa kulenga zaidi vijana na haswa wa sekondari za kata zilizosambaa nchi nzima.
 
Dar inawatu wengi wahovyo hovyo, mi nashangaa , mara kadhaa nikiwa hapo, nimewaona watu wasioshiriki siasa, wanajidai wako busy na mambo yao, halafu wanapenda sana kulalamika, wanapenda kuvuna wasipopanda. hao ndi wakazi wa mji huo.
kiwango cha kutojua haki na elimu ya uraia kiko chini, mnaniudhi sana.
 
Dar ndio sample ya aina ya watanzania wengi wasiotilia maanani haki zao za msingi katika kuzidai...na kuzisimamiaaa...

pamoja na fursa zote bado imekuwa nyuma kimwamko kisiasa kuliko tarime na karatu!!!!!
 
Hutakiwi kutumia akili sana kujua tatizo kwa nini - Ni u busy wa hali ngumu ya maisha ya wakazi wa dar. Mtu anaona hakuna haja kupanga foleni msululu mrefu just kujiandikisha daftari la wapiga kura wakati hana uhakika kwa msosi wake wa siku, - mimi mwenyewe nilijiandisha last day, siyo kwa sababu nilikuwa sitaki bali sikupata muda kabisa. unafika unakuta utaratibu hafifu, mambo hovyo hovyo sasa hiyo nayo inachangia. Leo hii NEC ikisema inaboresha tena daftari utaona watu kibao wanajaa kwenye vituo kujiandiksiha ukiwauliza walikuwa wapi hupati majibu kamili. kwa hiyo Kinachochangia zaidi ni mfumo hafifu wa Tume ya uchaguzi katika zoezi zima la kujiandikisha na upigaji wa kura. siwezi mimi kujipanga masaa 6 eti nasubiri foleni niingie kupiga kura sijui nchi za wenzetu pia wana utaratibu kama huu?

Mimi malalamiko yangu ni hiyo Tume ya Uchaguzi na hili zoezi zima la uandikishaji na upigaji wa kura. Wakiboresha zoezi zima la uandikishaji na upigaji wa kura basi utaona watanzania hata zaidi ya 30m watakua kwenye daftari. leo hii watanzania 19m tu kati ya 50m ndiyo wanao qualify kupiga kura na kati ya hao watakaojitokeza wanaweza kuwa 16m. Tusubiri mtaona.
 
kuna jamaa angu alikuwa mwanza alikuwa mzuri sana katika mambo ya siasa baada ya kuhamia dar amekuwa Kilaza mbayaa
 
Dar waislam ni wengi na ndio wanapenda ccm, alafu wengi ni elimu ya madrasa kwahiyo kujua dunia inakwenda wapi ni shida
 
Dar waislam ni wengi na ndio wanapenda ccm, alafu wengi ni elimu ya madrasa kwahiyo kujua dunia inakwenda wapi ni shida

K.m. ni na zako! Uislam na hayo wapi na wapi? Kule Pemba ni wayahud wale? Acha ubaguz wa kidini pimbi wewe!
 
Dar inawatu wengi wahovyo hovyo, mi nashangaa , mara kadhaa nikiwa hapo, nimewaona watu wasioshiriki siasa, wanajidai wako busy na mambo yao, halafu wanapenda sana kulalamika, wanapenda kuvuna wasipopanda. hao ndi wakazi wa mji huo.
kiwango cha kutojua haki na elimu ya uraia kiko chini, mnaniudhi sana.

Watu wengi wa dar wameadhiriwa sana na wadharamu awapendi kufanya kazi kwa bidii, wanapenda sana kuombaomba na hilo ndio tatizo kubwa
 
Dar waislam ni wengi na ndio wanapenda ccm, alafu wengi ni elimu ya madrasa kwahiyo kujua dunia inakwenda wapi ni shida

Wewe mjinga mm nafkiri mama yako na baba yako ndio ambao hawajui maisha yanaenda wapi , mpaka wakakufanya wewe uone siasa ni sehemu ya kukupeleka wew mbele.
Mbona huongei kitu kuhusu Dubai , Saudia, Qatar, Oman wote hao ndio wanamaisha mazuri tu.
 
Back
Top Bottom