Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

Tunaomba percentage wise ya kuanguka kulinganisha na soko la dunia ilivyoanguka
 
Kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta duniani kutoka $110 hadi $ 58 leo, itabidi bei elekezi mwezi ujao ishuke hadi sh 1,300 kwa lita au chini ya hapo. Watumiaji vyombo vya moto tuwe makini tudai bei ya chini, otherwise serikali itatoza kodi kubwa kufidia nakisi ya bajeti. Tuangalie haki zetu
 
haha,

wewe unaota ndoto za asubuhi, hata yatolewe bure huko arabuni, bei yako itapanda tu, wajomba hawaishiwi sababu hao.watakuambia gharama za usafiri zimepanda, bahari imejaa maji zaidi, hewa ya uarabuni imekuwa nzito, ilimradi tu..,
 
EWURA Ndo wanasaidiana na wezi, kwanini tusiwakatae EWURA jamani, mafuta yanapaswa kuwa 1400-1700 tu sio 2000TZS kama ilivyo sasa
 
Kwa sasa mafuta ni 1980 Petrol na Diesel 1860 tunatarajia yaendelee kushuka kabisa hadi 1300 kabisa...
 
Tatizo shilingi imepoteza thamani. Hizi sarakasi zinaathiri vingi ndani na nje ya nchi. Ngoja tuuguze tezi dume kwanza
 
Kwa sasa mafuta ni 1980 Petrol na Diesel 1860 tunatarajia yaendelee kushuka kabisa hadi 1300 kabisa...

Na pia gharama za usafiri wa Umma zishuke na gharama za bidhaa zishuke na gharama za umeme pia zishuke. Maana zote zinaguswa moja kwa moja na gharama za mafuta.

Ila kama John Hopkins Hospital hawajalipwa hela yao ya kumpasua mtu busha usitegemee gharama ya mafuta kushuka...
 
Kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta duniani kutoka $110 hadi $ 58 leo, itabidi bei elekezi mwezi ujao ishuke hadi sh 1,300 kwa lita au chini ya hapo. Watumiaji vyombo vya moto tuwe makini tudai bei ya chini, otherwise serikali itatoza kodi kubwa kufidia nakisi ya bajeti. Tuangalie haki zetu
umenena mdau. ndio tutaona kama ewura inalinda watumiaji wa mafuta au wanaendeleza unyonyaji wa wafanya biashara
 
Kwa sasa mafuta ni 1980 Petrol na Diesel 1860 tunatarajia yaendelee kushuka kabisa hadi 1300 kabisa...

Mkuu unajazia wapi......?......niambie sasa hivi niwashe Puma kutoka hapa Yaeda.........nije kujaza......hata kama ni huko Mbozi............
 
Nihabari njema lakin ninjema kwa majizi,na ewura,wananch hatuna letu
 
Mkuu unajazia wapi......?......niambie sasa hivi niwashe Puma kutoka hapa Yaeda.........nije kujaza......hata kama ni huko Mbozi............

Binamu huyu jamaa Ana jazia wapi maana sasa Leo na petrol imesimama shs.2029....
 
Kushuka huwaga ni issue hapa kwetu sasa live ni $ 55.94 kwa barrel ila hapa sasa dollar inakuwa na nguvu na kwa misingi yetu tunaweza mpaka feb tukana Tshs ikiwa 1950 hivi sasa hapo kushuka inaweza kuendelea kuwa shida. Ila kimsingi ilitakiwa kushuka sana
 
Kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta duniani kutoka $110 hadi $ 58 leo, itabidi bei elekezi mwezi ujao ishuke hadi sh 1,300 kwa lita au chini ya hapo. Watumiaji vyombo vya moto tuwe makini tudai bei ya chini, otherwise serikali itatoza kodi kubwa kufidia nakisi ya bajeti. Tuangalie haki zetu

Yaonekana unatabili Lake oil iungane na Panone. Hahahaaaaa!
 
Tatizo shilingi imepoteza thamani. Hizi sarakasi zinaathiri vingi ndani na nje ya nchi. Ngoja tuuguze tezi dume kwanza

Shillingi imeshuka thamani kwa asilimia 4.5% sasa tukitoa punguzo la thamani la bei ya mafuta katika soko la dunia ambapo inafikia 47.3% tunapata salio la 44%. Sasa tukizidisha kwa bei ya Tshs 2190 iliyokuwa hapo awali inamaan bei ya sasa ilitakiwa iwe ni Tshs 1,226 msitake kutudanganya bana shusheni bei mnatuumiza!!!! Ila mitanzania ndivyo tulivyo tutaishia kulalamika tu hamna kitu huku tunaumizwa na bei za kulanguliwa za mafuta
 
Binamu huyu jamaa Ana jazia wapi maana sasa Leo na petrol imesimama shs.2029....

Ngoja nizidi kumuuliza huyu ndugu Ili tujue.......weka LX V8 on binamu..........nakupitia.......
 
Riz1 atawambia wanzake wagome, maana hata ya sasa wanapiga sana deal.
 
Kwa sasa mafuta ni 1980 Petrol na Diesel 1860 tunatarajia yaendelee kushuka kabisa hadi 1300 kabisa...

Hiyo bei ni kwa mji gani kiongozi? Maana hapa DSM Petrol ni 2000-2029, Diesel ni 1900-1910. Tunapigwa sana sasa.
 
Nikija kutana na mtu yyt wa ccm peponi, mii ntatoka!
 
Back
Top Bottom