Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

kwenye soko la dunia petrol imeshuka sana sijui kwanini hapa bongo haishuki
 
Bongo ni nadra sana kukuta kitu kinashuka bei
 
Mbona imeshuka kidogo sana?? Wakati bei ya pipa moja katika soko la dunia imeshuka toka $68 had $40.

Hivi mkuu unaweza kuwa na mabadiliko ya bei za wese tangu 2000 mpaka leo katika soko la dunia ili tuone ni kwa kiasi gani hawa mafisadi wa wese wanavyofanya maisha ya mtanzania kuwa magumu siku hadi siku? Please.

On the other hand I think suala la kushuka litachukua mda kwa sababu wafanyabiashara wa wese bongo wanajifanyaga wajanja. Watakwambia stock walionayo waliinunua kipindi cha bei juu sasa hawawezi kushusha ghafla watapata hasara. Thats what happens in this country. Sidhani kama kunaweza kushusha bei fasta fasta hivi.
Tuombe tu mafisadi waondoke nchi hii. Wamefanya maisha yamekuwa magumu kwa mtanzania wa chini. Wanaweka hela zao nje wananufaisha maisha ya wazungu ulaya na mashariki ya mbali wakiacha watu wao wanateketea
 
Delivery ina matter sana katika bei za mafuta.

Mzigo unaoshushwa leo utakuta ulipakiwa na kununuliwa kabla bei hazijashuka.

Lakini tumeona toka kuanzishwa mfumo huu bei zikipanda na kushuka. Tutegemee bei za miezi miwili au mitatu ijayo kuwa zitakuwa na unafuu.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Kwahyo wakienda tena kununua na kukuta bei imepanda watakuja kutuuzia kwa bei ipi??
 
mbona mimi huku nlipo.imeshuka kama week 3 au mbili nyuma.
nakumbuka nlikuwa nanunua 2482/litre ila sasa hivi ni 2120.

Does it reflect the reality in the world market? NO.

A price of one barrel dropped from 68$ to 40$.

For this case your price should have been at least 1500-1700
 
Hivi mkuu unaweza kuwa na mabadiliko ya bei za wese tangu 2000 mpaka leo katika soko la dunia ili tuone ni kwa kiasi gani hawa mafisadi wa wese wanavyofanya maisha ya mtanzania kuwa magumu siku hadi siku? Please.

On the other hand I think suala la kushuka litachukua mda kwa sababu wafanyabiashara wa wese bongo wanajifanyaga wajanja. Watakwambia stock walionayo waliinunua kipindi cha bei juu sasa hawawezi kushusha ghafla watapata hasara. Thats what happens in this country. Sidhani kama kunaweza kushusha bei fasta fasta hivi.
Tuombe tu mafisadi waondoke nchi hii. Wamefanya maisha yamekuwa magumu kwa mtanzania wa chini. Wanaweka hela zao nje wananufaisha maisha ya wazungu ulaya na mashariki ya mbali wakiacha watu wao wanateketea




commodity-crude-oil.png

Price of crude oil in US $ per barrel from Jan. 2000 TO 3rd Dec.2014 in the world market
 
Wapi dar au mikoani? Hapa tanga wanauza 2,300/lita

Ni Dar na vituo vya mafuta vya Total, hapo nilipowekea mafuta kituo cha Mbezi Africana pump moja tu ndio ilikuwa inatumika na ndio yenye mafuta peke yake basi ni foleni balaa
 
hii nchi kila mtu ni mpiga dili hata mama ntilie mchele ukishuka bei sokoni yeye hashushi bei ya chakula hii ndio bongo
 
Mbona imeshuka kidogo sana?? Wakati bei ya pipa moja katika soko la dunia imeshuka toka $68 had $40.
Hapa mafuta yakipanda siku moja nao wanapandisha siku hiyo hiyo lakini yakishuka inaweza kutumia hata miezi sita!

 
Ni Dar na vituo vya mafuta vya Total, hapo nilipowekea mafuta kituo cha Mbezi Africana pump moja tu ndio ilikuwa inatumika na ndio yenye mafuta peke yake basi ni foleni balaa

Mkuu Total leo inasomaje bei?
 
Mbona ikipanda kesho yake ewura washa update bei mpya? Kwny kupanda waga haiangaliii stock ni ya lini?
 
Hapa mafuta yakipanda siku moja nao wanapandisha siku hiyo hiyo lakini yakishuka inaweza kutumia hata miezi sita!


Hayo ndo matatizo ya serikali dhaifu kwenye kusimamia sera zake.
 
Hivi mkuu unaweza kuwa na mabadiliko ya bei za wese tangu 2000 mpaka leo katika soko la dunia ili tuone ni kwa kiasi gani hawa mafisadi wa wese wanavyofanya maisha ya mtanzania kuwa magumu siku hadi siku? Please.

On the other hand I think suala la kushuka litachukua mda kwa sababu wafanyabiashara wa wese bongo wanajifanyaga wajanja. Watakwambia stock walionayo waliinunua kipindi cha bei juu sasa hawawezi kushusha ghafla watapata hasara. Thats what happens in this country. Sidhani kama kunaweza kushusha bei fasta fasta hivi.
Tuombe tu mafisadi waondoke nchi hii. Wamefanya maisha yamekuwa magumu kwa mtanzania wa chini. Wanaweka hela zao nje wananufaisha maisha ya wazungu ulaya na mashariki ya mbali wakiacha watu wao wanateketea

Bei ikipanda wanapandisha ghafla regardless na siku ya kununua na stock date.
 
Does it reflect the reality in the world market? NO.

A price of one barrel dropped from 68$ to 40$.

For this case your price should have been at least 1500-1700

Mkuu hiyo price ya $ 40 umeitoa wapi ? Price ilikuwa around $ 110- $ 115 kabla ya August, ikaanza kushuka taratibu mpaka wiki hii inachezea $ 66 - $ 73 per barrel na ndio the lowest for almost 5 years..
 


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI KIKOMO ZA MAFUTA AINA YA PETROLI KUANZIA
JUMATANO, TAREHE 3 Desemba 2014
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, Tarehe 3 Desemba 2014. Pamoja na kutambua bei kikomo za bidhaa mbalimbali za petroli nchi nzima, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:-
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

(a) Bei za jumla na rejareja kwa aina zote za mafuta, yaani, Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeshuka ikilinganishwa na toleo lililopita la tarehe 05 Novemba 2014. Katika toleo hili, bei za rejareja kwa Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimepungua kwa viwango vifuatavyo: Petroli Sh 149/lita sawa na asilimia 6.83 Dizeli Sh 119/lita sawa na asilimia 5.85 na Mafuta ya Taa Sh 106/lita sawa na asilimia 5.31. Aidha, kwa kulinganisha matoleo haya mawili, bei za jumla zimepungua kama ifuatavyo: Petroli,Sh 148.66/lita sawa na asilimia 7.16, Dizeli, Sh 118.69/lita sawa na asilimia 6.16, na Mafuta ya Taa,Sh 105.81/lita sawa na asilimia 5.59.

Mabadiliko haya ya bei yametokana na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la Dunia na kupungua kwa gharama za uagizaji mafuta, bei za mafuta katika soko la ndani zingepungua zaidi, isingekuwa kuendelea kupungua kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania dhidi ya Dola ya Marekani.

(b) Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2008, bei za bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko. EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta.

(c) Kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi bei hizo ziko chini ya bei kikomo (price cap) kama ilivyokokotolewa na fomula iliyopitishwa na EWURA na ambayo ilichapwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 432 la tarehe 29 Novemba 2013.

(d) Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana na yakionyesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika. Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta kutoka kwenye vituo vinavyouza mafuta kwa bei ndogo zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika.

(e) Wanunuzi wanashauriwa kuhakikisha kuwa wanapata stakabadhi ya malipo inayoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita. Stakabadhi hiyo ya malipo itatumika kama kidhibiti cha mnunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko bei kikomo; ama endapo utakuwa umeuziwa mafuta yenye kiwango cha ubora kisichofaa.

Kwa taarifa zaidi tusome gazeti la Mwanachi, Uhuru na Guardian leo. Mafuta yameshuka kwa mwezi wa nne mfululizo wadau.
 
Kuwepo kwa bei ya juu ya mafuta hauhusiani kabisa na petrol iliingia lini nchini this is because of poverty,inflation and high cost of living. Bei haitashuka kwetu kabisa ingawa mataifa mengine yameshusha ingawa sio yote, usafirishaji wa mafuta kwa njia ya malori unachangia kiasi kikubwa kwa kupanda kwa bei na hii tutegemee pia kupanda kwa vyakula na hata real estate pia. Hapa hatuna la kujivunia cha kuuza nje ni kukubali huu umaskini wa kujitakia utakula kwetu kila kukicha
 
Back
Top Bottom