Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

Kwanini bei ya mafuta Haishuki Tanzania?

Shillingi imeshuka thamani kwa asilimia 4.5% sasa tukitoa punguzo la thamani la bei ya mafuta katika soko la dunia ambapo inafikia 47.3% tunapata salio la 44%. Sasa tukizidisha kwa bei ya Tshs 2190 iliyokuwa hapo awali inamaan bei ya sasa ilitakiwa iwe ni Tshs 1,226 msitake kutudanganya bana shusheni bei mnatuumiza!!!! Ila mitanzania ndivyo tulivyo tutaishia kulalamika tu hamna kitu huku tunaumizwa na bei za kulanguliwa za mafuta

Utaelekeza maombi yako hata kwa mlinzi wa choo kama hujajifunza namna ya kuandika.
 
chart hiyo ya mafuta kwa mwaka huu halafu utajaji mwenyewe kama rate ya kupanda kwa dola na kushaka kwa bei toka mwezi wa nane mpaka sasa tunatakiwa tuwe tunalipa kiasi hiki kweli?

GraphEngine.ashx
 

Attachments

  • crude oil picture.gif
    crude oil picture.gif
    22.7 KB · Views: 112
Binamu huyu jamaa Ana jazia wapi maana sasa Leo na petrol imesimama shs.2029....
Upo sawa 2029, ila tukumbuke kuwa shilingi yetu pia ina tatizo ingawa leo pia ilikua imara kidogo rates ilikua chini ya 1725
 
Mkuu pipa kwa jana na leo lipo chini ya 55Usd almost nusu ya bei iliyokuwepo Miezi mnichache iliyopita.

tatizo lililopo ni kuwa kunawezekano mkubwa makusanyo ya serekali yapo Constant kwenye mafuta na kwa vyovyote yapo kwenye 1500 constant!
 
mbona mimi huku nlipo.imeshuka kama week 3 au mbili nyuma.
nakumbuka nlikuwa nanunua 2482/litre ila sasa hivi ni 2120.

Kama kwenye soko la Dunia mafuta yameshuka kwa zaidi ya 40% inakuwaje EWURA wanashusha kwa 5%-6%? Wao wangeshusha kwa 20% ingesaound kidogo, hiki kinachfanywa ni kiini macho tu biashara za wakubwa kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.
 
Delivery ina matter sana katika bei za mafuta.

Mzigo unaoshushwa leo utakuta ulipakiwa na kununuliwa kabla bei hazijashuka.

Lakini tumeona toka kuanzishwa mfumo huu bei zikipanda na kushuka. Tutegemee bei za miezi miwili au mitatu ijayo kuwa zitakuwa na unafuu.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

We Gamba kwanini wakisikia mafuta leo yamepanda bei kwenye soko la dunia na wao wanapandisha hapo hapo hawasubiri stock walionunua kwa bei ya chini iishe ndipo wapandishe? We kubali tu kuwa "Serikali Yoote imewekwa mfukoni na mafisadi"
 
Nikija kutana na mtu yyt wa ccm peponi, mii ntatoka!

Wacha nicheke aisee. Inamaana CCM wote ni jehanamu ndio kunakowafaa...... hahaha pamoja na mama Rwakatare.... uwi haponi mtu hapo.
 
Upo sawa 2029, ila tukumbuke kuwa shilingi yetu pia ina tatizo ingawa leo pia ilikua imara kidogo rates ilikua chini ya 1725

yeah ni kweli usemacho juu ya currency yetu....
 
Kabla ya kutoa conclusion, awali ya yote tunatakiwa kuangalia trend na kufahamu bei ya mafuta ilianza kushuka lini na kwa upande mwingine tuangalie mzigo wa mwisho Tanzania ulikuja lini. Ikiwa bei, say imeanza kushuka two weeks ago wakati mzigo ulio sokoni umeingia kabla ya hapo then there's no way bei itashuka... mafuta sio kama maharage ya Mbeya kwamba, ukishasikia bei ya maharage imeshuka, siku hiyo hiyo unaweza kwenda na kesho kurudi na mzigo wa bei ya chini.

Hadi October 20 bei ya pipa 1 kwenye soko la dunia ilikua $110, imeendelea kushuka hadi leo ni $59.360, na niseme hivi, tokea bei imeanza kushuka haijawahi kupanda hata siku 1 huko kwenye soko la dunia, tukubali tu hapa kwetu tunalo tatizo, Burundi, Rwanda, Kenya, Africa kusini kote huko bei ya petrol na diesel imeshuka pia, bongo wala haishuki! Tunayo shida, tena kubwa hapa.
 
Hadi October 20 bei ya pipa 1 kwenye soko la dunia ilikua $110, imeendelea kushuka hadi leo ni $59.360, na niseme hivi, tokea bei imeanza kushuka haijawahi kupanda hata siku 1 huko kwenye soko la dunia, tukubali tu hapa kwetu tunalo tatizo, Burundi, Rwanda, Kenya, Africa kusini kote huko bei ya petrol na diesel imeshuka pia, bongo wala haishuki! Tunayo shida, tena kubwa hapa.

Hapa kwetu wanachokifanya akina Riziwani Kikwete ni kushusha thamani ya shilingi vs dola kwa kushirikiana na BOT ili bei ya mafuta ibaki juu. Fuatilia trendi miaka yote kila bei ya mafuta ikishuka soko la dunia na shilingi inashuka thamani,,, coincidence????
 
Sijui kama kuna thread tayari inazungumzia hii topiki lakini nimeandika kama iko tayari inaweza kuunganishwa na hiyo nyingine. Nina maswali ambayo wanaojua wanaweza kunisaidia. Swali langu la kwanza kama sikosei kuna chama au advocacy group kilichoundwa kwa mujibu wa sheria chenye lengo la kulinda walaji kwa hapa wanunuzi wa petroli? Kama kipo kimefanya nini kutetea kwenye hili jambo? Kila mtu anajua na hakuna siri wala kuwa na upeo wa ajabu kujua kuwa mafuta yameshuka kwenye soko la dunia na yameshuka kwa watumiaji wa mwisho I.e wale wanaonunua kwenye vituo vya mafuta duniani kote isipokuwa Tanzania. Tanzania bei zimepungua kwa kiasi kidogo sana sababu ni nini lakini? Je ni serikali inaogopa kuporomoka kwa mapato yake? Kwa hakika kama serikali ingekuwa si mnufaika wa hili bei ingekuwa imeshashuka kwa kiasi kikubwa. Je serikali haioni serikali za nchi nyingine imebidi zi adjust bajeti zao kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta kwa sababu mapato pia yatashuka?
 
Naunga mkono hoja,nawaombeni waheshimiwa wa EWURA mkuje hapa mtupatie majibu
Tutashukuru sana maana tunapigika kila upande,hasa sisi wafanyakazi
tunalazimika kubeba kila mzigo wa taifa hili.
 
Back
Top Bottom