Nkerebhuke
JF-Expert Member
- Nov 1, 2021
- 796
- 2,027
Inawezekana kuna kundi kubwa halijua maana ya elimu ndio maana imekuwa ni kawaida sana kuisimanga, kuibagaza na kuishusha elimu. Elimu ni maarifa, elimu ni ujuzi, elimu ni mwanga, elimu ni silaha, elimu ni kio, elimu ni Pesa, elimu ni tiba, elimu ni kila kitu kwenye Maisha ya mwanadamu yoyote katika Dunia yoyote. Leo anatokea mtu anadharau badala ya kutoa maoni namna gani tutaunda na kuboresha elimu yetu.
Watanzania baadhi wanakera sana na bahati mbaya wengine wako bungeni kuibagaza elimu sijui inawezekana tumerogwa. Watu wanakalili wanafikili wasomi wanaweza kufanya miujiza wakihisi pengine msomi ni malaika hapana. Taifa letu lina wasomi wazuri ambao ujuzi wao unatumika vizuri kuliletea maendeleo na ustaarabu taifa, wapo serikalini na sector binafsi.
Inasikitisha sana maana hii laana imewashukia hata wasomi wenyewe kuweza kujidhalau na kushindwa kujiamini, kutetea mawazo, kupigania taaluma za kulinda hadhi na heshima ya utu wao. Hivi leo watu wanaita vyeti makaratasi kwa dhihaka hii ni laana sio bure. Kama kuna changamoto kwenye elimu yetu, tuiboreshe na sio kuibagaza inakera sana tunadhalau elimu huku tukipeleka watoto wetu shule
Watanzania baadhi wanakera sana na bahati mbaya wengine wako bungeni kuibagaza elimu sijui inawezekana tumerogwa. Watu wanakalili wanafikili wasomi wanaweza kufanya miujiza wakihisi pengine msomi ni malaika hapana. Taifa letu lina wasomi wazuri ambao ujuzi wao unatumika vizuri kuliletea maendeleo na ustaarabu taifa, wapo serikalini na sector binafsi.
Inasikitisha sana maana hii laana imewashukia hata wasomi wenyewe kuweza kujidhalau na kushindwa kujiamini, kutetea mawazo, kupigania taaluma za kulinda hadhi na heshima ya utu wao. Hivi leo watu wanaita vyeti makaratasi kwa dhihaka hii ni laana sio bure. Kama kuna changamoto kwenye elimu yetu, tuiboreshe na sio kuibagaza inakera sana tunadhalau elimu huku tukipeleka watoto wetu shule