Kwanini baadhi ya wanaume hawaoi wadada wazuri?

Kwanini baadhi ya wanaume hawaoi wadada wazuri?

Quinton Canosa

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2012
Posts
1,224
Reaction score
1,258
Habari zenu wanajamii forum,

Kuna jambo ambalo nalishanagaa kidogo japo sina uhakika asilimia 100 but kwa utafiti nilikokafanya kidogo tu nimegundua wale wanawake wazuri na wenye sura na muonekano mzuri wanatafuta sana watu wa kuwaoa lakini watu wote wanawakimbia, sijui ni kwanini na mara nyingi sasa hivi wale wa kina dada wenye muonekana wa kawaida kisura ndio wanaolewa.

Ili kulithibitisha hilo kuna dada mmoja mzuri sana aliniambia anataka mtu wa kumuona ila kila mwanaume anasema hawezi kuoa presha sasa sijui wanaume wenzangu kunani ni kweli uzuri wao unawatisha au kunanini nyuma ya pazia jamani wengi wanataka kuolewa lakini wanaume wanataka kuwatumia tu kuwaacha.

Jamani tujadili kuhusu hili
 
ha ha ha ww ni mmojawapo kati ya wale wadada wakali enheee
 
uoga wao tu na kusikiliza stori za vijiweni
 
Simple. Those who can't run with the big dogs, stay on the porch. Where's my big dogs at??
 
Kizuri gharama, tuwe wakweli kuna mtu kwa jinsi alivyoumbwa (kwa maana ya urembo & figure yake) dhamira inakusuta hastahili vitu vya kawaida. Kama ni gari basi liwe gari kweli, kama ni nguo basi ni nguo kweli n.k. Hata kama binti wa watu hana makuu na hahitaji mambo "makubwa" wewe lazima presha iwe juu.
 
Tatizo sio wanaume, tatizo ni hao wanawake wanaojiona/wanaodhani/waliombiwa kuwa ni wazuri kudhani kwamba uzuri wake ni kila kitu kwenye mahusiano.
Mwisho wa siku maisha ya mahusiano ni zaidi ya uzuri wako/muonekano wako.

1. Anaweza kuwa na sura nzuri,umbo zuri lakini akawa na kasoro nyingine kubwa huko ndani, wanaume tuliowahi kuwa na wanawake wazuri na tulionao mpaka sasa tunajua hili. ...etc

2. Wapo wanawake wazuri kwa sura na umbo na wanaelewa mahusiano na wanaolewa na kuheshimu ndoa zao

3. Wapo wanawake wanaodhaniwa kuwa ni wabaya lakini wanajua namna ya kuishi vyema katika mahusiano hivyo kuwavutia wanaume.

4. Wapo wanawake wanaodhaniwa kuwa ni wabaya kwa sura na umbo lakini wana mambo matamu kwenye baadhi ya maeneo.

Note: tafsiri zetu za uzuri na ubaya hazifani.

Mwanamke anaweza kuonekana mbaya kwako kwa mwingine akawa malkia au akaonekana mzuri kwako na mwingine akaona wa kawaida tu.
 
Tupe mfano hai nani kamuoa nani ambaye we unadhani sio mzuri.
 
Sio wew tu ndo umeona mim mwenywe nimeona hilo wengi wanawakimbiaga huwa wanajikutaga machino kichizi alafu wengi huwa ni Money Spenders wafujaji wakutupwa alafu ukiondoko nyumbani unakuwa roho mkno hivi watamuacha kwelii na uzri alionao lol shida kama hhiyo wengi wanaepuka
 
Mbona wanaolewa sana uswazi kwetu. Muonekano mzuri na sura nzuri ni relative. Kuna utofauti wa uzuri na gharama.Sio kila mwenye kuwa na nywele za gharama kichwani anavutia au ataonekana mzuri
 
Habari zenu wanajamii forum,

Kuna jambo ambalo nalishanagaa kidogo japo sina uhakika asilimia 100 but kwa utafiti nilikokafanya kidogo tu nimegundua wale wanawake wazuri na wenye sura na muonekano mzuri wanatafuta sana watu wa kuwaoa lakini watu wote wanawakimbia, sijui ni kwanini na mara nyingi sasa hivi wale wa kina dada wenye muonekana wa kawaida kisura ndio wanaolewa.

Ili kulithibitisha hilo kuna dada mmoja mzuri sana aliniambia anataka mtu wa kumuona ila kila mwanaume anasema hawezi kuoa presha sasa sijui wanaume wenzangu kunani ni kweli uzuri wao unawatisha au kunanini nyuma ya pazia jamani wengi wanataka kuolewa lakini wanaume wanataka kuwatumia tu kuwaacha.

Jamani tujadili kuhusu hili

....wazee wa zamani walisema kuchapiwa ni siri ya ndani.....NAIMBA TU....
 
Back
Top Bottom