Hii hoja kuna baadhi ya watu wake kwa waume wanairukia pasipo kuielewa. Kabla ya kuwajadili feminist kwa maana wafuasi wa hicho kitu ni vyema tukajadili kitu chenyewe ni nini, ambacho ni feminism.
Feminism wanasema kwa urahisi ni jinsia zote zinahitaji haki sawa na fursa (ambazo zimo kwenye jamii). Itikadi yao ni kuwa maadamu wote ni binadamu basi mwanaume na mwanamke ni sawa. Kwa maana hiyo wanawake wanahitaji haki sawa ndani ya jamii kama mwanaume.
Wanachoshindwa kufahamu ni kwamba mwanaume na mwanamke ni sawa kwa hali ya ukiumbe! Kwa maana wote ni binadamu. Lakini hawa binadamu wana utofauti wa kimaumbile, nguvu, ujasiri, nidhamu za kibailojia, kufikiri n.k na tunaishi kwenye jamii ambayo inatubidi tuwajibike.
Kwa muktadha wa namna huu kwa kutofautiana huku ni lazima kutakuwa na mgawanyo wa majukumu kwenye kuyaendea mambo kuwajibika kwenye jamii. Mambo mengine yanatokana na kanuni na nidhamu za kimaumbile (nature) mfano mwanamke anapenda kupika na majukumu mengine ambayo yanafahamika mwanamke anayoyafanya. Halikadhalika kwa mwanaume.
Feminist wanachokitaka ni usawa lakini usawa wao hawauhitaji kwenye majukumu. Mathalani kwa hapa Tz mwanamke anayedai usawa akiambiwa naye ahudumie familia kwa hali na mali kama mwanaume anavyojitoa kutoka kwenye pato lake hawakubali. Ukienda Uk wanataka walipwe mshahara mmoja na mwanaume wakati kwenye kitengo hicho hicho mwanaume anafanya kazi ya ziada ambayo inamlazimu atumie nguvu za mwili wake pia ukiacha taaluma.
Ni sawa sawa kusema Simba,Chui, Swala, Mbuzi, Duma, Paa wote wapewe majukumu sawa! Jawabu kwa vile wote ni wanyama. Huku ni kujibu kwa kuona na si kwa kutumia akili.
Ukiangalia kote feminists wanapigania ubinafsi na si haki sawa! Wafahamumwanamke na mwanaume si sawa kwa maana ya kimajukumu. Ni vyema wapiganie unyanyasaji wa kijinsia. Ila suala la haki sawalikiwekwa watakaopata madhara makubwa ni wao. Wanapigania kitu ambacho hawafahamu uhalisiya wake.
Moja ya athari hasi ya feminists hawana nidhamu. Si nidhamu ya kuongea ki kauli wala kuandika kimaandishi. Hawajali hisiya za mtu aliye tofauti na mtizamo wao ila wanataka hisiya zao zijaliwe.