Mchokoo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2015
- 1,188
- 1,604
Ndugu zangu Watanzania hakuna binadamu asiyekosea, iwe ni kwa makusudi au bahati mbaya. Kimsingi hilo ndilo hudhihirisha ubinadamu wenyewe. lngawa mara nyingi tunapogundua makosa yetu tunajaribu kutoyakubali kama ni makosa!
Au tukikubali tunaona shida sana kuomba msamaha, tukidhani kuonekana ni dhaifu, kitu ambacho siyo kweli. Kimsingi mtu anayekubali kuwa amemkosea Mungu, au wanadamu wenzake ni nguzo ya shaba katikati ya kizazi cha waoga.
Hivyo basi naisihi serikali katika hili la mkataba wa bandari; ikubali kuomba radhi. Mkifanya hivyo hamtaonekana wadhaifu, bali wakomavu sana.
Msituangushe hata wale tunaowanga mkono tangu Mungu awaweke madarakani. Kwani ukitazama kwa makini sana ni kama hili limekuja kufuta mema yote yaliyofanywa na awamu hii.
Sasa kwa nini iwe hivyo, na kwa faida ya nani?
Au tukikubali tunaona shida sana kuomba msamaha, tukidhani kuonekana ni dhaifu, kitu ambacho siyo kweli. Kimsingi mtu anayekubali kuwa amemkosea Mungu, au wanadamu wenzake ni nguzo ya shaba katikati ya kizazi cha waoga.
Hivyo basi naisihi serikali katika hili la mkataba wa bandari; ikubali kuomba radhi. Mkifanya hivyo hamtaonekana wadhaifu, bali wakomavu sana.
Msituangushe hata wale tunaowanga mkono tangu Mungu awaweke madarakani. Kwani ukitazama kwa makini sana ni kama hili limekuja kufuta mema yote yaliyofanywa na awamu hii.
Sasa kwa nini iwe hivyo, na kwa faida ya nani?