Kwamba Serikali ya Tanzania haiwafahamu wenye nyumba kiasi cha kumkata mpangaji kodi ya Majengo ni uongo wa kiwango cha chini sana na ni wizi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,674
218,183
Kodi ya Majengo imelipwa ndani ya nchi hii kwa miaka na miaka , kwa kipindi kirefu ililipwa kwenye Halmashauri na kuwa mapato ya Halmashauri husika ili kusaidia miradi mbali mbali , mimi mwenyewe nina nyumba 2 kwenye halmashauri ya Temeke , nafahamu ninachoandika , Jina langu linafahamika vema kabisa na Halmashauri hiyo kama wenye nyumba wengine wanavyofahamika , huku kila jengo au nyumba ikirasimishwa kwa kupewa namba Maalum na kubandikwa Ukutani ili kila mtu aone .

Baada ya uchaguzi Mkuu wa 2015 ccm kuangushwa kwa kunyang'anywa halmashauri kubwa kubwa , ikiwemo Halmashauri ya Jiji la DSM , yenye majengo mengi na yenye kulipiwa pesa nyingi , kwa roho yake Mbaya , Rais wa wakati huo Magufuli akaamua kuzinyang'anya kodi ya majengo halmashauri kwa vile sasa zilikuwa chini ya Chadema , na kuamuru wenye majengo wote nikiwemo mimi kulipia kodi hiyo kupitia TRA , rekodi zote zipo na wenye nyumba wote wapo na wanatambulika na tayari walishawekwa kwenye mfumo wa malipo ( japo baada ya uchafuzi wa 2020 kodi hii imerejeshwa tena halmashauri maana chadema hawapo tena ), sasa kuwalipisha watu wasiohusika huku wahusika wanaopaswa kulipa kodi wapo na wanafahamika ni wizi wa kishamba sana uliolenga kutunisha mfuko wa serikali kwa NJIA YA HARAMU .

Kama walipaji walishakuwa kwenye mfumo na wanafahamika , huku kila nyumba mpya inayojengwa ujenzi wake hufanywa baada ya vibali vya halmashauri , kwanini Serikali imeamua kupora pesa za raia wasiohusika ?

Itaendelea ....
 
Kodi ya Majengo imelipwa ndani ya nchi hii kwa miaka na miaka , kwa kipindi kirefu ililipwa kwenye Halmashauri na kuwa mapato ya Halmashauri husika ili kusaidia miradi mbali mbali , mimi mwenyewe nina nyumba 2 kwenye halmashauri ya Temeke , nafahamu ninachoandika , Jina langu linafahamika vema kabisa na Halmashauri hiyo kama wenye nyumba wengine wanavyofahamika , huku kila jengo au nyumba ikirasimishwa kwa kupewa namba Maalum na kubandikwa Ukutani ili kila mtu aone .

Baada ya uchaguzi Mkuu wa 2015 ccm kuangushwa kwa kunyang'anywa halmashauri kubwa kubwa , ikiwemo Halmashauri ya Jiji la DSM , yenye majengo mengi na yenye kulipiwa pesa nyingi , kwa roho yake Mbaya , Rais wa wakati huo Magufuli akaamua kuzinyang'anya kodi ya majengo halmashauri kwa vile sasa zilikuwa chini ya Chadema , na kuamuru wenye majengo wote nikiwemo mimi kulipia kodi hiyo kupitia TRA , rekodi zote zipo na wenye nyumba wote wapo na wanatambulika na tayari walishawekwa kwenye mfumo wa malipo ( japo baada ya uchafuzi wa 2020 kodi hii imerejeshwa tena halmashauri maana chadema hawapo tena ), sasa kuwalipisha watu wasiohusika huku wahusika wanaopaswa kulipa kodi wapo na wanafahamika ni wizi wa kishamba sana uliolenga kutunisha mfuko wa serikali kwa NJIA YA HARAMU .

Kama walipaji walishakuwa kwenye mfumo na wanafahamika , huku kila nyumba mpya inayojengwa ujenzi wake hufanywa baada ya vibali vya halmashauri , kwanini Serikali imeamua kupora pesa za raia wasiohusika ?
Hivi kweli unaandika kwa kutoa povu kabisa kuwa kila nyumba inayojengwa Tanzania serikali inaijua na imeipa kibali cha ujenzi? Eti hii ndiyo msingi wa hoja yako kuwa serikali inawafahamu wenye nyumba wote Tanzania!! Ndiyo tatizo la kushikiwa akili na watu kama Lema na Lissu. Sijui Chadema mnafeli wapi
 
Hhivi kweli unaandika kwa kutoa povu kabisa kuwa kila nyumba inayojengwa Tanzania serikali inaijua na imeipa kibali cha ujenzi? Hati hii ndiyo msingi wa hoja yako kuwa serikali inawafahamu wenye nyumba wote Tanzania!! Ndiyo tatizo la kushikiwa akili na watu kama Lema na Lissu. Sijui Chadema mnafeli wapi
unabisha nini ?
 
Hebu tulipe hii kodi jamani! Imekuwapo muda mrefu tumekuwa tukilipa na wengine wakikwepa kulipa! Hivi mwenye nyumba ambaye hanunui umeme kwenye nyumba uliyopanga watampata wapi? Dawa ni hiyo wewe unayenunua umeme ukatwe na wewe utamkata mwenye nyumba wakati wa kulipa kodi yake! Chukulia kwa mfano unalipa kodi kwa miezi 6 kuna ugumu gani wewe kumkata shilingi elfu 6 ya kodi ya jengo? Tulipe kodi! Katika hili niko upande wa mama!
 
Serikali imekuwa ikitamka wazi kuwa ni asilimia 25 tu ya eneo la Tanzania ndilo limepimwa. Maana take zaidi ya 75% ya nyumba zote zimejengwa maeneo yasiyopimwa, ujenzi wake unafanyika bila vibali na hivyo hazitambuliwi rasmi kwenye data za ardhi. Acha upotoshaji.
kwahiyo kwa vile 75% hawajarasimishwa basi ndio tuwapore wengine !
 
Serikali imekuwa ikitamka wazi kuwa ni asilimia 25 tu ya eneo la Tanzania ndilo limepimwa. Maana take zaidi ya 75% ya nyumba zote zimejengwa maeneo yasiyopimwa, ujenzi wake unafanyika bila vibali na hivyo hazitambuliwi rasmi kwenye data za ardhi. Acha upotoshaji.
Wewe ndo huelewi kitu.. hizo nyumba zipo kwenye mahandaki?

Kwa hiyo unashindwa hata kuwaza namna gani zikatambuliwa.

TRA walishafanya hilo zoezi..labda kama nao waliishia kuacha kwenye makaratasi.

Hii inji ni kama wote tunajifunza kila kitu.
 
Hebu tulipe hii kodi jamani! Imekuwapo muda mrefu tumekuwa tukilipa na wengine wakikwepa kulipa! Hivi mwenye nyumba ambaye hanunui umeme kwenye nyumba uliyopanga watampata wapi? Dawa ni hiyo wewe unayenunua umeme ukatwe na wewe utamkata mwenye nyumba wakati wa kulipa kodi yake! Chukulia kwa mfano unalipa kodi kwa miezi 6 kuna ugumu gani wewe kumkata shilingi elfu 6 ya kodi ya jengo? Tulipe kodi! Katika hili niko upande wa mama!
nyumba yenye mita 6 tunafanyaje , na hii inakatwa bei gani ?
 
TRA jana wamelitolea maelezo hilo jambo kwamba wenye nyumba zenye mita zaidi ya moja waende TRA kusema ni mita gani iwe inakatwa kodi ya jengo ili kuondoa huo mkanganyiko.
Nani atakwenda ? kwanini hili lisingefanyika kabla ya makato kuanza ?
 
nyumba yenye mita 6 tunafanyaje , na hii inakatwa bei gani ?
Hili limeshatolewa ufafanuzi, kwamba mwenye nyumba aende na hizo taarifa za mita zote TRA ili akabainishe ni mita ipi itakuwa inatozwa kodi ya jengo! Tuache kubisha tu ili tuonekane tunajua kubisha. Kodi ya nyumba ni halali, tulipe jamani, tumekwepa sana hii kodi!
 
TRA jana wamelitolea maelezo hilo jambo kwamba wenye nyumba zenye mita zaidi ya moja waende TRA kusema ni mita gani iwe inakatwa kodi ya jengo ili kuondoa huo mkanganyiko.
Ko kwa wale wa flame au office za NHC tunaenda au NHC wanakuwa washaenda, na hayo majumba ya mashirika wanataka walipa umeme ndo walipe kodi za majumba yao
 
Au mfano unanyumba ambayo umepangisha watu, umo kila mpangaji ana mita yake, so kila mpangaji analipa ama, mana kusema umuhamishie mpangaji moja majukum ni kuleta mtafarakano
 
Hili limeshatolewa ufafanuzi, kwamba mwenye nyumba aende na hizo taarifa za mita zote TRA ili akabainishe ni mita ipi itakuwa inatozwa kodi ya jengo! Tuache kubisha tu ili tuonekane tunajua kubisha. Kodi ya nyumba ni halali, tulipe jamani, tumekwepa sana hii kodi!
Asipoenda mnamfanyaje na je kwanini wenye nyumba wasiitwe mapema kabla ya wizi kufanyika ?
 
Back
Top Bottom