Kwa wenye magari binafsi piteni hapa

Mkuu, tatizo hapa unaona lifti Dar tu; Tz ni kubwa. Sehemu zingine ukitoa lifti bila kuombwa watu hawakuelewi.

Nina ushahidi, siku moja nilitoka West Kilimanjaro Moshi kuelekea mjini nikiwa peke yangu kwenye Noah, nikawakuta akinamama wawili wako kituo fulani nikasimama kuwasaidia kutokana na usafiri ulivyokuwa shida siku hiyo. Nilivyoshusha kioo wakaona ndani ya gari hakuna abiria hata mmoja waligeuka mbio wala hawakunisemesha.

Unaweza kudhani washamba lakini baadhi ya maeneo kama huko nasikia watu wana itikadi kuwa kuna kafara hutolewa Mirerani!
 
Weeee naye kama ndio umekuja leo?????? Wakati ni pacha wangu!!!!
Aaargh mwisho utashangaa tembo mkubwa anazama samaki ndama anaogelea!!!!!!

Changamukaaaaa!!!!!
hahahahaha
kumbe napitwa itabidi nije kwenye hiyo sensa chap chap sana lol
 
Uchunguzi ulobandika hapa ndo umekupa PhD? Basi hii yako haina tofauti na ile ya Dr Bana! Hv BRN ipo hadi kwenye PhD?
 
yaani gari yangu imetoka kuoshwa 5min ago,na hizi mvua za dar nimpe mtu lift na matope yake na jinsi alivyoloa,na ki vitz changu kilivyo chini hivyo ukilinganisha na mabonde ya hapa riverside kibangu, weweeeeee hiyo haipo,mleta mada nashawishika kukuita mlevi

Tatizo hicho kigari hakijatengenezwa kwa matumizi yako..Huo ni ubakaji
 
Inshu ni kwamba, watz tujitambue.... kwamba hakuna maana yoyote wewe kutoka Kimara kwenda posta ukiwa pekeyako kweye gari yenye uwezo wakubeba watu wa4。Huu nauita Ubinafsi. Ili uwasaidie wenzako na upunguze matumizi yako (mafuta na matengenezo) ni bora upande public bus.kufanya hivyo utakuwa umesaidia kupunguza folen zisizo za lazima hapa mjin nakuwafanya wasio na usafiri binafsi wawahi wanapokwenda.
Mi nashauri itungwe sheria ndogo ya jiji kuwadhibiti watu wenye usafiri binafsi kuingia katikati ya jiji...
Ni maoni sio kesi wadau....
 
Tatizo mimi huwa wanapanda akina dada tu, halafu wanaishia kunisumbua kwenye Simu. Mara ooghh ushatoka kazini au ushatoka home? Usichelewe Niko kituoni nakusubiri.....
 
Inshu ni kwamba, watz tujitambue.... kwamba hakuna maana yoyote wewe kutoka Kimara kwenda posta ukiwa pekeyako kweye gari yenye uwezo wakubeba watu wa4。Huu nauita Ubinafsi. Ili uwasaidie wenzako na upunguze matumizi yako (mafuta na matengenezo) ni bora upande public bus.kufanya hivyo utakuwa umesaidia kupunguza folen zisizo za lazima hapa mjin nakuwafanya wasio na usafiri binafsi wawahi wanapokwenda.
Mi nashauri itungwe sheria ndogo ya jiji kuwadhibiti watu wenye usafiri binafsi kuingia katikati ya jiji...
Ni maoni sio kesi wadau....

wewe naye mtu wa ajabu sanaaa! gari ninunue mimi na ushuru nilipie mimi na kodi ndg ndg nilipue mimi alafu nilazimishwe kuwapa watu luft hakuna kitu kama hicho, kwanza kiusalama hutakiwi umpandishe mtu usiye mjue wewe unaweza ukapataa balaaa ambayo hujaitegemea.....fikirini kabla ya kuamuaa jambo
 
Uzuri wa gari km uko man alone umkute mtoto mzuriiiii then umpe lift, hapo ht safari huwa ni tamu sana
 
Natoka tunduma nipo chalinze nataka niingie posta na SEMI TREILA vp inawezekana? wakuu nijulisheni haraka.
 
Back
Top Bottom