Usedcountrynewpipo
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,636
- 2,734
Wao hela zao wamejengea nyumba. Wanatupangisha na kodi tunawalipa alafu magari yetu ndio wapande buree eeh? Nyooo!
Ningekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ingekuwa ni marufuku kwa mtu yeyote yule kuendesha gari yoyote ile akiwa peke yake ndani ya gari.
Haiwezekani mtu atoke posta akiwa kwenye gari yenye siti nne na nyingine zina siti sita halafu mtu yupo peke yake wakati kuna watu wanasubiri daladala masaa mawili mpaka matatu.
Najua ni gari yako, ulinunua kwa pesa zako na hakuna aliyekuchangia ila kwa hilo mngeniona mchungu.
Najua nitakuwa navunja sheria ila nisingewaacha. Ukaguzi wa magari hayo private kwa watu wanaotoka posta na kariakoo ungekuwa unafanyikia Jangwani kwa wanaenda Ubungo, Ubalozi wa Ufaransa kwa wanaoenda Mwenge, kurasini kwa wanaoenda mbagala na temeke, UKIKUTWA UPO PEKE YAKO KWENYE GARI UNARUDISHWA POSTA KUBEBA WATU.
____________
UPDATE: Kama kumpa mtu lift unaogopa usalama wako basi hata gari ikikusumbua usiwaombe watu wakusukume maana huwajui hivyo itahatarisha usalama wako.
Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)
wewe naye mtu wa ajabu sanaaa! gari ninunue mimi na ushuru nilipie mimi na kodi ndg ndg nilipue mimi alafu nilazimishwe kuwapa watu luft hakuna kitu kama hicho, kwanza kiusalama hutakiwi umpandishe mtu usiye mjue wewe unaweza ukapataa balaaa ambayo hujaitegemea.....fikirini kabla ya kuamuaa jambo
Natoka tunduma nipo chalinze nataka niingie posta na SEMI TREILA vp inawezekana? wakuu nijulisheni haraka.
Suala si kutoa lift, suala ni wew kuchangia kusababisha folen isiyo ya lazima mjini kwa wewe kutembea pekeyako na gari kumbe ungetumia public transport ungesaidia na wasio na magari kuwahi waendako kwa kupunguza msongamano wa magari na wewe kusave fedha ambazo ungetumia kwa mafuta na matengenezo ya gari. Tumia gari lako pale inapobidi kufanya hivyo tu na sio wote wapandao usafiri wa umma hawana magari....
Ni ushauri tu...
Phd = pengine huna degree..