Mafao ya Viongozi: Mwenza wa Rais Mstaafu kulipwa 60% ya Mshahara wa Rais kwa maisha yake yote

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
MABADILIKO YA SHERIA YA MAFAO YA VIONGOZI NA FAMILIA ZAO:

Jina la sheria - THE POLITICAL SERVICE RETIREMENT BENEFITS ACT, (CAP. 225)

"THREAD"

BADILIKO 1:

Ongezeko la kifungu kipya cha 9A ambacho hakipo kwenye sheria kinachotaja mafao ya mke/mume wa rais mstaafu. Baada ya rais kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa rais alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Yaani, kama rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 3B, basi mwenza wake atalipwa TZS 750M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo.

BADILIKO 2:

Kwenye kifungu cha 11 kinachohusu mafao ya mjane wa rais mstaafu (survivor's pension) ambapo kwa sasa kila mwezi mjane hulipwa 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani. Asilimia imeongezwa na sasa mjane atalipwa 60%. Mfano kama rais anapokea TZS 30M kwa mwezi, basi mjane wa rais atalipwa TZS 18M kila mwezi.

BADILIKO 3:

Ongezeko la kifungu kipya cha 12A ambacho hakipo kwenye sheria kinachotaja mafao ya mke/mume wa makamu wa rais mstaafu. Baada ya makamu wa rais kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa makamu wa rais alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Yaani, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 2B, basi mwenza wake atalipwa TZS 500M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo.

BADILIKO 4:

Kufutwa kwa kifungu cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), mwenza wake, atalipwa (survivor's pension) sawa na 40% ya mshahara wa makamu wa rais aliye madarakani, na stahiki nyingine zilizoelezwa kwenye jedwali la sheria hiyo, ikiwemo nyumba, matibabu na mengine mengi. (kifungu hiki kimefutwa).

Kifungu kipya cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), wategemezi wake (dependants) watalipwa kiasi cha fedha sawa na mshahara wote wa makamu wa rais alioupokea wakati akiwa madarakani. Mfano, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa TZS 2B kama mshahara, basi wategemezi wake watalipwa kiasi hiko cha TZS 2B kama pension. Ifahamike, kwa mujibu wa sheria hii, neno "dependants" limefafanuliwa kwenye kifungu cha 4, na maana yake ni mke au wake, mume, watoto (ambao walikuwa ni tegemezi kwa marehemu), pamoja na wazazi wa marehemu (wategemezi).

Pia, mke wa marehemu (makamu wa rais) atalipwa fedha (survivor's pension) kila mwezi sawa na 40% ya mshahara wa wa makamu wa rais aliye madarakani kwa sasa. Pia, atapata stahiki nyingine zilizotajwa kwenye jedwali la sheria hii.

BADILIKO 5:

Kifungu cha 14 kimeongezwa kifungu kidogo cha "4" kinachotoa haki ya "msaidizi wa kazi" mmoja kwa mtu aliyewahi kuwa Waziri Mkuu kabla ya sheria hii kutungwa. Hapa tunazungumzia Mawaziri wakuu wastaafu wakati wa Mwalimu.

BADILIKO 6:

Ongezeko la kifungu kipya cha 14A ambacho hakipo kwenye sheria ya sasa> Kifungu hiki kinataja mafao ya mke/mume wa Waziri Mkuu mstaafu. Baada ya Waziri Mkuu kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa Waziri Mkuu alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Mfano, kama Waziri Mkuu ameshika madaraka kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 1B, basi mwenza wake atalipwa TZS 250M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo (lump sum).

BADILIKO 7:

Kifungu cha 15(2) kimefanyiwa nyongeza ya neno "granted monthly", ambapo kwa sheria ya sasa, kifungu hiki kinamtaja mjane wa Waziri Mkuu kupokea kiasi cha fedha 40% ya mshahara wa Waziri Mkuu aliye madarakani. Kilichoongezeka ni kwamba, hiki kiasi atakuwa analipwa KILA MWEZI.

BADILIKO 8:

Kifungu cha 18(2) kimefanyiwa nyongeza ya neno "granted monthly", ambapo kwa sheria ya sasa, kifungu hiki kinamtaja mjane wa Spika wa Bunge kupokea kiasi cha fedha 40% ya mshahara wa Spika aliye madarakani kwa sasa. Kilichoongezeka ni kwamba, hiki kiasi atakuwa analipwa KILA MWEZI.

BADILIKO 9:

Badiliko la JEDWALI la sheria hii linalotaja nyongeza ya mafao ya viongozi.

1. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka magari 2, sasa atapata magari 3 yasiyopungua uzito wa tani 3 (yaani hawezi pewa Corola, bali ni gari kubwa kama V8 n.k, ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

2. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 2 na sasa atapewa 3.

3. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

4. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

5. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

6. Makamu wa Rais atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

7. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Makamu wa Rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama Makamu wa Rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

8. Makamu wa Rais atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

9. Waziri Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

10. Warizi Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

11. Waziri Mkuu mstaafu atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

12. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Waziri Mkuu mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake atakapofariki.

13. Waziri Mkuu atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

14. Mjane wa Rais mstaafu, kwa sheria ya sasa anapata 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani kila mwezi kama "maintenance allowance", asilimia hii imepanda sasa atalipwa 60%.

15. Sheria ya sasa inatoa gharama za matibabu kwa mjane wa Rais mstaafu kwenye hospitali za ndani ya nchi tu, lakini badiliko la sheria mpya, atalipiwa na Serikali matibabu ya hospitali za nje ya nchi pia.

16. Mjane wa Rais mstaafu ameongezewa huduma za gari toka gari moja mpaka magari mawili, na dereva 2 kufanya shughuli zake za kila siku. Serikali inalipia gharama za mafuta pia. Magari haya yatakuwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5. Pia, ameongezewa mpishi, mfua nguo na mtunza bustani. Atapata ulinzi wa TISS.

17. Mjane wa Makamu wa Rais, anapata stahiki kama za mjane wa rais isipokuwa tofauti yake ni moja, yeye atapata gari moja la Serikali na dereva mmoja.

18. Mjane wa Waziri Mkuu mstaafu anapata stahiki za ziada kama mjane wa Makamu wa Rais, isipokuwa gari analotumia la Serikali litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka 7.

19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.

20. Hii ni nyongeza kwa Spika wa Bunge kwenye mafao yake: gari moja, Bima ya Afya yake binafsi, matumizi ya VIP lounge, pia anapata stahiki nyingine kama LITA 70 za mafuta kwa wiki

NB:
Sheria hii imefanyiwa MABADIRIKO kwa kile kilichoitwa "MABORESHO" na Rais SSH wakati anatoa maagizo kwa aliyekuwa Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akikabidhi nyumba mpya kwa Rais mstaafu JK.
 
MABADILIKO YA SHERIA YA MAFAO YA VIONGOZI NA FAMILIA ZAO:

Jina la sheria - THE POLITICAL SERVICE RETIREMENT BENEFITS ACT, (CAP. 225)

"THREAD"


Sheria hii imefanyiwa MABADIRIKO kwa kile kilichoitwa "MABORESHO" na Rais SSH wakati anatoa maagizo kwa aliyekuwa Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akikabidhi nyumba mpya kwa Rais mstaafu JK.


Hao sio wa kwanza kuanza haya mambo Africa, wanaandaa maanguko yao.
 
19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.
Mimi nina swali hapa, je hiki kipengele cha Waziri na Naibu Waziri

Ni waziri mkuu na naibu wake?, au Ni kwa mawaziri na naibu waziri wote waliowahi kushika nafasi tangu kuasisiwa kwa taifa hili, na je ni visiwani na bara? Au wao visiwani wana utaratibu wao
 
Wacha watu wale. Wakivimbiwa watarudi...😭😭😭😭

Tuzidi kuliombea taifa litoke mikononi mwa majambazi 😭🙏
 
Duh, basi yafaa pia ukiwa Rais, makamu wa rais, Waziri mkuu, spika wa bunge pamoja na wajane au wagane ama wake na waume zake mtangaze mali zenu kabla hamjaingia madarakani kama sheria inavyotaka vinginevyo ni kukaribisha anguko lenu na taifa kwa ujumla. SIUNGI MKONO HUU UPUMBAVU HATA KIDOGO.

viongozi wanaongezeka kila siku na mahitaji yao yatabebwa na masikini kila siku du. Familia za marais zipo sita, zitahitaji magari 18, wapishi 6, madereva 18 watunza bustani 6, madobi 6, walinzi 12 nyumba za kifahari 6 diplomat pasport kwa mke na mume kwa gharama za walala hoi plus monthly allowance isiyopungua milioni 30 (YES MAKE FAMILIA YA MWINYI, KIKWETE NA SAMIA wote mme na mke watalipwa huku MAGUFULI, NYERERE NA MKAPA familia zao zikipotea monthy alowance na lump sum ya wazee wao kupitia kwa mama[hii ni tofauti na mafao ya mzee] tuelewane hapa ) kila famili. Gharama za mafuta ya magari matatu pamoja na service za gari zote 3. Bado familia za makamu wa rais, waziri mkuu NW mkuu, spika wa bunge, na jaji mkuu. WTF
 
Watu maskini huwa walafi sana... licha ya yfisadi alioufanya yeye na mmewe, mafao anayopokea bado anang'ang'ana na ubunge huku mtoto wao akiwa Naibu Waziri!!

Waswahili ni walafi hadi wanatia kinyaa!

IMG_4146.jpg
 
MABADILIKO YA SHERIA YA MAFAO YA VIONGOZI NA FAMILIA ZAO:

Jina la sheria - THE POLITICAL SERVICE RETIREMENT BENEFITS ACT, (CAP. 225)

"THREAD"

BADILIKO 1:

Ongezeko la kifungu kipya cha 9A ambacho hakipo kwenye sheria kinachotaja mafao ya mke/mume wa rais mstaafu. Baada ya rais kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa rais alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Yaani, kama rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 3B, basi mwenza wake atalipwa TZS 750M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo.

BADILIKO 2:

Kwenye kifungu cha 11 kinachohusu mafao ya mjane wa rais mstaafu (survivor's pension) ambapo kwa sasa kila mwezi mjane hulipwa 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani. Asilimia imeongezwa na sasa mjane atalipwa 60%. Mfano kama rais anapokea TZS 30M kwa mwezi, basi mjane wa rais atalipwa TZS 18M kila mwezi.

BADILIKO 3:

Ongezeko la kifungu kipya cha 12A ambacho hakipo kwenye sheria kinachotaja mafao ya mke/mume wa makamu wa rais mstaafu. Baada ya makamu wa rais kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa makamu wa rais alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Yaani, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 2B, basi mwenza wake atalipwa TZS 500M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo.

BADILIKO 4:

Kufutwa kwa kifungu cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), mwenza wake, atalipwa (survivor's pension) sawa na 40% ya mshahara wa makamu wa rais aliye madarakani, na stahiki nyingine zilizoelezwa kwenye jedwali la sheria hiyo, ikiwemo nyumba, matibabu na mengine mengi. (kifungu hiki kimefutwa).

Kifungu kipya cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), wategemezi wake (dependants) watalipwa kiasi cha fedha sawa na mshahara wote wa makamu wa rais alioupokea wakati akiwa madarakani. Mfano, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa TZS 2B kama mshahara, basi wategemezi wake watalipwa kiasi hiko cha TZS 2B kama pension. Ifahamike, kwa mujibu wa sheria hii, neno "dependants" limefafanuliwa kwenye kifungu cha 4, na maana yake ni mke au wake, mume, watoto (ambao walikuwa ni tegemezi kwa marehemu), pamoja na wazazi wa marehemu (wategemezi).

Pia, mke wa marehemu (makamu wa rais) atalipwa fedha (survivor's pension) kila mwezi sawa na 40% ya mshahara wa wa makamu wa rais aliye madarakani kwa sasa. Pia, atapata stahiki nyingine zilizotajwa kwenye jedwali la sheria hii.

BADILIKO 5:

Kifungu cha 14 kimeongezwa kifungu kidogo cha "4" kinachotoa haki ya "msaidizi wa kazi" mmoja kwa mtu aliyewahi kuwa Waziri Mkuu kabla ya sheria hii kutungwa. Hapa tunazungumzia Mawaziri wakuu wastaafu wakati wa Mwalimu.

BADILIKO 6:

Ongezeko la kifungu kipya cha 14A ambacho hakipo kwenye sheria ya sasa> Kifungu hiki kinataja mafao ya mke/mume wa Waziri Mkuu mstaafu. Baada ya Waziri Mkuu kustaafu, mwenza/wenza wake atapokea kiasi cha fedha (kwa mkupuo) sawa na 25% ya mshahara wa Waziri Mkuu alioupokea katika kipindi chote alichokuwa madarakani. Mfano, kama Waziri Mkuu ameshika madaraka kwa miaka 10, akalipwa mshahara wa TZS 1B, basi mwenza wake atalipwa TZS 250M, fedha ambayo inalipwa kwa mkupuo (lump sum).

BADILIKO 7:

Kifungu cha 15(2) kimefanyiwa nyongeza ya neno "granted monthly", ambapo kwa sheria ya sasa, kifungu hiki kinamtaja mjane wa Waziri Mkuu kupokea kiasi cha fedha 40% ya mshahara wa Waziri Mkuu aliye madarakani. Kilichoongezeka ni kwamba, hiki kiasi atakuwa analipwa KILA MWEZI.

BADILIKO 8:

Kifungu cha 18(2) kimefanyiwa nyongeza ya neno "granted monthly", ambapo kwa sheria ya sasa, kifungu hiki kinamtaja mjane wa Spika wa Bunge kupokea kiasi cha fedha 40% ya mshahara wa Spika aliye madarakani kwa sasa. Kilichoongezeka ni kwamba, hiki kiasi atakuwa analipwa KILA MWEZI.

BADILIKO 9:

Badiliko la JEDWALI la sheria hii linalotaja nyongeza ya mafao ya viongozi.

1. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka magari 2, sasa atapata magari 3 yasiyopungua uzito wa tani 3 (yaani hawezi pewa Corola, bali ni gari kubwa kama V8 n.k, ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

2. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 2 na sasa atapewa 3.

3. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

4. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

5. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

6. Makamu wa Rais atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

7. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Makamu wa Rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama Makamu wa Rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

8. Makamu wa Rais atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

9. Waziri Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

10. Warizi Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

11. Waziri Mkuu mstaafu atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

12. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Waziri Mkuu mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake atakapofariki.

13. Waziri Mkuu atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

14. Mjane wa Rais mstaafu, kwa sheria ya sasa anapata 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani kila mwezi kama "maintenance allowance", asilimia hii imepanda sasa atalipwa 60%.

15. Sheria ya sasa inatoa gharama za matibabu kwa mjane wa Rais mstaafu kwenye hospitali za ndani ya nchi tu, lakini badiliko la sheria mpya, atalipiwa na Serikali matibabu ya hospitali za nje ya nchi pia.

16. Mjane wa Rais mstaafu ameongezewa huduma za gari toka gari moja mpaka magari mawili, na dereva 2 kufanya shughuli zake za kila siku. Serikali inalipia gharama za mafuta pia. Magari haya yatakuwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5. Pia, ameongezewa mpishi, mfua nguo na mtunza bustani. Atapata ulinzi wa TISS.

17. Mjane wa Makamu wa Rais, anapata stahiki kama za mjane wa rais isipokuwa tofauti yake ni moja, yeye atapata gari moja la Serikali na dereva mmoja.

18. Mjane wa Waziri Mkuu mstaafu anapata stahiki za ziada kama mjane wa Makamu wa Rais, isipokuwa gari analotumia la Serikali litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka 7.

19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.

20. Hii ni nyongeza kwa Spika wa Bunge kwenye mafao yake: gari moja, Bima ya Afya yake binafsi, matumizi ya VIP lounge, pia anapata stahiki nyingine kama LITA 70 za mafuta kwa wiki

NB:
Sheria hii imefanyiwa MABADIRIKO kwa kile kilichoitwa "MABORESHO" na Rais SSH wakati anatoa maagizo kwa aliyekuwa Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akikabidhi nyumba mpya kwa Rais mstaafu JK.
Mbona sasa mapato yoote ya Bandari, Madini, na mapato Yoote ya Utalii yataishia kwao??

😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆
Ndio maana wanachapana wakati wa Uchaguzi
 
Duh, basi yafaa pia ukiwa Rais, makamu wa rais, Waziri mkuu, spika wa bunge pamoja na wajane au wagane ama wake na waume zake mtangaze mali zenu kabla hamjaingia madarakani kama sheria inavyotaka vinginevyo ni kukaribisha anguko lenu na taifa kwa ujumla. SIUNGI MKONO HUU UPUMBAVU HATA KIDOGO. viongozi wanaongezeka kila siku na mahitaji yao yatabebwa na masikini kila siku du. Familia za marais zipo sita, zitahitaji magari 18, wapishi 6, madereva 18 watunza bustani 6, madobi 6, walinzi 12 nyumba za kifahari 6 diplomat pasport kwa mke na mume kwa gharama za walala hoi plus monthly allowance isiyopungua milioni 30 (YES MAKE FAMILIA YA MWINYI, KIKWETE NA SAMIA wote mme na mke watalipwa huku MAGUFULI, NYERERE NA MKAPA familia zao zikipotea monthy alowance na lump sum ya wazee wao kupitia kwa mama[hii ni tofauti na mafao ya mzee] tuelewane hapa ) kila famili. Gharama za mafuta ya magari matatu pamoja na service za gari zote 3. Bado familia za makamu wa rais, waziri mkuu NW mkuu, spika wa bunge, na jaji mkuu. WTF
Naomba waendelee kujisahau hivi hivi.
 
Back
Top Bottom