rodney jr.
Senior Member
- Feb 12, 2014
- 139
- 71
Ningekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ingekuwa ni marufuku kwa mtu yeyote yule kuendesha gari yoyote ile akiwa peke yake ndani ya gari.
Haiwezekani mtu atoke posta akiwa kwenye gari yenye siti nne na nyingine zina siti sita halafu mtu yupo peke yake wakati kuna watu wanasubiri daladala masaa mawili mpaka matatu.
Najua ni gari yako, ulinunua kwa pesa zako na hakuna aliyekuchangia ila kwa hilo mngeniona mchungu.
Najua nitakuwa navunja sheria ila nisingewaacha. Ukaguzi wa magari hayo private kwa watu wanaotoka posta na kariakoo ungekuwa unafanyikia Jangwani kwa wanaenda Ubungo, Ubalozi wa Ufaransa kwa wanaoenda Mwenge, kurasini kwa wanaoenda mbagala na temeke, UKIKUTWA UPO PEKE YAKO KWENYE GARI UNARUDISHWA POSTA KUBEBA WATU.
____________
UPDATE: Kama kumpa mtu lift unaogopa usalama wako basi hata gari ikikusumbua usiwaombe watu wakusukume maana huwajui hivyo itahatarisha usalama wako.
Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)
Kuna baba wa rafiki angu aliwapa lifti watu kutoka mwenge-posta..yule mzee aliweka pc chini ya kiti..na alipakia watu wazima na heshima zao..anasema anafika ofisini tu....kwishney...laptop imeondoka na doc zote za muhimu..haijulikani nani aliondoka nayo kati ya wale aliowapa lift... So watch out kwa dunia ya sasa mkuu. Mwanadamu ni zaidi ya umfikiriavyo..
Last edited by a moderator: