Kwa wazazi: hii kitu inamsaidia nini mtoto?

Nayachukia sana haya makitu, watoto wengi wa uswahilini ndio wanaovishwa, mkononi au kiunoni. Nayahusisha na imani haba..
 
Naomba kuuliza kwa wale wenye watoto.
angalia picha hapo chini.
Mkono wa huyo mtoto amevalishwa kamba nyeusi.
Nimewaona watoto wengi hasa uswahilini huvishwa hiyo kitu.
Ni urembo kwa mtoto au hiyo kitu inamaana gani kwa mtoto?
NB: Pichani ni msanii wa bongo fleva na producer maarufu, Bob Junior akiwa na familia yake.
Hapo ilikuwa katika hafla ya kufuturu. ni hafla ya kiimani zaidi.
Kikwetu wanasema kuwa mtoto anaona kila kitu ambacho sisi watu wazima hatuwezi kiviona, mfano mtoto ni rahisi kumuona mchawi na mwanga ndiyo maana mtoto anaweza akastuka akalia sana usijue analilia nini kumbe ameona vitu vya kumuogopesha.So wataalam wanasema kuwa mtoto akifungwa kitu cheusi mkononi ama mguuni hawezi tena kuona vitu vya kutisha, kuna wengine wananawawekea jani utosini.
Kuna siku moja nilikuwa nasafiri na basi kutokea Tarime kwenda Mwanza, tulipofika Msoma akapanda babu mmoja kwenye basi, hapo hapo mtoto mmoja kama wa miezi 2 akaanza kulia sana.Mama yake alibembeleza sana lakini wapi,basi jamaa mmoja kwenye gari akamwambia kuwa mtoto anatakiwa afungwe kitambaa cheusi mkononi eti kwa kuwa ameona kitu kisicho cha kawaida lakini yule mama akagoma.Tulipofika maeneo ya Lamadi yule mzee akashuka na hapo hapo mtoto akanyamaza,basi kuna mama mmoja akasema kuwa yule babu aliepandia Musoma alikuwa mganga wa kienyeji so ndiyo maana mtoto alilia sana maana kuna vitu unusual ameviona.Kwa hiyo kwa kifupi kufunga kitambaa cheusi ni imani inayoendana na kumlinda mtoto asione mambo ya kutisha
 
Ni imani zaidi. Kuna baadhi ya wahindi pia wanavaa kama kamba mkononi. Inawezekana ni kwa sababu zinazofanana?
 
Kikwetu wanasema kuwa mtoto anaona kila kitu ambacho sisi watu wazima hatuwezi kiviona, mfano mtoto ni rahisi kumuona mchawi na mwanga ndiyo maana mtoto anaweza akastuka akalia sana usijue analilia nini kumbe ameona vitu vya kumuogopesha.So wataalam wanasema kuwa mtoto akifungwa kitu cheusi mkononi ama mguuni hawezi tena kuona vitu vya kutisha, kuna wengine wananawawekea jani utosini.
Kuna siku moja nilikuwa nasafiri na basi kutokea Tarime kwenda Mwanza, tulipofika Msoma akapanda babu mmoja kwenye basi, hapo hapo mtoto mmoja kama wa miezi 2 akaanza kulia sana.Mama yake alibembeleza sana lakini wapi,basi jamaa mmoja kwenye gari akamwambia kuwa mtoto anatakiwa afungwe kitambaa cheusi mkononi eti kwa kuwa ameona kitu kisicho cha kawaida lakini yule mama akagoma.Tulipofika maeneo ya Lamadi yule mzee akashuka na hapo hapo mtoto akanyamaza,basi kuna mama mmoja akasema kuwa yule babu aliepandia Musoma alikuwa mganga wa kienyeji so ndiyo maana mtoto alilia sana maana kuna vitu unusual ameviona.Kwa hiyo kwa kifupi kufunga kitambaa cheusi ni imani inayoendana na kumlinda mtoto asione mambo ya kutisha

Kwa hiyo we unaunga mkono just to know manake id yako na ulichoandika nimestuka.Ni miungu tu .
 
Ni vile hatujuani tu humu ndani mtakuwa mmewawekea watt wenu mpaka za miguuni sio mikononi tu vikisachiwa kwenye nepi mpaka kiunoni zipo acheni kushauka hapa wakati wenyewe mmezivaa
 
Hiyo inakutambulisha imani, upeo wa kiakili pamoja na level ya elimu ya hao wazazi wa wenye watoto wa namna hiyo.
 
Woote mnaosema hapo mliishavaa,sasa mgeuliza wazee walikuwa na maana gani.

Na utakuta hapa wengine kwa waganga wa kienyeji ndio kwao.
Hivi hapa nani hajawahi kwenda kwa mganga wa kienyeji na kwanini asiende Hospital.

Mle kwenye kitambaa kunakuwa kunafungwa Mvuje,na ule mvuje humsaidia mtoto asiweze kustukastuka na pia kukumbwa na mapepo ya njiani.Mbali na yote pia huwa na dua mbalimbali.
Na inaonekana upeo wa watu kwenye maandiko hata ya vitabu hapa ni mdogo sana.Haya mambo yapo tangu wakati wa mitume wote.

Unajua wengine tukifika mjini ndio tunaona kila kitu,ila tukianza kuumwa tu haoo vijijini.


Mie nipo Tofauti na nyie,kwamba naamini baathi ya mambo huwa ni sahihi na sio kila kitu kubeza.
Hapa mkulizwa faida ya Shanga kiunoni kwa mwanamke wooote mtajibu kwa jibu moja tu linalofana na moja kwa moja kwenye Ngono,maana ndio our first impression in mind.Wakati in deep kuna vitu vingi ndani yake.

neno hilo,ukitaka meza usipoweza tafuna.
 
hv na zile kambakamba zivaliwazo mikononi na wahindi si kama hizi kamba nyeusi kwa huyo mtoto?
Its just a belief to gods but not the living God.
 
Hiyo inakutambulisha imani, upeo wa kiakili pamoja na level ya elimu ya hao wazazi wa wenye watoto wa namna hiyo.
Jamani Imani za watu tusiziingilie kwani kuna vitu vingi tu tunavifanya na watoto wetu wanapona.
Ntamuunga mkono bornagain hii mila ipo sana kwa waarabu, kuwa mtoto mchanga huwa anaona vitu km majini nk
Mila za kwenu Wabantu mtoto akilia mfululizo ni kwamba lazima akapewe jina la babu yake na ndio ataacha kulia mara kwa mara
Kuna ile imani kuwa mtoto akipiga qwiki (kutoa hewa tumboni kma alikunywa maziwa au maji) wakina mama humfungia uzi wanaoufumua katika nguo yoyote waliyombebea na kuipakaza mate kisha kumbandika katika paji la uso hapo kwikwi huisha
Mtoto kuwa na kitovu kilichotokeza ni kumvisha mshipi wenye shilingi (sarafu) juu ya hicho kitovu na huisha
Mkojo kuuma hasa mtoto wa kiume ambaye si mchanga ni kumpa maji uliyoyapoozea kwa kutumbukiza kaa la moto na akinywa maji hayo hupona kabisa hayo maumivu
Mtoto kuumwa na tumba hata la kuharisha ni kumtafunia au kutwanga majani ya mpera na kumpa anywe majiyake au atafune na kufyonza,
Ugonjwa wa athma, ni kumpa mtoto avute moshi wa majani ya maua fulani yaliyokaushwa na moshi huo ukiingia kwenye mapafu, huondoa majimaji (Bubles) ndani ya mapafu zinazosababisha kifua kubana wakati wa kupumua.
Kwa hiyo hizi imani za kamba nyeusi ni za wenzetu Waarabu na mm nazisikia na kuziona
Ila zet ngoja na Mzizi Mkavu atusaidie km mm nimuongo atanisahihisha
lakini samahani kwa kuwadanganya
 
Last edited by a moderator:
Ni utamaduni wetu Africa ingawa hata wengine pia wanao. Ni imani ambayo kwangu naogopa sema ni ya kishirikina kwasababu sababu/(reasoning) bado zitakuwa ni falsafa za kuletwa na weupe, sawa tu na mtu anayeogesha maiti, kuvisha nguo za gharama saana, jeneza bei kubwa saana....ni ubatili mtupu ingawa naogopa kusema hivyo! Hata enzi za mitume na manabii kuna mila na desturi zimeandikwa lakini hazikuwa dini eg. baada ya siku 3 walitoka kwenda kupaka mafuta (perfumed oil) maiti.......ukiitizama haijatulia sana, lakini ilikuwa ni tamaduni za watu wale. Upande wa pili ndio kuna mila.....lukuki. Kama huyo dogo akiugua anapelekwa hosp kwa ukawaida hiyo kwangu haina noma, hata mimi nimevaa kiunoni na...Tuheshimu mambo ya watu wengine
 
Kwahiyo mkuu upeo wa hao wazaazi unauelezea vp? wapo katika kundi gani?
Nikianza na imani, imani yao haba hasa kwa kuamini Mungu aliyemleta huyo mtoto hapa duniani hana uwezo wa kumkuza na kumlinda. Sasa moja kwa moja wanaamua kuwa na imani kwa miungu ya kisanamu.
Upeo, kwa kweli ni mdogo mno. Wanakuwa awawezi kujitawala basi na shaka kabisa wanatumia akili za kuchanganywa na za wengine.
Elimu, sina shaka kabisa ni level ya Secondary na kushuka chini.
 
Back
Top Bottom