Muhimu! Wazazi mnaolea watoto bila baba zao

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,439
Ndugu zangu,

Jamii ya sasa imejaa watoto wanaolelewa na mzazi mmoja hasa akina mama. Hili tatizo kwa kiasi kikubwa linasababishwa na sisi wanaume wa zama hizi ambao kuzaa holela na kutelekeza mama na mtoto imekuwa kama kitu cha kawaida na tunakipa sababu rahisi tu.

Sasa hapa leo nataka nitoe angalizo muhimu kwa wanawake hasa single mothers. Mara nyingi baada ya kutelekezwa au kukosa maelewano na mzazi wa kiume kuna hatua mnachukua kwa hasira bila kujua matokeo yake.

Nimekuwa inspired kuandika hili baada ya kuona video ya mtoto wa msanii maarufu Anti Ezekiel akijiita jina la baba wa kufikia badala ya baba yake halisi. Sasa nisikieni kwa makini.

Mtoto ukizaa na mtu tambua hiyo damu inatambulika ni ya ukoo huo sio na Mungu tu, bali hadi miungu/mizimu ya huko kwenye ukoo. Vita yenu wazazi haiondoi uhalali wa hiyo bloodline na mambo ya kwao. Juhudi za makusudi kushiriki kumtenga mtoto na huko ni hatari labda wawe wamemkataa wenyewe lakini sio kupishana tu wazazi.

Hatari zaidi ni wewe mwanamke kumpakia mtoto chuki na baba yake, mtoto kwa kutokujua akashiriki kwa vitendo au kukiri kwa kinywa kumkataa baba yake halali huku baba yake akimtambua kama mwanae! Tofauti zenu za kimaisha ikiwemo matunzo hafifu tambua mstari hatari kuvuka ni kukana damu!

Sasa sikieni dada na mama zangu, mara nyingi hawa watoto wanaweza kukua vizuri ila wakishapata ufahamu wa kutosha hutokea matatizo ya ajabu! Utahangaika makanisa yote hutoboi na hapo sasa ni mpaka mtoto kwasababu ni mtu mzima mtumishi au Mungu mwenyewe amuonyeshe aina ya toba ya kufanya.

Hizi shida mara nyingi hutegemea na hizo familia za baba zao. Kama ni familia yenye miungu/ mizimu mikali ni hatari zaidi! Na ikitokea mtoto ni wa kiume ndio balaa maana ni wa urithi.

Kwenye ugomvi wowote upo mstari usivuke, usihusishe mtoto na kumuingiza kwenye maagano yatayokuja kumgharimu kuyafuta akipata ufahamu. Kama mzazi mwenzio amekutelekeza hizo hatua unazochukua hazitaleta ugali wala ada.

Mtegemee Mungu, kabidhi mtoto kwa Mungu aliyekupa then songambele hapo madhara ya huo uovu utabakia kwa baba pekee na familia yake kama imehusika.

Mwenye masikio na asikie! Mambo ya ukoo! Mizimu/miungu yapo. Wewe zaa alafu uenende bila kuchunga hatua zako na mtoto uone huko mbele msalaba utaobeba.
 
Mkuu umesema sahihi lakini kikubwa;

Wanaume tujifunze kuwajibika kwa kulea watoto wetu.

Maana kuna wimbi limeibuka la Sisi Wanaume kutelekeza familia zetu kisa kushindwa na maisha hivyo kuwafanya WaMama/ Dada kuwa Single Mamas huku wakilea watoto peke yao.

Ukiweza kulea na kutunza familia yako huyo mtoto/Watoto wataendelea kutumia majina yako na kuendelea kukuheshimu kama Baba yao
 
Waafrika na mizimu Sasa..
Yapo mzee na kama huna experience yake pole sana . Usishangae ya Israel na Palestina, ardhi ni picha iliyoko mbele ila nyuma ni bloodline tu.

Mtoto hasa wa kiume lazima ufahamu asili ya kwenu na ufike pia. Sio kwaajili ya kutambika bali ni wajibu wa msingi ambao kizazi hiki wengi hawafundishwi. Ukienda na kutambika ni vile wewe unavyoamini lakini zipo njia za Kikristo za kushiriki baraka za ardhi yenu ambayo ndio asili yako.
 
Yapo mzee na kama huna experience yake pole sana . Usishangae ya Israel na Palestina, ardhi ni picha iliyoko mbele ila nyuma ni bloodline tu.

Mtoto hasa wa kiume lazima ufahamu asili ya kwenu na ufike pia. Sio kwaajili ya kutambika bali ni wajibu wa msingi ambao kizazi hiki wengi hawafundishwi. Ukienda na kutambika ni vile wewe unavyoamini lakini zipo njia za Kikristo za kushiriki baraka za ardhi yenu ambayo ndio asili yako.
Siamini haya mambo babu!.. hakuna cha mizimu Wala mashetani..
Kwanza mizimu inatokea wapi..?
Haya mambo yapo kuwashika watua akili tu.. naomba unijibu chanzo cha mizimu na kazi yake..?
 
Siamini haya mambo babu!.. hakuna cha mizimu Wala mashetani..
Kwanza mizimu inatokea wapi..?
Haya mambo yapo kuwashika watua akili tu.. naomba unijibu chanzo cha mizimu na kazi yake..?
Niliwahi kuwa na mawazo kama yako ila ndugu yangu africa ni mwendo wa mizimu tu,mizimu ndio saints kwa english,RC huwa wanasali au kuomba dua fulani kupitia watakatifu,utasikia mtakatifu mdukuziiii utuombeeee.
Like wise mizimu inaweza kukuharibia au kukunusuru na mabalaa
 
Ndugu zangu,

Jamii ya sasa imejaa watoto wanaolelewa na mzazi mmoja hasa akina mama. Hili tatizo kwa kiasi kikubwa linasababishwa na sisi wanaume wa zama hizi ambao kuzaa holela na kutelekeza mama na mtoto imekuwa kama kitu cha kawaida na tunakipa sababu rahisi tu.

Sasa hapa leo nataka nitoe angalizo muhimu kwa wanawake hasa single mothers. Mara nyingi baada ya kutelekezwa au kukosa maelewano na mzazi wa kiume kuna hatua mnachukua kwa hasira bila kujua matokeo yake.

Nimekuwa inspired kuandika hili baada ya kuona video ya mtoto wa msanii maarufu Anti Ezekiel akijiita jina la baba wa kufikia badala ya baba yake halisi. Sasa nisikieni kwa makini.

Mtoto ukizaa na mtu tambua hiyo damu inatambulika ni ya ukoo huo sio na Mungu tu, bali hadi miungu/mizimu ya huko kwenye ukoo. Vita yenu wazazi haiondoi uhalali wa hiyo bloodline na mambo ya kwao. Juhudi za makusudi kushiriki kumtenga mtoto na huko ni hatari labda wawe wamemkataa wenyewe lakini sio kupishana tu wazazi.

Hatari zaidi ni wewe mwanamke kumpakia mtoto chuki na baba yake, mtoto kwa kutokujua akashiriki kwa vitendo au kukiri kwa kinywa kumkataa baba yake halali huku baba yake akimtambua kama mwanae! Tofauti zenu za kimaisha ikiwemo matunzo hafifu tambua mstari hatari kuvuka ni kukana damu!

Sasa sikieni dada na mama zangu, mara nyingi hawa watoto wanaweza kukua vizuri ila wakishapata ufahamu wa kutosha hutokea matatizo ya ajabu! Utahangaika makanisa yote hutoboi na hapo sasa ni mpaka mtoto kwasababu ni mtu mzima mtumishi au Mungu mwenyewe amuonyeshe aina ya toba ya kufanya.

Hizi shida mara nyingi hutegemea na hizo familia za baba zao. Kama ni familia yenye miungu/ mizimu mikali ni hatari zaidi! Na ikitokea mtoto ni wa kiume ndio balaa maana ni wa urithi.

Kwenye ugomvi wowote upo mstari usivuke, usihusishe mtoto na kumuingiza kwenye maagano yatayokuja kumgharimu kuyafuta akipata ufahamu. Kama mzazi mwenzio amekutelekeza hizo hatua unazochukua hazitaleta ugali wala ada.

Mtegemee Mungu, kabidhi mtoto kwa Mungu aliyekupa then songambele hapo madhara ya huo uovu utabakia kwa baba pekee na familia yake kama imehusika.

Mwenye masikio na asikie! Mambo ya ukoo! Mizimu/miungu yapo. Wewe zaa alafu uenende bila kuchunga hatua zako na mtoto uone huko mbele msalaba utaobeba.
Msiache kutoa masomo km haya inasaidia sana...
 
Niliwahi kuwa na mawazo kama yako ila ndugu yangu africa ni mwendo wa mizimu tu,mizimu ndio saints kwa english,RC huwa wanasali au kuomba dua fulani kupitia watakatifu,utasikia mtakatifu mdukuziiii utuombeeee.
Like wise mizimu inaweza kukuharibia au kukunusuru na mabalaa
🤣🤣 Hichi nacho ni kituko chengine cha haja!
 
NAzifaham scenario 2 kuhusu ulichoandika japo zenyewe hazihusian na u single mother but african taboos

1. Dada etu mkubwa mzee alimzaa nje. Yule mama yetu mdogo alikua mkorofi sana wakatibuana na mzee akataka kumtenga mtoto na mzee akampelekaga Tukuyu huko Mbeya kwa bibi yake ili tu mzee asiwe na access nae. Akakaa sana huko mpaka kakawa kakubwa around 4 years. Ghafla mtoto akaanzaga kuumwa sana yan anaumwa pima hospital zoote hakuna kitu. Baada ya kesi kuwa nzito ikabid mama mtu amshirikishe mzee kuwa hali ya mtoto ni mbaya amekua akisumbuliwa na magonjwa ambayo hayaeleweki .mzee akamwambia mlete town tujaribu hospital za huku lakin nita deal nae mwenyewe. Bas sister akaletwa town. Alikua hamjui kabisaa mzee. Siku alipoletwa town yuko hoiiii , kitendo tu cha kuonyeshwa mzee (baba yake) na kuambiwa huyu ndio baba, yan ilikua ni pale pale mtoto akasimama mbio kamkimbilia mzee ,akawa mzima kabisaaaa na habar ya hospital ikaishia hapo akawa mzima na akaanza kuishi home na mzee na mke wa ndoa wa mzee toka that time.

2. Scenario hii inamuhusu mshkaji wangu.
Brother ake na mshkaji alioa mke na wakazaa mtoto wao wa kwanza wa kiume. Huyu brother ni mtoto wa kwanza kwao na kiutamaduni wa kwao jina la mtoto waliyemzaa lilipaswa kutolewa na babu yake (baba ake na huyu brother) ila wao wakaleta umjini wakapiga chini hii kitu. Baada ya muda flan mtoto kukua akaanza kupata shida za maradhi mazito ya mara kwa mara wakahangaika nae sana bila mafanikio. Habari hii ikamfikia babu mtu huko mkoa wa Mara, na yeye haraka akawaambia mleteni mtoto nyumbani, walipofika babu mtu anambeba mjukuu wake akamwambia (mtoto mdogo hata hajui kuongea) "wewe jina lako si hili(akaataja jina alilopewa na wazazi wake), bali kuanzia leo wewe jina lako ni hili(akampa jina lake yeye (alikua anaitwa Funga)".

Mchezo ukaishia hapo dogo akapona, hakuna dawa ilitumika wala maombi yaliofanywa.

Mila za kiafrika zipo na ziko effective tuu ni vile tumeamua kuzidharau ndio maana hata ma grand nao wameamua kutupuuza tunabaki tuna hangaika
 
Mtoa mada yuko sahihi kabisa kwa mtizamo wangu. Lkn endapo baba ndiye mkaidi (aliyesababisha kutengana na mtoto/watoto wake) na hakuonesha juhudi zozote za kujirudi itakuwa kinyume chake. Mizimu hiyohiyo ya kwao itamtesa kwa kutelekeza damu yake.
 
NAzifaham scenario 2 kuhusu ulichoandika japo zenyewe hazihusian na u single mother but african taboos

1. Dada etu mkubwa mzee alimzaa nje. Yule mama yetu mdogo alikua mkorofi sana wakatibuana na mzee akataka kumtenga mtoto na mzee akampelekaga Tukuyu huko Mbeya kwa bibi yake ili tu mzee asiwe na access nae. Akakaa sana huko mpaka kakawa kakubwa around 4 years. Ghafla mtoto akaanzaga kuumwa sana yan anaumwa pima hospital zoote hakuna kitu. Baada ya kesi kuwa nzito ikabid mama mtu amshirikishe mzee kuwa hali ya mtoto ni mbaya amekua akisumbuliwa na magonjwa ambayo hayaeleweki .mzee akamwambia mlete town tujaribu hospital za huku lakin nita deal nae mwenyewe. Bas sister akaletwa town. Alikua hamjui kabisaa mzee. Siku alipoletwa town yuko hoiiii , kitendo tu cha kuonyeshwa mzee (baba yake) na kuambiwa huyu ndio baba, yan ilikua ni pale pale mtoto akasimama mbio kamkimbilia mzee ,akawa mzima kabisaaaa na habar ya hospital ikaishia hapo akawa mzima na akaanza kuishi home na mzee na mke wa ndoa wa mzee toka that time.

2. Scenario hii inamuhusu mshkaji wangu.
Brother ake na mshkaji alioa mke na wakazaa mtoto wao wa kwanza wa kiume. Huyu brother ni mtoto wa kwanza kwao na kiutamaduni wa kwao jina la mtoto waliyemzaa lilipaswa kutolewa na babu yake (baba ake na huyu brother) ila wao wakaleta umjini wakapiga chini hii kitu. Baada ya muda flan mtoto kukua akaanza kupata shida za maradhi mazito ya mara kwa mara wakahangaika nae sana bila mafanikio. Habari hii ikamfikia babu mtu huko mkoa wa Mara, na yeye haraka akawaambia mleteni mtoto nyumbani, walipofika babu mtu anambeba mjukuu wake akamwambia (mtoto mdogo hata hajui kuongea) "wewe jina lako si hili(akaataja jina alilopewa na wazazi wake), bali kuanzia leo wewe jina lako ni hili(akampa jina lake yeye (alikua anaitwa Funga)".

Mchezo ukaishia hapo dogo akapona, hakuna dawa ilitumika wala maombi yaliofanywa.

Mila za kiafrika zipo na ziko effective tuu ni vile tumeamua kuzidharau ndio maana hata ma grand nao wameamua kutupuuza tunabaki tuna hangaika
Asante kwa mifano hai. Hakuna issues complicated kudeal nazo kama zinahusisha mambo ya ukoo na bloodline! Ndio maana ukifata ma real exorcist kabla ya huduma lazima wakuhoji kwa kina sana kama daktari anavyohoji mgonjwa.
 
Mtoa mada yuko sahihi kabisa kwa mtizamo wangu. Lkn endapo baba ndiye mkaidi (aliyesababisha kutengana na mtoto/watoto wake) na hakuonesha juhudi zozote za kujirudi itakuwa kinyume chake. Mizimu hiyohiyo ya kwao itamtesa kwa kutelekeza damu yake.
Kabisa, ukifanya uovu Mungu anajitenga na kuacha miungu/mizimu n.k kushughulika na wewe hadi ujisahihishe kwa usahihi
 
Back
Top Bottom