Gwanggaeto the Great
JF-Expert Member
- Apr 14, 2018
- 817
- 1,772
Hii drama kila sehemu inasifiwa.daebak, muda huu ndio nimemaliza kuingalia hii drama episode mbili za wiki hii (mpira wa ulaya nimeusamehe kwa siku ya leo). zimebaki episode 4 ili hii drama imalizike na sijajua kama kutakuwepo na uwezekano wa seson 2 japokuwa ningelipenda uwepo muendelezo wake kwa sababu nahisi stori ndio kwanza inachangamka, binafsi nimezoea episode 16 zenye kubeba wastani wa dakika 70 - 90 kupitia tvN tofauti na hiki kituko wanachotufanyia SBS cha kutuonuyesha lisali moja lilisilotimia kwa kila episode kana kwamba hii drama imebeba episode 20.
jessica lee ni mwanadada ambaye ana uwezo wa kusurvive kwenye hali yoyote ya hatari haijalishi anapambana na simba akiwa peke yake ndani ya chumba kisichokuwa na mlango, harakati zake kama lobbyist za kuhakikisha kampuni yake inajiweka ukaribu na wenye nguvu kubwa za kuwaongoza walalahoi zinanikumbusha drama ya lobbyist ambapo alikuwemo mwanadada lobbyist anayekwenda kwa jina la Maria ambaye na yeye hakuona tabu kuutumia mwili wake kama chambo kwa lengo la kuu la kumteka mteja wake kifikra na kimaamuzi.
Ameshinda dili la kusupply ndege za kijeshi lakini bado anainyemelea tenda ya mafuta ambayo waziri mkuu amemwambia raisi tayari anaye partner hivyo basi haitokuwa jambo rahisi kumuingiza jessica lee kwenye project ya mafuta.
je huyo partner aliyemlenga waziri mkuu ni nani?
nina wasiwasi huenda partner akawa ni Edward Park na kampuni yake ya dynamic ambayo pia ni kampuni pinzani, hivyo basi kuna uwezekano waziri mkuu naye ana upande wake anaoshirikiana nao kama ilivyo kwa bwana Yun aliyejiweka karibu na jessica.
halafu kuna issue ya slush fund: hii serikali yote hakuna aliyemsafi kuanzia raisi mwenyewe hadi muajiriwa anayesafisha choo cha raisi wote ni baba mmoja na mma mmoja. Nje ya drama serikali kama hizi zimejaa zaidi ndani ya bara letu la afrika ndio maana vita ya ufisadi na uwajibikaji inaendelea kuwa ni ngumu haijalishi teknolojia ya sasa imepevuka na sababu kubwa ni kukosekana kwa uwazi hususani juu ya matumizi ya serikali, mara nyingi mafisadi na madikteta hujificha kwenye mwamvuli wa kuwapambania wananchi ili wapate stahiki zao na wakati huo huo kwenye nafsi zao wakiongozwa zaidi na ubaya wa kutamani kupora kila kilicho mbele yao.
inaonekana dhahiri secretary Yun ndiye engine kuu ya muheshimiwa raisi kwenye mission zote chafu zinazomuhusu muheshimiwa aliyejificha kwenye kivuli cha utakatifu, kinachokwenda kutokezea baadae ni watatu hao kusalitiana hapo mbeleni kama itatokezea kuvuja kwa siri ya kuwepo kwa mlolongo wa rushwa kwenye dili la kununua ndege za kivita.
mpaka sasa mtu pekee mwenye uhakika wa kusurvive kwenye hili pambano licha ya kuwa naye ni mchafu wa matendo na si mwengine ni waziri mkuu kwa sababu ana ushahidi mwingi sana unaomuhusu muheshimiwa raisi pamoja na waziri wa ulinzi (tukumbuke mwanzoni drama waziri wa ulinzi alihongwa rushwa tofauti na bi jessica ikiwemo rushwa ya ngono na picha zilimfikia muheshimiwa raisi)
heshima kwake bwana judge kwa kuchelewesha kesi licha ya kupokea oda ya kuimaliza kesi ile kutoka chief justice ambaye alikwisha pokea amri kutoka kwa muhimili mchafu (jessica na crew yake)
kama raisi ndiye bingwa wa kupokea rushwa kutoka kwa matajiri unadhani rushwa hii itaweza kuondoshwa kwa mikono yake hususani kwa kuwatishia vyanzo hivi vya chini vya utumishi vinavyoendelea kupokea mshahara wa chini baada ya makato na kodi?
rushwa haiwezi kuondolewa kwa rushwa.
ufisadi hauwezi kuondolewa na mfumo fisadi.
ni sawa na mtengenezaji pombe kuweka tangazo la kukataza ummah uliopotea kunywa pombe.
dah! kadri ninavyomuona my love from joseon hwang bo ra moyo wangu unakatika vipande vipande kama samaki. Wengine wanajileta kwangu nakuniambia kwa nini usinipende mimi daemusin matokeo yake nabaki kuwajibu.
kama wewe kama wewe upendwe nini ?
siwaumbo si wa nywele si wa ghuyuni,
mbele zero nyuma hakujulikani
baraka ya wanja, kujipakaza machoni
kwenye visura wewe huko hisabuni
Zunguka bongo waone kila mahala
figure zao za kupigiwa mfano
sio zumbukuku na shepu ya penseli
hivyo unadhani kwa yakini watakiwa kwa uzuri gani hasa wa kujizuzua
sibasi tu sibasi tu sibasi tu
View attachment 1246653
next: my country drama ndipo nilale.
sitaki niamke kesho nikiwa na fikra za kuangalia korean drama haijalishi ni kwa nusu saa.