Umeicheki IRIS? Hizi ni facts 10 usizozijua kuhusu series hiyo

Krikichino

JF-Expert Member
Oct 5, 2019
651
1,098
Nakumbuka mara ya kwanza kuona tamthiliya ya Iris ilikuwa ni ITV pale mwaka 2013 kama sio 2014 kipindi hicho hata smartphone sina.

Nilivyoiona tu mara ya kwanza sijui ilikuwaje lakini tangu hapo sikuacha kuifatilia mpaka episodes zote 20 zilivyoisha.Nakumbuka nilikuwa nachelewa kulala siku alhamisi na ijumaa saa 22:00 mpk 23:00 ili tu nione Kim Hyun Jun ameishia wapi.

Kiukweli Iris ndio imenifanya mpaka leo mimi niwe shabiki wa Korean dramas na ndio maana leo nimeamua kuweka hapa facts 10 ambazo inawezekana huzifahamu kuhusiana na drama hii ambayo iligharimu takribani 16M USD ili kuikamilisha :

1. Kim Hyun Jun ambaye ndo alikuwa "steringi" kwenye series alikuwa analipwa takriban Tzs milioni 200 kwa episode moja. Tukumbuke episode zilikuwa 20! Huku Choi Seung Hui yeye alilipwa takriban Tzs million 40 per episode!

2. IRIS Ilitengenezwa na Taewon Entertainment moja ya kampuni kubwa sana nchini Korea. Na IRIS haikushirikisha kituo chochote cha TV wakati inatengenezwa. Producers walitaka chaneli kama SBS, MBC na KBS 2 vishindane dau atayeshinda ndie atakayepata haki ya kuonesha IRIS. Of course KBS 2 ndio ilishinda na IRIS ikaanza kuoneshwa October 14 mwaka 2009.

3. IRIS pia shooting ilifanyika kwenye nchi tatu. Walianza kushoot Japan pale Akita March 10 2009 kisha wakaenda Budapest huko Hungary ( rejea episode ya 2) na kumalizia principal photography huko Seoul South Korea.

4. Kim Tae Hee ambaye kwenye series ameigiza kama Choi Seung Hui ilibidi ajifunze martial arts kidogo ili aweze kufit kwenye series hasa kwenye upande wa action hii scenes. Pia kwenye series waigizaji walikuwa wanafanya Stunts zao wenyewe.

5.Bajeti ya series nzima ilikuwa ni takribani 16M USD. Kupelekea Iris kuwa mojawapo ya tamthiliya za kikorea zilizogharimu mkwanja mrefu.

6. IRIS pia imezalisha watoto au series nyingine kama IRIS 2 starring Jang hyuk ambao ni muendelezo wa IRIS 1 japo actors ni tofauti na ATHENA starring Soo Ae. Ukiachana na hizo series mbili pia kuna movie inaitwa IRIS THE MOVIE ambayo hii ina utofauti kidogo na series.

7. Wengi wanasema IRIS imeisha vibaya maana haijulikani nani alimuua Kim Hyeonjun. Lakini aliyemuua Kim ni AGENT RAY sniper hatari sana kutokea kwenye kikundi cha Iris. IRIS 2 imeelezea vizuri tukio hilo.


8. Kuna ile scene kwenye Episode ya 19 ambapo Kim Hyun Jun na Choi Seung Hui wanapigana na magaidi wanaotaka kulipua Seoul, barabarani. Sasa ile scene ilifanya barabara ya Seoul karibu na Gwanghamun plaza ifungwe kwa masaa 12. Kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa 1 usiku ili tu kushoot hiyo scene.

Serikali ya Seoul City ilivyoulizwa ikasema imeruhusu jambo hilo kwani itasaidia kukuza utalii hapo mjini Seoul.

9. Katika hali ya kushangaza kidogo kituo cha TV kiitwacho TBS kutokea Japan kilinunua haki za kuonesha series hiyo kwa USD Million 4.2.

Baada ya kununua series hiyo ili ionyeshwe huko Japan ilifanya dubbing huku waigizaji wakubwa huko Japan kama Tatsuya wakiingiza sauti zao na ofcourse walivyoanza tu kuionesha ratings za watazamaji zilipanda sana.

10. IRIS ni mojawapo kati ya series ambazo ziliangaliwa sana huko Korea ikiwa na audience share ya wastani 30% kitu ambacho kipindi kile ilikuwa ni nadra sana kutokea

Yes! Najua uzi ulikuwa mrefu kidogo ila hayo ni machache tu kwa leo.



Wasaalam.
828302c9fb4b710127ecd4a9fb734647.jpg
b67c0ab651163bbd750555c38d68e888--irises-k-drama.jpg
AAAABZ-PL74Ag9VJeKoCTYx-KlasyWulBe0RAIbBuvTpPfbw8cVhRWuksmVPd7UrfGBQTgIlzhXSQ1_DlvAKWSFytcvDxc...jpg
leebyunghun_0512_10.jpg
Iris%2BKorean%2BDrama%2B2.jpg
 
Mara ya kwanza kucheki Korea series ilikuwa Athena,sikudhani kama kutakuwa na series kali kama hiyo.

Ila huo mzigo wa Iris ni ilikuwa ni shida nyingine,kuanzia sterling hadi adui wana balaa.Mzee baba Baek San,Kim Sun Hwa,Jin Sa Woo,Choi Seung Hee na yule Dr kichaa wa kule NSS bado kule North Korea na Security Service yao na yule boss wao,mtaalam wa machare kama yote vile.

Love story kali,action kali,matumizi ya akili makubwa mno. Huwezi kupredict kinachofuata.

Nilikuwaga naangalia na sister angu home,kuna kipindi alikuwa analia sana jinsi Kim Hyun Jan alivyokuwa anateseka na maisha yake ya kusalitiwa.

Sema wazee mapenzi ni matamu sana na yana nguvu mno. Ila vipi TISS wetu sijui wapo kama vile kwenye recruitment hadi kufanya kazi. Na IRIS wa nchi yetu sijui ni wakina nani.

Kwa nini na sisi tusiandike movie kali kama ile moja tu.Kila siku tuna deal na mapenzi tu. At least vipepeo weusi The Bold alitupa utamu kunoga.

IRIS itabaki kuwa IRIS tu,ila Athena na yenyewe ni shida nyingine wazee.
Hahaha mkuu uliipenda sana hii sema hapa kwetu bado kuna vitu vingi vya kwenye system havijakaa sawa
 
IRIS hata me nakumbuka niliiangalia mda ila kuna series moja ya kikorea nmeiangalia n balaa inaitwa SIX FLYING DRAGONS yan kila nikiangalia huwa siichok walah
Nitaitafuta hiyo, IRIS hata niiangalie mara trilioni bado inanihamasisha kuangalia tena.

Ni bonge la action movie isiyopungua kiu ya kuitamani kuiangalia wakati wote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom