beefinjector
JF-Expert Member
- Jul 23, 2009
- 2,762
- 2,736
Mkuu hatubishani tunaeleweshana!! Ndio thamani halisi ya jamvi hili , kuna tofauti kati ya documentary na conspiracy theories japo zote huonekana kama zinafanana , documentary ni factual story zilizowahi kutokea kunakuwa na msimuliaji ambaye anakuunganisha na wahusika wa stori kwa kuwahoji au kuchukua mawazo yao, mara zote ,yeye huwa hayuko upande wowote wa story .nia na madhumuni ni kukupa wewe msikilizaji uelewa wa jambo linalozungumziwa bila kukuchagulia upande..
conspiracy theories nazo huwa ni fact zilizowahi kutokea , tofauti ni kuwa msimuliaji huwa ana upande anaoelemea na wahusika wanaohojiwa au kutoa maoni huwa wahusika kamili wa tukio, ambao hutoa maoni ya kushabihiana na mawazo ya msimuliaji ,malengo hasa ni kukuaminisha mambo ambayo mtengenezaji au msimuliaji anadhani yako hivyo.
mkuu mara nyingi documentary sources zake huwa ni news tv channels science findings and the likes , bbc cnn discovery nat geo history chanell e.tc na unaweza kutrace mpaka siku zilipokuwa aired kwa mara ya kwanza ,conspiracy mara nyingi hutokea kwa kikundi au mtu fulani ambaye anaopingana na serikali yake kwa sababu kadhaa, nyingi ya theories zinakufikia kwa namna ya dvd ,kwa sababu sources zake sio reliable,mfano michael moore ni maarufu sana amerika kwa upande wa conspirancy.
Unaonekana hujui tofauti ya documentary na conspiracy theory. Documentary ni filamu ambayo inaongelea mambo ambayo sio hadithi (non-fiction) ili kuhifadhi historia au kuelimisha. Conspiracy theory ni pendekezo (explanatory proposition) kuwa mtu au kikundi cha watu fulani wamepanga na kutekeleza kwa siri mpango haramu ambao umesababisha madhara.
Conspiracy theory inaweza kuwa katika mfumo wa kitabu, documentary n.k. Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa conspiracy theory ikiwa kwenye mfumo wa kitabu hakitaitwa kitabu? Sababu ulizotoa hapo juu kuwa eti documentary za conspiracy theory huwa hazionyeshwi kwenye TV ni upuuzi kwa sababu mimi nishaziona nyingi tu mfano kifo cha Rais JFK. Si kila documentary lazima ionyeshwe kwenye TV.
Documentary pekee ya Michael Moore ambayo unaweza kusema kuwa ni conspiracy theory labda Fahrenheit 9/11 lakini nyingine zote ( nimeziona zoote) ni factual wala hakuna conspiracy yoyote.