"‘Kwa Usalama wa Taifa" kichaka cha kunyima uhuru wa kutoa taarifa na kuhabarishwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,016
9,885
Prof Chachage S Chachage ni kati ya watu waliokuwa mstari wa mbele kwenye kutetea uhuru wa kuongea, kupata taarifa na kuhabarishwa. Suala hili liko wazi kwenye kazi zake ikiwemo Makuadi wa Soko Huria na kazi nyinginezo ambazo ameonesha uhitaji wake wa kuwa na uhuru wa kutoa na kupata taarifa.

Katika kazi yake “Uchambuzi wa Sera, Uongozi na Maslahi ya Watanzania” Ukurasa wa 219 ameandika hivi

Hapa kwetu (Tanzania) Katiba na sheria zinatungwa ili kuwadhibiti au kuwakomoa wananchi. Na hapa sheria zinatumika kuwalinda wale walioko madarakani ili waweze kuendelea kuwepo na kuzuia au kupinga Mawazo au misimamo tofauti isijitutumue.

Katika hali kama hii, utawala wa misingi ya kisheria hauna maana yeyote, na ndiyo maana katiba inaweza kubadilika kila wakati kwa visingizio vya ‘Usalama wa taifa na mshikamano’.”


Wataalamu mbalimbali wanatambua umuhimu wa usalama wa Taifa, ndio sababu ya kujadili namna ya kujadili usalama wa Taifa bila kuathiri uhuru wa kujieleza na haki ya kupata taarifa. Mwaka 1995 wataalamu walikuja na The Johannesburg Principles on National Security, Freedom of Expression and Access to Information ambayo Tanzania ni moja kati ya nchi iliyosaini makubaliano hayo kuwa itaheshimu.

Johannesburg Principles zinalenga kushughulikia usawa kati ya usalama wa taifa na haki ya uhuru wa kujieleza na habari kwa kutoa mwongozo na viwango kwa serikali kufuata. Mipango hii inasisitiza umuhimu wa kulinda haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na uhuru wa kujieleza na habari, wakati pia inatambua haja ya usalama wa taifa. Uhuru wa kujieleza na habari ni muhimu kwa jamii ya kidemokrasia na ni muhimu kwa maendeleo na ustawi wake.

Makubaliano yanasisitiza kutungwa kwa sheria zenye wigo mdogo wa usalama wa Taifa na kuhakikisha mahitaji muhimu ya utawala wa sheria. Inatambulika kwamba baadhi ya ukiukaji wa haki za binadamu na uhuru hupewa kigezo kulinda usalama wa taifa. Hivyo misingi hii inawakataza serikali kutumia usalama wa taifa kama kisingizio cha vikwazo visivyostahili kwa uhuru wa kujieleza na habari.

Kwa ujumla, Mipango ya Johannesburg inalenga kuleta usawa kati ya usalama wa taifa na haki ya uhuru wa kujieleza na habari kwa kukuza kutambuliwa kwa wigo mdogo wa vikwazo na haja ya ulinzi wa kisheria na mahakama kwa uhuru huu.
 
Prof Chachage S Chachage ni kati ya watu waliokuwa mstari wa mbele kwenye kutetea uhuru wa kuongea, kupata taarifa na kuhabarishwa. Suala hili liko wazi kwenye kazi zake ikiwemo Makuadi wa Soko Huria na kazi nyinginezo ambazo ameonesha uhitaji wake wa kuwa na uhuru wa kutoa na kupata taarifa.

Katika kazi yake “Uchambuzi wa Sera, Uongozi na Maslahi ya Watanzania” Ukurasa wa 219 ameandika hivi

Hapa kwetu (Tanzania) Katiba na sheria zinatungwa ili kuwadhibiti au kuwakomoa wananchi. Na hapa sheria zinatumika kuwalinda wale walioko madarakani ili waweze kuendelea kuwepo na kuzuia au kupinga Mawazo au misimamo tofauti isijitutumue.

Katika hali kama hii, utawala wa misingi ya kisheria hauna maana yeyote, na ndiyo maana katiba inaweza kubadilika kila wakati kwa visingizio vya ‘Usalama wa taifa na mshikamano’.”


Wataalamu mbalimbali wanatambua umuhimu wa usalama wa Taifa, ndio sababu ya kujadili namna ya kujadili usalama wa Taifa bila kuathiri uhuru wa kujieleza na haki ya kupata taarifa. Mwaka 1995 wataalamu walikuja na The Johannesburg Principles on National Security, Freedom of Expression and Access to Information ambayo Tanzania ni moja kati ya nchi iliyosaini makubaliano hayo kuwa itaheshimu.

Johannesburg Principles zinalenga kushughulikia usawa kati ya usalama wa taifa na haki ya uhuru wa kujieleza na habari kwa kutoa mwongozo na viwango kwa serikali kufuata. Mipango hii inasisitiza umuhimu wa kulinda haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na uhuru wa kujieleza na habari, wakati pia inatambua haja ya usalama wa taifa. Uhuru wa kujieleza na habari ni muhimu kwa jamii ya kidemokrasia na ni muhimu kwa maendeleo na ustawi wake.

Makubaliano yanasisitiza kutungwa kwa sheria zenye wigo mdogo wa usalama wa Taifa na kuhakikisha mahitaji muhimu ya utawala wa sheria. Inatambulika kwamba baadhi ya ukiukaji wa haki za binadamu na uhuru hupewa kigezo kulinda usalama wa taifa. Hivyo misingi hii inawakataza serikali kutumia usalama wa taifa kama kisingizio cha vikwazo visivyostahili kwa uhuru wa kujieleza na habari.

Kwa ujumla, Mipango ya Johannesburg inalenga kuleta usawa kati ya usalama wa taifa na haki ya uhuru wa kujieleza na habari kwa kukuza kutambuliwa kwa wigo mdogo wa vikwazo na haja ya ulinzi wa kisheria na mahakama kwa uhuru huu.
Ni dhahiri ccm haijali lolote, hainadiliki na lengo lake ni kuwadidimiza WaTz. Mambo ya kutoheshimu Katiba, kubadili hovyo kwa maslahi hewa Katiba na sheria na kudhibiti Uhuru wa WaTz, yalishatokea kipindi hadi kupelekea hilo tamko la J'berg 1995 na mpaka leo, wameshika kasi kwenda kinyume cha tamko hilo.
 
Kuna hatari ya viongozi wetu kuwa nyuma ya wakati na kuishi nyakati za giza.

Siku zote unapaswa kuwa mbele ya muda ya watu unawaongoza.
 
Ni dhahiri ccm haijali lolote, hainadiliki na lengo lake ni kuwadidimiza WaTz. Mambo ya kutoheshimu Katiba, kubadili hovyo kwa maslahi hewa Katiba na sheria na kudhibiti Uhuru wa WaTz, yalishatokea kipindi hadi kupelekea hilo tamko la J'berg 1995 na mpaka leo, wameshika kasi kwenda kinyume cha tamko hilo.
Kaazi kweli kweli
 
Mie naamini kama IDARA YA USALAMA WA TAIFA INGEKUWA INAWAJIBIKA JAPO KWA 40% nchi ingekuwa salama na imara kiuchumi, kiasiasa, jamii, kiulinzi na kiutamaduni ila idara imekuwa kitengo kuteka na kutesa raia wema. TISS EBU JARIBUNI KUJISAHIHISHA JAMANI!!!!!!!!!!
 
Kuna wakati huwa nashindwa kabisa kuwatofautisha hao jamaa na wale vijana wa uvccm. Maana naona wamejikita zaidi kwenye kulinda maslahi ya chama na watu wake, kuliko hata ya Taifa.
 
Mie naamini kama IDARA YA USALAMA WA TAIFA INGEKUWA INAWAJIBIKA JAPO KWA 40% nchi ingekuwa salama na imara kiuchumi, kiasiasa, jamii, kiulinzi na kiutamaduni ila idara imekuwa kitengo kuteka na kutesa raia wema. TISS EBU JARIBUNI KUJISAHIHISHA JAMANI!!!!!!!!!!
Hivi watakuelewa kweli?Je, hawatakuweka kwenye orodha yao ya maadui zao ambao ni "Most Wanted."
 
Back
Top Bottom