Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

You should have gone to specsavers, CCM chama cha weledi, kwa taarifa yako rasimu hii ni kuwakaanga Mi-Chadema kwa mafuta yao, Leo CCM imezaliwa upya na imeonyesha kukomaa kwake kisiasa.
 
Hata mimi nimepita hapo nikakuta hakuna lolote zaidi ya design ya kitoto kitoto.

Cha kushangaza hata waandishi wa habari wetu baada ya kusema hivyo, wangeangalia haraka kupata uhakika na kumrudia na swali lakini wameamini maneno yake peke yake.

Kupata soft copy au kuwekwa kwenye website yao usishangae itachukua weeks.

Bora asingesema kuwa "Rasimu ya Katiba itapatikana kwenye tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya www.katiba.go.tz" unless alikuwa na uhakika kuwa tayari ilikuwa pale.
 
Na wewe mbona una chuki za kijinga?

Alicholeta manyerere au kilichotolewa na Tume ya warioba ni dibaji na Contents ambazo inshort kama unaishughulisha akili yako unaelewa wazi kile kilichomo.

Kumbuka hili siyo gazeti bali ni thread ambayo Members wengine wataiongezea nyama na kutoa mitazamo yao, nashangaa wewe umemkomalia mleta hoja tu vipi Jombaaa!!

Hi rasimu ya katiba ni kifo cha CCM na sipati picha uko mbele itakuwaje ili CCM waikubali maana wao wapo wengi kwenye vyombo vya maamuzi, hili ni pigo takatifu kwa CCM na wengi walidhani Warioba atakuwa mnafki wa kuibeba CCM kumbe sivyo na hajawasahau kitendo walichomfanyia swahiba yake Salim Ahmed Salim.

Kwa Wazee wenye busara kuna umri mtu akifika anaka kuacha legacy kwenye society na Warioba nadhani hili ndio lengo lake na anajuwa ana miaka mingi zaidi ya kuishi Duniani.

kichwa chako na wewe hakiko sawa kifo cha ccm kipo wapi kwani ccm ndiyo wanasera ya majimbo? rasmu imepiga marufuku sera ya majimbo ambayo ni sera ya chadema lakini kunawatu walionyimwa uhuru ndani ya chadema watagombea nafasi binafsi mfano zito,shibuda na wengine halafu maadili ya ya viongozi wa chadema wote hawana maadili hiki nacho ni kitanzi kwao na sijui nani atagombea bara,zanzibar,na shirikisho.kwazi kwao.
 
Kitakachotokea sasa ni kwamba wale watu ambao wana mitandao yao binafsi wakishindwa CCM, au wasiporidhika na utendaji wa CCM, sasa watagombea kama wagombea binafsi na kuishia kugawa kura za upinzani.
Yaani waondolewe CCM kwa kuonewa then wagawe kura za upinzani how!. Imagine Lowassa afanyiwe mizengwe halafu agombee kama mgombea binafsi unategemea kura za CCM zitabaki zilezile.
 
Mkuu Manyerere,
Kwa mawazo yangu mimi, hili suala la mgombea binafsi lina madhara zaidi kwa upinzani kuliko kwa CCM.

Watu wengi wazuri waliokuwa wanashindwa CCM kwa kuonewa au kwa njama zingine walikuwa wanakimbilia upinzani. Hata wale waliokuwa wanabaki bado wapenzi wao wengi walikuwa wanagoma kumpigia kura mgombea wa CCM na kuishia
kuchagua upinzani.

Kitakachotokea sasa ni kwamba wale watu ambao wana mitandao yao binafsi wakishindwa CCM, au wasiporidhika na utendaji wa CCM, sasa watagombea kama wagombea binafsi na kuishia kugawa kura za upinzani.

Imagine hili lingelikuwepo 2010, huenda leo hii Msigwa na Lema wasingelikuwa wabunge. Watu wengi wa Mwakalebela walimpigia kura Msigwa na hivyo hivyo watu wengi wa Mrema kule Arusha walimpigia kura Lema.

CCM wanalijua hili na ndio maana katika vyama ni wao walipendekeza hili la mgombea huru ingawaje wao walitaka litumike kuanzia chini mpaka ubunge.
Mkuu, ina maana tume haikupendekeza independent candidate kwa chaguzi zote? Mbona Manyerere Jackton ameonyesha kama mapendekezo yako mpaka vitongoji.
 
CCM ni sawa na nyoka bila kumponda kichwa kabisa hafi,hii ni rasimu inaenda kupita kwenye mabaraza ya katiba na bunge la katiba ambapo ccm tayari wameshapenyeza watu wao so lazima tujiandae kuwakabili kwenye hatua hizo wasije kujipenyeza na kuharibu hii rasimu, naamini swala la serikali tatu hawatalikubali, mgombea binafsi hawataki na tume huru hawataki !! kwa vyovyote kazi bado pevu mbele yetu!!

Ndo naingia jf nakuta comment hii hapa. Nimeipenda. Napitia nyingine pia na natamani nione rasm hiyo.
 
Chama kina utaratibu wa kukua na kubadilisha mifumo yake inayotumika katika kujiendesha lakini kwa sasa pamoja na kele zote hizi za upinzani bado CCM ni imara labda huko baadae.

mkuu upinzani ndiyo basi pengine wajipange baada ya miaka kumi ijayo tena.
 
Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

CCM siyo wajinga wa kujimaliza kirahisi hivyo. They know what they are doing. Kama unapima upepo wa ushabiki wa watu kwenye katiba haina tatizo. Naamini kabisa CCM watakuwa wamefanyia kazi 'Scenarios' zote ambazo wewe unaona zinaweza kuwamaliza na kubuni mbinu za kuikinga. Kama mwandishi ulitakiwa kutafikiti kwa nini CCM wameamua vile na madhara yake wamejipangaje kuyakabili?

Hivi unafikiri kuachia dola ni kazi rahisi sana, tena Afrikaaaaaaaaaa?
 
Lowassa, Membe, Mwakyembe, Magufuli, Sitta, Sumaye wote ndani ya kinyang'anyiro hata bila kupitia mwavuli wa CCM.
 
Kifo cha CCM kinatokea wapi kwenye hii rasimu?.

Kama chagizo ni independent candidate, CCM ndiyo walipendekeza hili kwenye mapendekezo yao kwa tume.

Kwa serikali tatu, CCM hawakuwa na jinsi na katika kolido za kiutawala, kwao hili ni ushindi kwa sababu mzimu wa Mwl. Nyerere wamepata njia ya kuutua.

Tume ya uchaguzi kuunganishwa na msajiri wa vyama lilikuwa ni obvious lingetokea kulingana na demokrasia za nchi nyingi za Africa.

Kama ni kufa basi lazima itakuwa imekufa zamani lakini siyo kwa hili kwa sababu haya karibia yote ni mapendekezo ya CCM.

Mbona watu mnajivua uelewa au memory?
Hebu tuombe radhi kwanza kabla hujajibu maswali nyangu machache.......

Sera ya serikali 3 ni sera ya chama gani?

hoja ya mgombea binafsi muhasisi ni nani na ninani amekuwa akiipinga kwa nguvu zote mpaka kuitisha Court of appeal full bench?

Ni Ilani ya chama gani Tanzania ambayo ilani yake iliahidi Mahakama ya kadhi? je ahadi hiyo ilitekelezwa? na kama haijatekelezwa kwenye rasimu ya katiba mpya ipo Mahakama ya kadhi? je CCM ina gutts za kuomba kura za waislamu mwaka 2015? wait n see.
 
Yaani waondolewe CCM kwa kuonewa then wagawe kura za upinzani how!. Imagine Lowassa afanyiwe mizengwe halafu agombee kama mgombea binafsi unategemea kura za CCM zitabaki zilezile.

hizo ni ndoto za mchana kwani lowasa ni nani,lowasa ni maarufu ndani ya ccm na akitoka nje siyo maarufu tena asikudanganye kuwa yeye ni maarufu nje ya ccm huko ni kujifariji tu.
 
Mleta mada mwenyewe kaileta kinafiki tu na ndiyo anapata mashambulizi, badala aongelee rasmu yenyewe anaanza kutaja vyama, mbona hakusema rasimu hiyo itakifufua chama gani kama itaua CCM.

Mkuu, pamoja na ushabiki wa kivyama, ni ukweli usiopingika kuwa, CCM kama chama tawala kimekuwa mstari wa mbele kupinga wagombea binafsi. Rejea kesi ya Mch. Mtikila dhidi ya Mwanasheria mkuu wa serikali ya TZ, na hukumu yake na nini kilifuatia kuhusu utekelezaji wa hukumu hiyo? Ndiyo maana huyu bwana pamoja na mambo mengine ya rasimu ya katiba amekuja na mada hiyo ambayo kwake ameona ni ya muhimu. Sasa iwapo kwako si ya muhimu basi achana nayo, siyo lazima kuchangia kwa sababu tu ya ushabiki wa kisiasa.
 
Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

Jackton

Habari za tangu Dodoma? Naomba nikwambie kitu kimoja tu "the devil lies in the details".

Lakini pia, CCM kama chama cha siasa kimeshakufa.

Natumaini utakuwa umenielewa...
 
Wewe nawe unajifanya Mwandishi lakini uandishi wako uko shallow kupita maelezo.

Nyie ndio maripota wa matukio halafu mnajiita wandishi.

Na wewe si utoe maoni kuhusu hicho alichokileta? Au kwa sababu ni mwandish ulitaka alete makala kuubwa ya rasimu yote,acha hizo chuki binafs toa maon kwa hicho alicholeta baaasi,hayo ya uandish tafuta gazet lake usome!
 
Bora asingesema kuwa "Rasimu ya Katiba itapatikana kwenye tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya www.katiba.go.tz" unless alikuwa na uhakika kuwa tayari ilikuwa pale.
Kwa lugha ya kisheria Mzee Warioba amedanganya!!.

Inawezekana alipata briefing kama rasimu iko live and kicking kumbe hata hawajaiweka. Kama unavyojua wazee wetu wala wahajishughulishi na IT, na kwa sababu hii wala hakuhakiki kuona kama inafanya kazi.

Acha tusubiri.
 
Jacton lete issue zote tuzidiscuss sasa wewe umeleta moja tuu na kuitolea tamati.
Usikute kuna kipengele kinasema usiwe ulishawaikuwa mwanachama wa chama chochote au kushika nyazifa serikalini!
 
Hebu tuombe radhi kwanza kabla hujajibu maswali nyangu machache.......

Sera ya serikali 3 ni sera ya chama gani?

hoja ya mgombea binafsi muhasisi ni nani na ninani amekuwa akiipinga kwa nguvu zote mpaka kuitisha Court of appeal full bench?

Ni Ilani ya chama gani Tanzania ambayo ilani yake iliahidi Mahakama ya kadhi? je ahadi hiyo ilitekelezwa? na kama haijatekelezwa kwenye rasimu ya katiba mpya ipo Mahakama ya kadhi? je CCM ina gutts za kuomba kura za waislamu mwaka 2015? wait n see.

kwa hiyo wewe unataka kutuambia kuwa ccm walipaswa kuilazimisha tume kufuata matakwa ya ccm au ilikuwa ni tume huru na huu uhuru siimepewa na serikali ya ccm,au umelala usingizia au wewe na chama chako utaomba kura kwa kushinikiza mahakama ya kazi acha kupandikiza udini hutaweza kupotosha watu wanaakili zao.
 
CCM siyo wajinga wa kujimaliza kirahisi hivyo. They know what they are doing. Kama unapima upepo wa ushabiki wa watu kwenye katiba haina tatizo. Naamini kabisa CCM watakuwa wamefanyia kazi 'Scenarios' zote ambazo wewe unaona zinaweza kuwamaliza na kubuni mbinu za kuikinga. Kama mwandishi ulitakiwa kutafikiti kwa nini CCM wameamua vile na madhara yake wamejipangaje kuyakabili?

Hivi unafikiri kuachia dola ni kazi rahisi sana, tena Afrikaaaaaaaaaa?
CCM sio kwamba wamependa iwe hivyo wamelazimika wakubali yaishe, Waryoba hakuwa rahisi kuyumbishwa kama mlivyotegemea.
 
Umeongea pointi nzuri sana. Nasikia huyu ni mwandishi wa habari? Ni kweli? Kama ni kweli basi kazi tunayo Watanzania, kuwa na wanahabar wa upeo wa huyu...

Yeye kaleta mjadala kuhus hicho kipengele kimoja tu cha mgombea binafs nyie mlitaka aandike nini? Kwa sabab hapa ni kwenye jukwaa la mijadala,yeye ana option ya kuleta makala au short and clear kama alivyofanya sasa? Au mlitaka aandike makala jamaa!
 
Back
Top Bottom