Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

Udikteta wa CHADEMA kwisha
 
Unadhani watu wote wanaweza kuwa ulipo wewe muda wote!?
Na wewe mbona una chuki za kijinga?

Alicholeta manyerere au kilichotolewa na Tume ya warioba ni dibaji na Contents ambazo inshort kama unaishughulisha akili yako unaelewa wazi kile kilichomo.

Kumbuka hili siyo gazeti bali ni thread ambayo Members wengine wataiongezea nyama na kutoa mitazamo yao, nashangaa wewe umemkomalia mleta hoja tu vipi Jombaaa!!

Hi rasimu ya katiba ni kifo cha CCM na sipati picha uko mbele itakuwaje ili CCM waikubali maana wao wapo wengi kwenye vyombo vya maamuzi, hili ni pigo takatifu kwa CCM na wengi walidhani Warioba atakuwa mnafki wa kuibeba CCM kumbe sivyo na hajawasahau kitendo walichomfanyia swahiba yake Salim Ahmed Salim.

Kwa Wazee wenye busara kuna umri mtu akifika anaka kuacha legacy kwenye society na Warioba nadhani hili ndio lengo lake na anajuwa ana miaka mingi zaidi ya kuishi Duniani.
 
jamani huo nimfano sio katiba kwaiyo msipende kukulupuka .CCM hawaogopi mgombea binafsi kwani nutural ya ranzania mgombea binafsi ni lazima ashindwe.hata kuwa na pesa za kufanya campeni na hata akiwa nazo huyo mtu nia atari hivyo awezi kupitishwa na NEC hizo pesa zitakua zimetoka nje.
KIDUMU CHAMA CHAMA PINDUZI......
 
Umeongea pointi nzuri sana. Nasikia huyu ni mwandishi wa habari? Ni kweli? Kama ni kweli basi kazi tunayo Watanzania, kuwa na wanahabar wa upeo wa huyu...
Mkuu, tangu mwanzo wa uzi huu umekuwa ukimshambulia mleta mada. Ni dhahiri kabisa una chuki za kitoto na huyu bwana. Katika kuchangia mada si muhimu kujua nani kaileta, bali inahusu nini. Au ni kanuni ipi ya JF inayosema ili u-post mada ndani yake ni lazima uwe mwandishi wa habari? Hukulazimishwa kuisoma na wala kuchangia. Tunaofuatilia mada za JF, tunataka kusoma michango ya GTs na inapobidi kuchangia na siyo unachoki-post wewe, ambacho kinakera sana na kutuondolea umakini wa JF. Samahani kama nimekukera.
 
Mkuu Manyerere,
Kwa mawazo yangu mimi, hili suala la mgombea binafsi lina madhara zaidi kwa upinzani kuliko kwa CCM.

Watu wengi wazuri waliokuwa wanashindwa CCM kwa kuonewa au kwa njama zingine walikuwa wanakimbilia upinzani. Hata wale waliokuwa wanabaki bado wapenzi wao wengi walikuwa wanagoma kumpigia kura mgombea wa CCM na kuishia
kuchagua upinzani.

Kitakachotokea sasa ni kwamba wale watu ambao wana mitandao yao binafsi wakishindwa CCM, au wasiporidhika na utendaji wa CCM, sasa watagombea kama wagombea binafsi na kuishia kugawa kura za upinzani.

Imagine hili lingelikuwepo 2010, huenda leo hii Msigwa na Lema wasingelikuwa wabunge. Watu wengi wa Mwakalebela walimpigia kura Msigwa na hivyo hivyo watu wengi wa Mrema kule Arusha walimpigia kura Lema.

CCM wanalijua hili na ndio maana katika vyama ni wao walipendekeza hili la mgombea huru ingawaje wao walitaka litumike kuanzia chini mpaka ubunge.

Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.
 
Na wewe mbona una chuki za kijinga?

Alicholeta manyerere au kilichotolewa na Tume ya warioba ni dibaji na Contents ambazo inshort kama unaishughulisha akili yako unaelewa wazi kile kilichomo.

Kumbuka hili siyo gazeti bali ni thread ambayo Members wengine wataiongezea nyama na kutoa mitazamo yao, nashangaa wewe umemkomalia mleta hoja tu vipi Jombaaa!!

Hi rasimu ya katiba ni kifo cha CCM na sipati picha uko mbele itakuwaje ili CCM waikubali maana wao wapo wengi kwenye vyombo vya maamuzi, hili ni pigo takatifu kwa CCM na wengi walidhani Warioba atakuwa mnafki wa kuibeba CCM kumbe sivyo na hajawasahau kitendo walichomfanyia swahiba yake Salim Ahmed Salim.

Kwa Wazee wenye busara kuna umri mtu akifika anaka kuacha legacy kwenye society na Warioba nadhani hili ndio lengo lake na anajuwa ana miaka mingi zaidi ya kuishi Duniani.
Nimeelezea pale nilipom-quote EMT.
 
Manyerere nnavokujua wewe ulivyo gamba afu unakuja na mawazo haya Kuna kitu unafurahia kwa kutufunga chadema macho kwa kutumia kioo.
 
Tanzania kwa maswala ya IT bado nyuma sana.

Tume ya Warioba pamoja na kutengewa mabilioni ya pesa, lakini wanashindwa hata kuajiri mtu/kampuni full time katika kuweka documents muhimu kama rasimu kwenye website yao ili wananchi waisome.

Kwenye presentation yake amesema "Rasimu ya Katiba itapatikana kwenye tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya www.katiba.go.tz"

Lakini hakuna chochote kwenye hiyo tovuti. Hapa pana summary tuu ya alichoongelea: https://dl.dropboxusercontent.com/u/92908476/Speech/Hotuba%20ya%20Warioba,%20Rasimu%20ya%20Katiba%20Mpya,%20June%203,%202013.pdf
 
Kifo cha CCM kinatokea wapi kwenye hii rasimu?.

Kama chagizo ni independent candidate, CCM ndiyo walipendekeza hili kwenye mapendekezo yao kwa tume.

Kwa serikali tatu, CCM hawakuwa na jinsi na katika kolido za kiutawala, kwao hili ni ushindi kwa sababu mzimu wa Mwl. Nyerere wamepata njia ya kuutua.

Tume ya uchaguzi kuunganishwa na msajiri wa vyama lilikuwa ni obvious lingetokea kulingana na demokrasia za nchi nyingi za Africa.

Kama ni kufa basi lazima itakuwa imekufa zamani lakini siyo kwa hili kwa sababu haya karibia yote ni mapendekezo ya CCM.

Mbona watu mnajivua uelewa au memory?
 
Mr Manyerere Kengele ya Ng'ombe inafukuza wanyama ila ndege za Mwarabu zinawafutia wanyama,
 
Hakuna cha kushabikia....mabaraza ya Katiba na Bunge la Katiba ndo yataamua mwisho wa Katiba..humu mote CCM ipo na ina majority!!yanayoenda kuiumiza CCM hayatakubalika!..Ni sawa na uwe na ndoto ya kupata watoto mapacha,Ultra Sound ikupe majibu ya mapacha..lakn miscarriage kwa mke ifute ndoto za mapacha...Mabaraza ya Katiba yaliyojaa makada wa CCM Yatawauwa mapacha wa ndoto zetu
 
Mkuu, tangu mwanzo wa uzi huu umekuwa ukimshambulia mleta mada. Ni dhahiri kabisa una chuki za kitoto na huyu bwana. Katika kuchangia mada si muhimu kujua nani kaileta, bali inahusu nini. Au ni kanuni ipi ya JF inayosema ili u-post mada ndani yake ni lazima uwe mwandishi wa habari? Hukulazimishwa kuisoma na wala kuchangia. Tunaofuatilia mada za JF, tunataka kusoma michango ya GTs na inapobidi kuchangia na siyo unachoki-post wewe, ambacho kinakera sana na kutuondolea umakini wa JF. Samahani kama nimekukera.

Mleta mada mwenyewe kaileta kinafiki tu na ndiyo anapata mashambulizi, badala aongelee rasmu yenyewe anaanza kutaja vyama, mbona hakusema rasimu hiyo itakifufua chama gani kama itaua CCM.
 
Hakuna cha kushabikia....mabaraza ya Katiba na Bunge la Katiba ndo yataamua mwisho wa Katiba..humu mote CCM ipo na ina majority!!yanayoenda kuiumiza CCM hayatakubalika!..Ni sawa na uwe na ndoto ya kupata watoto mapacha,Ultra Sound ikupe majibu ya mapacha..lakn miscarriage kwa mke ifute ndoto za mapacha...Mabaraza ya Katiba yaliyojaa makada wa CCM Yatawauwa mapacha wa ndoto zetu

Hofu tu hakuna lolote hapo
 
Chama kina utaratibu wa kukua na kubadilisha mifumo yake inayotumika katika kujiendesha lakini kwa sasa pamoja na kele zote hizi za upinzani bado CCM ni imara labda huko baadae.
 
Kwenye presentation yake amesema "Rasimu ya Katiba itapatikana kwenye tovuti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya www.katiba.go.tz"

Lakini hakuna chochote kwenye hiyo tovuti. Hapa pana summary tuu ya alichoongelea: https://dl.dropboxusercontent.com/u/92908476/Speech/Hotuba%20ya%20Warioba,%20Rasimu%20ya%20Katiba%20Mpya,%20June%203,%202013.pdf
Hata mimi nimepita hapo nikakuta hakuna lolote zaidi ya design ya kitoto kitoto.

Cha kushangaza hata waandishi wa habari wetu baada ya kusema hivyo, wangeangalia haraka kupata uhakika na kumrudia na swali lakini wameamini maneno yake peke yake.

Kupata soft copy au kuwekwa kwenye website yao usishangae itachukua weeks.
 
Back
Top Bottom