Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Kwa rasimu hii, CCM inakufa

Sio uchambuzi wa mtu mwenye taaluma ya uandishi?
 
Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

vipi kama wataenda vyama vingine kama sasa.wanavyohama.?
..vipi kama hata wale walio katika vyama vingine..nao wakitumia FURSA hii ...kuwa wagombea binafsi?
huoni kwamba hii ni changamoto kwa vyama vyotee...?
 
Kwakweli na mimi ntacheka mwishoni

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Waungwana pamoja na Mapungufu aliyonayo Manyerere ( kama mlionayo nyinyi ) lakini kwenye hili ni kama mnamuonea tu , hebu twende kwenye ukweli , Wagombea binafsi Ni Tabu zaidi kwa CCM KULIKO CHAMA CHOCHOTE , bado sijajua pale palipo oza hadi Pakanuka ( TUME YA UCHAGUZI ) patakuwaje , nikipata ILE FULL TEXT nitajadili kwa upana .
 
Wewe umeshaisoma hiyo rasimu na kufanya analysis ya kila kipengele?

Kama umeisoma yote basi tugawie nakala yake ili na sisi tuisome na kuifanyia a comprehensive analysis.
Mkuu,
Nimeshangaa kwa muda mfupi mwenzetu ameshaisoma na kuichambua hiyo rasimu na tayari amekuja na uchambuzi wa mistari miwili. Kama kweli ameisoma nilitegemea pamoja na mambo mengine, afanye haya:

1. Atuwekee hiyo rasimu ili na sisi tuisome kisha twende sawa katika uchambuzi.
2. Atoe uchambuzi wa kina halafu na sisi tujadili kutokana na huo uchambuzi wake, badala ya kutuletea kikombe kilichojaa maji halafu anatuambia hii ni bahari. Na ukichukulia taaluma/kazi yake, nilitarajia aende mbali zaidi ya hicho alichokiandika.
 
Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.
CCM ni sawa na nyoka bila kumponda kichwa kabisa hafi,hii ni rasimu inaenda kupita kwenye mabaraza ya katiba na bunge la katiba ambapo ccm tayari wameshapenyeza watu wao so lazima tujiandae kuwakabili kwenye hatua hizo wasije kujipenyeza na kuharibu hii rasimu, naamini swala la serikali tatu hawatalikubali, mgombea binafsi hawataki na tume huru hawataki !! kwa vyovyote kazi bado pevu mbele yetu!!
 
Mkuu,
Nimeshangaa kwa muda mfupi mwenzetu ameshaisoma na kuichambua hiyo rasimu na tayari amekuja na uchambuzi wa mistari miwili. Kama kweli ameisoma nilitegemea pamoja na mambo mengine, afanye haya:

1. Atuwekee hiyo rasimu ili na sisi tuisome kisha twende sawa katika uchambuzi.
2. Atoe uchambuzi wa kina halafu na sisi tujadili kutokana na huo uchambuzi wake, badala ya kutuletea kikombe kilichojaa maji halafu anatuambia hii ni bahari. Na ukichukulia taaluma/kazi yake, nilitarajia aende mbali zaidi ya hicho alichokiandika.

TV zote kubwa nchini, pamoja na redio zinazosikika nchi nzima, zimetangaza. Hukuwa na muda wa kuambulia lolote?
 
Mkuu, hapa nilipo tayari ninayo maana nilikuwa Karimjee. Ina kurasa 133 za A4. Kimsingi ina vionjo vitamu sana. Nikipata soft copy naiweka hapa mara moja.

I reserve my comment until I read it in full, though nilishapinga mchakato mzima wa katiba mpya.
 
Waungwana pamoja na Mapungufu aliyonayo Manyerere ( kama mlionayo nyinyi ) lakini kwenye hili ni kama mnamuonea tu , hebu twende kwenye ukweli , Wagombea binafsi Ni Tabu zaidi kwa CCM KULIKO CHAMA CHOCHOTE , bado sijajua pale palipo oza hadi Pakanuka ( TUME YA UCHAGUZI ) patakuwaje , nikipata ILE FULL TEXT nitajadili kwa upana .
Hili halina ubishi, CCM ina mtihani mgumu katika hili lakini vile vile litaondoa rushwa iliyokuwa inazidi kuongeza katika chaguzi na teuzi zao. Watakao pelekwa kugombea, watakuwa wasafi kwa vile kule watapambana siyo tu na wagombea wengine kutoka kwenye vyama vingine bali pia na independent ambao wana uwezo kikazi na kifedha.

Kwa sasa swala la rushwa litaondoka ndani ya vyama automatically na litahamia kwenye chaguzi za nje ya vyama.

Kama hakutakuwa na sheria ya kudhibiti matumizi ya pesa kwenye kampeni, kuna hatari ya kuwepo kwa rushwa ya hali ya juu katika chaguzi na matumizo ya kukufuru ya pesa.
 
Niliwai kusema kuwa katika hali yoyote ile Katiba mpya inayoundwa haiwezi kukamilika kikamilifu na kutumika kwa uchaguzi mkuu wa 2015. sina hakika Katiba ya Tanganyika itaandaliwa lini kuweza kupata uongozi wa ksiasa na serkali katika upande huu wa muungano? Je tunaweza kuwa na serkali ya muungano na serkali ya upande mmoja (Zanzibar) bila kuwa na serkali ya upande mwingine? Nasubiri kuiona rasmu yenyewe.
 
Tatizo lako umekaa kichama zaidi sema hivi kwa katiba vyama vya siasa vyote vinachangamoto make mtu ataweza kujitathimini akiona anapendwa atakwenda kugombea yeye kama yeye kama yeye bila kutegemea chama.

Nashukuru kwa kuongea nilichataka kuchangia!!
 
Katiba ya ccm ipo kwenye mfuko wa shati wa KINAna anasubiri tu mudondoshe karata zenu wooote!! Halafu ndio anafuta ya kwake na kuidondosha!!!!! Ntawakumbusha mtakapo tawanyika kwa njia 16 (idadi ya vyama vyetu vya upinzani) hivi munaijua ccm?munamfahamu vizuri KINAna ?
 
Last edited by a moderator:
Manyerere kumbuka katiba hii imeteka hoja nyingi za chadema. kui- neutralize hoja ya mpinzani kisiasa ni ushindi pia.

Nchi za wenzetu Ulaya na marekani wanazitumia sana hoja za wapinzani ili wakati wa kampeni za uchaguzi wapinzani wawe na hoja chache dhidi ya chama tawala.
Pamoja na rasimu kuchukua hoja nyingi za Chadema unafikiri Chadema kimeishiwa hoja, mbona matatizo ya watanzania bado ni mengi tuu.
 
mim ningesuuzika kama kungeanzishwa mfumo wa majimbo,lakin kama itaendelea sera ya mikoa, ningependa wakuu wa mikoa na wilaya wapigiwe kura ili wawajibike kwa wanachi waliowachagua..
 
Rasimu inasemaje juu ya hoja ilokuwa ikitololewa na baadhi ya wananchi kwamba Mawaziri wasitokane na Wabunge? Mzee Warioba hajazungumza lolote juu ya hilo.
 
Wadau, wale tuliofuatilia vema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba, ni wazi kwamba kwa mapendekezo ya rasimu, CCM inakufa. Kuruhusu wagombea binafsi kuanzia Kitongoji hadi Taifa, kunatoa mwanya kwa wanaCCM wengi wasiopenda yanayoendelea ndani ya chama hicho, wawe huru kuamua pa kwenda. Aidha, mapendekezo haya ya Katiba mpya yanaleta utaifa zaidi ya u-chama. Sioni CCM watachomoka vipi.

Sijui wengine mna mtazamo gani.

binafsi nachotaka kuona zaidi ni rasimu katiba ya Tanzania bara (Tanganyika) na sioni kama hii ya jamhuri ya muungano pamoja na kuezelea yote hayo mazuri inawezekana ikawa ni kutaka watu wa concentrate kwenye katiba ambayo kwangu mimi sioni kama ni deal kubwa sana kubwa ulaji ukabaki vile vile kwenye serikali ya Tanzania bara ambako ndio kuna deal.

Kumbuka kwa kuwa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inapendekeza kuwa na serikali tatu, yaani ya zanzibar, ya Tanzania bara na ya Muungano ki msingi nataka nijue hiyo katiba ya Tanzania bara itakuwaje kwani ndio kwenye deal na ulaji mkubwa na inawezekana CCM wakawa ndio sehemu yao ya kupiga bao hapo.
 
Tanzania kwa maswala ya IT bado nyuma sana.

Tume ya Warioba pamoja na kutengewa mabilioni ya pesa, lakini wanashindwa hata kuajiri mtu/kampuni full time katika kuweka documents muhimu kama rasimu kwenye website yao ili wananchi waisome.

Wananchi tuna haki popote pale tulipo kuisoma rasimu ya katiba kwa wakati wowote ule kupitia website yao.

Yaani hata design ya website yao ni vichekesho tupu. Sijui kuna watu wamefisadi na kuajiri cheap web designer.

Kwa nchi hizi za wenzetu, baada tu ya kumaliza kuigawa hii document kwa press, ingekuwa tayari pia inapatikana kwenye website yao.

Ina maana kwa tulioko nje ya nchi itabidi tutembelee ofisi za ubalozi kuipata?

Why are they having website kama hawawezi kuweka document kama hii.
 
Back
Top Bottom